Makapuku Forum

Makapuku Forum

Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Deus Seif amesema Walimu walionufaika kwa kupandishwa madaraja (vyeo) katika Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu katika kipindi cha mwaka 2021/2022 pekee ni 92.9% ya Walimu wote ambao ni takribani 260,000.

Deus ametoa kauli hiyo akiwa Mwanza leo ambapo amesema "Ajira imetolewa kwa awamu nne, ya kwanza Walimu 13,000, ya pili 7000, ya tatu 6000 na ya nne ni hii ya juzi 12,000 kwa harakaharaka ni sawa na 15% ya Walimu waliopo"

"Kwa upande wa madaraja (vyeo) mwaka jana Walimu 127,000 wamepanishwa vyeo, mwaka huu zajdi ya 60,000, watakaonufaika na daraja la mserereko ni Walimu 52,0000 ambapo kwa haraka jumla ya walionufaika ma madaraja ni sawa na 92.9%"

"Ukiacha miundombinu ya madarasa/samani na vitabu tayari TAMISEMI imeanza zoezi la ujenzi wa nyumba za Walimu, unaachaje kusema asante kwa Mh. Rais kwa hatua hii kubwa kwa Walimu, Asante Mama"
View attachment 2195608
Shubaakengemiti zake.
 
Polisi Lindi wanamtafuta Saidi Haji Ngamila (30) wa Kijiji cha Barikiwa Wilaya ya Liwale kwa tuhuma za kumuua Mke wa Mtu (Mwajuma Ally Lipala miaka 49 ) ambaye alikua Mchepuko wake kwa kumkata na kitu chenye ncha kali na kutengenganisha kichwa na kiwiliwili na kisha kuchimba shimo na kumfukia.

Mume wa marehemu Rashid Ally Mkumba (69) amesema Aprili 14,2022 yeye na Mkewe walikwenda kwenye shamba lao la mahindi na mihogo kwa ajili ya ujenzi wa kibanda cha kulinda wanyama waharibifu lakini wakati anaendelea na ujenzi Marehemu alimuaga kuwa anakwenda kukata nyasi za kuezekea kibanda lakini hakurudi tena.

Baada ya kutorejea kwa Mke wake, Rashid alikwenda kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji ambapo juhudi za kumtafuta zilianza na ilipofika Aprili 16,2022 mwili wake uligundulika kufukiwa pembeni mwa nyumba ya Mtuhumiwa Saidi Haji Ngamila ambapo Kamanda wa Polisi Lindi Mtatiro Kitinkwi amesema uchunguzi wa awali umeonesha wawili hao walikuwa Wapenzi.

Kamanda Kitinkwi pia amesema polisi kwa kushirikiana na ndugu wa Marehemu waliikuta mundu ya kukatia nyasi aliyokuwa anaitumia Marehemu siku aliyotoweka na viatu alivyovaa mara ya mwisho vilikuwa nyumbani kwa Mtuhumiwa.
View attachment 2195611
Daaah!![emoji1787][emoji2297][emoji2297][emoji2297]
 
Back
Top Bottom