Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waziri wa TAMISEMI,Innocent Bashungwa Bungeni leo amesema Serikali inatambua mchango mkubwa wa Wamachinga katika kukuza uchumi, hivyo amewaelekeza Viongozi wote wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri kuhakikisha vitendo vya kuwanyanyasa machinga na kutumia nguvu katika kuwaondoa na kuwapanga ikiwemo kuharibu bidhaa zao kama ilivyotokea kwa Jiji la Mwanza vinakomeshwa.

"Katika kuboresha miundombinu ya kufanyia biashara kwa Wamachinga, Serikali imechukua ya kuwapanga Machinga kwenye maeneo rasmi kwa utulivu pasipo kutumia nguvu katika Halmashauri zote zilizokuwa na machinga wengi kupitia Ofisi za Wakuu wa Mikoa.

"Hatua nyingine iliyochukuliwa ni Serikali kutoa Shilingi bilioni 5.0 kwa ajili ya kuboresha maeneo ya kufanyia biashara machinga katika Halmashauri 11, hatua nyingine inayoendelea ni kuwepo kwa majadiliano na Wizara ya Fedha na Mipango ili kufanya marekebisho ya Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura 290 ili kuruhusu sehemu ya fedha za Mikopo ya 10% kutumika katika kuboresha miundombinu ya Machinga.

"Marekebisho ya Sheria hii yanapendekezwa kufanyika kupitia Sheria ya Fedha ya Mwaka 2022, majadiliano hayo yakikamilika, tunatarajia kiasi cha Shilingi bilioni 38.01 zitapatikana kupitia mlango huo kwa ajili ya ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya Wafanyabiashara Wadogo (Machinga)"
Screenshot_20220421-040841_Instagram.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa, Bungeni Dodoma leo amesema posho za Madiwani sio hisani ya Mkurugenzi wa Halmashauri bali ni haki ya Madiwani kulipwa posho hizo na kusema kwa sasa Serikali inaandaa mwongozo juu ya utaratibu wa ulipaji wa posho za vikao kwa Madiwani ambao utapaswa kutumika kwa Halmashauri zote.

"Waziri mwenye Dhamana na Serikali za Mitaa alishatoa Waraka wenye Kumb. Na. 215/443/01/50 wa tarehe 23/12/2014 juu ya posho za mwezi za Madiwani"

"Aidha posho za vikao za Madiwani zimeelekezwa katika waraka Kumb. Namba CHB/443/01 wa tarehe 26/11/2007 na kusisitizwa katika waraka Kumb. Na PM/P/1/567/59 wa terehe 16/08/2012 ambapo ni shilingi 40,000, hivyo posho za Madiwani sio hisani ya Mkurugenzi wa Halmashauri"
Screenshot_20220421-040938_Instagram.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa ametangaza Bungeni leo kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ametoa idhini ya ajira za Watumishi wa Sekta ya Elimu na Afya 17,412 ambapo nafasi 9,800 ni za Walimu na 7,612 ni za kada za afya ambao wataajiriwa katika mwaka huu wa Fedha 2021/22.

"Naomba kutoa taarifa rasmi kuwa Watanzania wenye sifa wanaelekezwa kuanza kuomba kuanzia leo, aidha, napenda kuwaelekeza kuwa maombi ya ajira hizi ni bure na yanafanyika kupitia mfumo wa kielektroniki ambao maelekezo yake yatakuwa katika tangazo la ajira"

"Asilimia tatu (3%) ya ajira hizo wataajiriwa Watu wenye Ulemavu kulingana na Sheria"
Screenshot_20220421-041125_Instagram.jpg
 
Watu wawili wamefariki kwenye ajali iliyotokea leo April 20,2022 kati ya Kijiji cha Mavuji na Nangurukulu Wilayani Kilwa Mkoa wa Lindi ikihusisha Basi la Kampuni ya Buti la Zungu ambalo limegongana na pikipiki, RPC wa Lindi Mtatiro Kitinkwi amethibitisha.

RPC Mtatiro amesema "Pikipiki ilikuwa ikiendeshwa na Jafari Madega (30) akiwa amembeba abiria aitwaye Athuman Madega (58) ambaye ni Mfanyakazi wa TANESCO Wilayani Kilwa, Dereva huyu wa pikipiki na abiria wake ndio ambao wamefariki kwenye ajali hiyo, wote wamefia palepale kwenye eneo la tukio"

"Miili ya Marehemu imehifadhiwa Kituo cha Afya Kilwa Masoko, uchunguzi wa awali unaonesha Dereva wa pikipiki alihama upande wake na kwenda upande wa Basi hilo, Polisi tunamshikilia Dereva wa Basi kwa uchunguzi zaidi"
Screenshot_20220421-041652_Instagram.jpg
 
Mkuu wa huduma ya kitaifa ya Polisi nchini Kenya Inspekta Jenerali Hilary Mutyambai amesema takribani Maafisa 2,000 wa Polisi wa Kenya wana matatizo ya afya ya akili na kwamba hawana uwezo wa kiakili wa kufanya kazi yao.

Amesema wamebaini jambo hilo la kushangaza baada ya kuwafanyia uchunguzi wa kimatibabu Maafisa wote wa Polisi, Kenya ina Maafisa 100,000 wa polisi wanaofanya kazi chini ya Huduma ya Kitaifa ya Polisi ambapo ripoti hii inakuja huku kukiwa na ongezeko la idadi ya matukio ya Polisi kujiua kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo msongo wa mawazo.

Mutyambai amesema shughuli ya kuwaondoa kazini baadhi ya Polisi hao wenye matatizo ya afya ya akili imeanza kwa kuzingatia umuhimu wa kuwa na Polisi walio sawa kiakili "Zana yetu ya kazi ni bunduki na risasi moja inapopigwa madhara yake ni makubwa"

Siku za hivi karibuni Kumekuwa na wasiwasi unaoongezeka juu ya afya ya akili ya Polisi ambapo Serikali ya Kenya imeanza kulishughulikia hilo kwa kuanzisha Bodi ya Kitaalamu ya Afya inayojumuisha Washauri na Madaktari wa akili walioidhinishwa na Wizara ya Afya kutoa huduma za afya ya akili.
Screenshot_20220421-041747_Instagram.jpg
 
Polisi Tanga wanamshikilia Mkazi mmoja wa Bwembwela Wilayani Muheza kwa tuhuma za kumjeruhi Elias Omari (55) kwa panga mpaka kupelekea kufariki dunia akidai kuwa amemuibia unga na dagaa.

RPC wa Tanga Safia Jongo ameithibitishia @ayotv_ tukio hilo na kusema chanzo ni ugomvi wa kugombania unga na dagaa uliopelekea wawili hao kupigana kwa kutumia mapanga na kusababisha kifo kwa mmoja wao.

Kamanda Jongo amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia April 17,2022 na kwamba Mtuhumiwa (30) alijeruhiwa pia katika ugomvi huo na kwa sasa yupo Hospitali teule ya Muheza kwa matibabu zaidi.

Katika hatua nyingine Kamanda Jongo amesema kuelekea msimu wa Sikukuu ya Eid Jeshi la Polisi Tanga linaendelea na operesheni za usalama barabarani ili kuhakikisha Wasafiri wanatumia barabara katika hali ya usalama.
Screenshot_20220421-041856_Instagram.jpg
 
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema wapo tayari kusota na kutembea kwa mguu lakini hawakubali kuchukua ruzuku ya Sh110 milioni inayotolewa na Serikali kwa vyama vya siasa vinavyostahili.

Mbowe amesema wakichukua ruzuku hiyo watahalalisha matunda ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2020 ambao waliupinga haukuwa halali.

Mbowe ametoa kauli hiyo leo Jumatano Aprili 20, 2022 wakati akizungumza na wafanyabiashara wa Mtaa wa Raha Square Kariakoo alipofanya ziara ya kuwatembelea ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni ya 'Join the Chain' yenye lengo la kuwahamasisha wananchi kukichangia chama hicho kwa ajili ya uendeshaji.
Screenshot_20220421-042204_Instagram.jpg
 
CITY WANAREJEA KILELENI [emoji772]
.
FT: MAN CITY 3-0 BRIGHTON
53’—[emoji460]️ Mahrez
65’—[emoji460]️ Foden
82’—[emoji460]️ Silva
.
Vita ya Ubingwa [emoji471]
1. Man City — 77
2. Liverpool — 76
.

………
Screenshot_20220421-042320_Instagram.jpg
 
LONDON IS RED [emoji837]
.
FT: CHELSEA 2-4 ARSENAL
13’—[emoji460]️ Nketiah
17’—[emoji460]️ Werner
27’—[emoji460]️ Smith-Rowe
32’—[emoji460]️ Azpilicueta
57’—[emoji460]️ Nketiah
90+2’—[emoji460]️ Saka
.
4G [emoji15]
Screenshot_20220421-042437_Instagram.jpg
 
Cristiano Ronaldo tayari amewasili jijini Manchester siku ya leo na alihudhuria mazoezi ya jioni na kufanya session nzima

Ikumbukwe alisafiri kuelekea jijini Madrid kwa ajili ya msiba wa mwanae wa kiume
Screenshot_20220421-043727_Instagram.jpg
 
Maisha wakati mwingine yanaweza kukutimizia ndoto zako ndani ya sekunde moja tu kama ilivyo kwa Binti mmoja huko nchini Ufaransa

Binti alikuja kwenye lift moja na nyota wa PSG, akiwemo Lionel Messi, Neymar Jr, Sergio Ramos na Kylian Mbappe, ikabidi atumie nafasi hiyo kupata selfie
Screenshot_20220421-043913_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom