Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kuna kipindi watu wengi tuliadimika sababu ya ubize ...ila hapa ni familia ya milele tunarud kama hivi

Shunie kama kawaida mwendo wa kutupa updates na magazeti kila dairy

Nigendako ubize anakuja mara moja moja
Binamu wangu ndugu yako Obe huyu yupo kama hayupo [emoji23][emoji23][emoji23]
Wageni wanapita mara moja moja

Tumosa kaadimika haswaaa

BITOS ndo sjui nani alimkimbiza

Mndali yupo anakuja akipata mda

Na wengine wengi wapo wanakuja mara moja moja
Hakuna tabu.. Kiukweli bitoz nyangema hata sijui kahamia mtaa gani, kimya saana.

Wabarikiwe woote ambao wanauendeleza huu mji wa makapuku, wazawa, wageni, wapangaji, wafanyabiashara nakadhalika woote wabarikiwe bila wao huu mtaa ungepotea.
 
Mtaani kwetu uswahilini, ukiingiza demu saa 7 usiku asubuhi kila mtu habari anazo, sasa uibiwe visempele vyako kauka nikuvae umeanika saa 7 mchana watu wanaiba na kila mtu anakwambia "mi sijui" [emoji23]
Unajua majirani zetu ndio wanao tufwatilia kuliko hata wewe unavyo jiweka

Na wizi mwizi wa kwanza ni jirani yako
 
Mwanaume mmoja wa Kentucky nchini Marekani amelipwa USD 450,000 baada ya kampuni yake kumfanyia tafrija ya kushtukiza (suprise) ya siku ya kuzaliwa kwake licha ya onyo alilolitoa kuwa ingeweza kumsababishia msongo wa mawazo na hofu.

Mlalamikaji, Kevin Berling, anadai kuwa tafrija ile ambayo hakuitaka ya siku ya kuzaliwa ya mwaka 2019 ilimsababishia matukio kadhaa ya kuwa na hofu, madai ya kesi ya Berling yanadai kuwa kampuni hiyo ilimbagua kwa sababu ya ulemavu wake, Kampuni hiyo imekanusha kufanya jambo lolote baya.

Kwa mujibu wa kesi iliyowasilishwa katika Kaunti ya Kenton, Kentucky, Berling ambaye ana matatizo ya kuwa na wasiwasi alimwomba Meneja wake asisherehekee siku yake ya kuzaliwa kazini kama ilivyo kawaida kwa Wafanyakazi wengine kwasababu inaweza kumsababishia mashambulizi ya hofu na kurejesha kumbukumbu zisizofurahi za utotoni ambapo licha ya ombi la Berling, kampuni hiyo, ambayo hufanya vipimo vya Covid-19, ilimfanyia sherehe ya kushtukiza Agosti 2019, na kusababisha shambulio la hofu.

Haraka alitoka kwenye sherehe na kumalizia chakula chake cha mchana kwenye gari lake, kesi hiyo inabainisha kuwa Berling alishutumiwa na kukosolewa katika mkutano siku iliyofuata, ambapo alishutumiwa kwa kutowafurahisha Wafanyakazi wenzake.

Mkutano huo wa mvutano ulisababisha shambulio la pili la hofu, baada ya hapo kampuni ikamrudisha nyumbani kwa muda uliosalia wa Agosti 8 na 9 Agosti.View attachment 2193614
Ngija mtu ajichanganye kunisapraizi nikamsapraizishe mahakamani.

Mafuta yaishapanda bei, maisha magumu watu wanataka pesa rahisi.
 
Back
Top Bottom