Imeandikwa na @swalehmawele
FT: Yanga 0 - 0 Tanzania Prisons

Plan ya kwanza kwa Tanzania Prisons ilikuwa kuzuia, plan ya pili ikawa kuzuia na plan ya tatu ikawa kushambulia, walichagua kwanza kubaki kwenye eneo lao zaidi, wacheze low block ili kuziba mianya ya Yanga kutengeneza nafasi kutokea kwenye flanks na eneo la kiungo.

Tanzania Prisons hawakuonyesha madhara katika lango la Yanga walipokuwa na mpira, walishambulia wakiwa na idadi ndogo ya wachezaji, zilitokea 1 v 3 au 2 v 5 nyingi, Yanga walipokonya mipira mingi na kuanzisha wao mashambulizi.

Kama unachagua kukaa zaidi kwenye eneo lako hakikisha unakuwa na usahihi wa pasi mnapokuwa na mpira, kasi na mcheze direct ili kuitumia mianya baada ya walinzi wa timu pinzani kusogea katika high line, Prisons hawakufanya hivyo, walipoteza mipira mingi kirahisi.

Mohamed Nabi alitaka zaidi bao kuliko perfomance, alichagua kubadilisha game plan katika kipindi cha pili, watumie mipira mirefu inayodondoka katika eneo la kumi na nane kisha washindane kwenye aerial balls, hata sub ya Makambo ilikuwa katika mpango huo kutokana na uwezo wake mkubwa wa kucheza mipira ya juu.

Labda kama namtazama tofauti, Saido Ntibazonkiza ameshuka kidogo kiwango chake, katika takriban mechi tano za mwisho hajacheza kama tunavyomjua.

Linapokuja swala la kuzuia na kutumia nguvu hii Prisons naifanyananisha na Burnley ya Uingereza, watakupa mechi hasa hata kama utashinda.

Jumanne Ninkaza, mwanaume wa shoka hasa, maana halisi ya defensive midfielder.

Nilisema katika analysis yangu kabla ya mechi hii kuanza, kama Prisons atafanikiwa kumzuia Yanga katika kipindi cha kwanza pengine akaokota alama, Prisons wamefanikiwa.