Makapuku Forum

Africa ni sehemu ya jehamu ukisema ukweli
 
Ligi bora hutoa washindani bora

Ligi ukiona mmoja anachuku mfululizo ujue ubora wa ligi ni mdogo sana

Na hilo inakubidi uangalie uwekezaji wa timu pinzan na huyo bingwa
 
FISTON Mayele alitoa ahadi mbili ambazo moja ilikuwa ni kuifunga Namungo FC ambayo ameikamilisha na ya pili ni ya kupachika bao katika mechi ya watani wa jadi, Yanga na Simba itakayochezwa Jumamosi kuanzia saa 11 jioni kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

Lakini, wakati watu wakisubiri kuona kama mshambuliaji huyo atatimiza ahadi hiyo au la, ameweka rekodi ambayo bila shaka upande wa pili wakiisikia hawawezi kumdharau mshambuliaji huyo na watalazimika kumuandalia ulinzi wa ziada ili asiwaletee madhara.

Rekodi hiyo ya Mayele ambayo sio taarifa nzuri kwa Simba kuelekea mechi baina yao Jumamosi ni ile ya kuhusika moja kwa moja na mabao saba katika michezo sita mfululizo ya Ligi Kuu ambayo Yanga imecheza kabla ya mchezo huo wa watani wa jadi.
 
MWAMUZI Ramadhan Kayoko amepewa kazi kuchezesha mchezo wa Kariakoo Derby kati ya Yanga na Simba utakaochezwa April 30, kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.
Kayoko atasimama katikati huku akisaidiwa na Frank Komba (Dar es Salaam), Mohamed Mkono (Tanga), wakati Elly Sasii (Dar es Salaam) atakuwa mwamuzi wa mezani.
 
LICHA ya kwamba mkataba wake unaelekea ukingoni huku akihusishwa na kurejea Azam, kipa namba moja wa Simba, Aishi Manula juzi usiku alitamka kauli ambayo ni wazi msimu ujao atakuwa Msimbazi.

Kipa huyo baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere wakitokea nchini Afrika Kusini walikotolewa na Orlando Pirates alisema; “Tuna kazi kubwa msimu ujao.”

“Binafsi naona tunapiga hatua kuanzia robo fainali ya kwanza mpaka ya tatu kuna maendeleo makubwa, kwa hiyo naona msimu ujao tunaweza tusiishie tulipoishia leo bali tukaanzia hapa,” alisema Manula ambaye habari za chinichini ni Azam walimwekea cheki mezani mwezi mmoja uliopita na wanamsikilizia yeye.
 
Mambo ya Usindusi utafanyeka hapa Auntie
( kwa sauti ya Zumaridi)
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…