Makapuku Forum

Makapuku Forum

Polisi Tanga wanamshikilia Mkazi mmoja wa Bwembwela Wilayani Muheza kwa tuhuma za kumjeruhi Elias Omari (55) kwa panga mpaka kupelekea kufariki dunia akidai kuwa amemuibia unga na dagaa.

RPC wa Tanga Safia Jongo ameithibitishia @ayotv_ tukio hilo na kusema chanzo ni ugomvi wa kugombania unga na dagaa uliopelekea wawili hao kupigana kwa kutumia mapanga na kusababisha kifo kwa mmoja wao.

Kamanda Jongo amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia April 17,2022 na kwamba Mtuhumiwa (30) alijeruhiwa pia katika ugomvi huo na kwa sasa yupo Hospitali teule ya Muheza kwa matibabu zaidi.

Katika hatua nyingine Kamanda Jongo amesema kuelekea msimu wa Sikukuu ya Eid Jeshi la Polisi Tanga linaendelea na operesheni za usalama barabarani ili kuhakikisha Wasafiri wanatumia barabara katika hali ya usalama.View attachment 2194795
Auntie hadi nyie mmeanza matukio ya hivi[emoji2297][emoji2297]
 
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema wapo tayari kusota na kutembea kwa mguu lakini hawakubali kuchukua ruzuku ya Sh110 milioni inayotolewa na Serikali kwa vyama vya siasa vinavyostahili.

Mbowe amesema wakichukua ruzuku hiyo watahalalisha matunda ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2020 ambao waliupinga haukuwa halali.

Mbowe ametoa kauli hiyo leo Jumatano Aprili 20, 2022 wakati akizungumza na wafanyabiashara wa Mtaa wa Raha Square Kariakoo alipofanya ziara ya kuwatembelea ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni ya 'Join the Chain' yenye lengo la kuwahamasisha wananchi kukichangia chama hicho kwa ajili ya uendeshaji.
View attachment 2194799
Nchi ina vimbwanga hii[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom