Makapuku Forum

Makapuku Forum

Wakati Mataifa mbalimbali ikiwemo Marekani yakiendelea kutuma silaha
kuisaidia Ukraine kupambana na Urusi, China imesema kuipa Ukraine silaha kunachochea vita na kutoa wito kwa Mataifa mbalimbali kuweka nguvu kubwa kwenye kumaliza vita na sio kuchochea.

Mjumbe wa kudumu wa China kwenye Umoja wa Mataifa, Zhang Jun amezitaka Urusi na Ukraine kufanya majadiliano ya amani na kumaliza vita huku akizitaka Nchi nyingine kushiriki kuleta amani badala ya kuendelea kuipa Ukraine silaha za kivita.

Kauli ya China inakuja wakati huu ambapo tayari Ukraine imepokea ndege za kivita kutoka Marekani kwa ajili ya kujilinda katika uvamizi unaofanywa na Urusi nchini humo huku Rais wa Ukraine Volodomyr Zelenskiy akiendelea kuitaka NATO itume msaada wa ndege za kivita nchini humo.

Wakati huohuo Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau amesema nchi hiyo itaipa msaada wa silaha nzito za kijeshi Ukraine kufuatia wito wa msaada uliotolewa na Rais Zelenskiy.
Screenshot_20220420-142445_Instagram.jpg
 
Watu sita wamefariki dunia na wengine wanne wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari Toyota Noah ambayo imegongana na lori (Scania) katika eneo la Alkatani Kata ya Sepeko Tarafa ya Kisongo Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha katika barabara ya Arusha-Babati.

RPC wa Arusha ACP Justine Masejo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo amesema ajaili hiyo imetokea usiku wa April 19,2022 na kusema Noah ilikuwa inatokea Arusha mjini kwenda Karatu na lori lilikuwa linatokea makuyuni kwenda Arusha mjini.
"Chanzo cha ajali ni uzembe wa Dereva wa lori ambapo alishindwa kulimudu lori na kuhamia upande mwingine wa barabara na kusababisha kugongana na Noah, tunamshikilia Dereva huyo aliyesababisha ajali"

"Bado tunaendelea kufanya uchunguzi wa majina ya waliofariki katika ajali hii na nawaomba Wananchi wafike Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha (Mount Meru) kutambua miili ya Marehemu" RPC Masejo
Screenshot_20220420-142714_Instagram.jpg
 
Ukraine imepokea ndege za kivita kutoka Marekani kwa ajili ya kujilinda katika uvamizi unaofanywa na Urusi nchini humo.

Msemani wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani John Kirby amesema kwa sasa Ukraine ina ndege zaidi za kivita ikilinganishwa na wiki mbili zilizopita.

Kirby lakini hakutoa maelezo zaidi kuhusiana na zilikotengenezwa ndege hizo au muundo wake, Rais wa Ukraine Volodomyr Zelenskiy alikuwa ameitaka NATO kutuma msaada wa ndege za kivita nchini humo.

Wakati huohuo Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau amesema nchi hiyo itaipa msaada wa silaha nzito za kijeshi Ukraine kufuatia wito wa msaada uliotolewa na Rais Zelenskiy.
Screenshot_20220420-142817_Instagram.jpg
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Innocent Bashungwa @innocentbash amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro, Hassani Njama Hassani kuanzia leo tarehe 20.04.2022 ili kupisha uchunguzi.

Waziri Bashungwa amechukua hatua hiyo baada ya Mkurugenzi huyo kushindwa kutekeleza maagizo aliyoyatoa wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanya Tarehe 10.03.2022 Wilayani humo.

Wakati wa ziara hiyo Waziri Bashungwa alibaini upotevu wa Fedha za miradi na matumizi yasiyo sahihi ya kiasi cha shilingi milioni 231.84 katika ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kumbukumbu ya Moringe Sokoine zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa bwalo la chakula, jiko na bweni na kumuagiza Mkurugenzi huyo kuwachukulia hatua za kiutumishi Wakuu wote wa Idara na watumishi waliohusika na ukiukwaji wa taratibu za manunuzi katika mradi huo.

Hadi kufikia leo hii hakuna Mkuu wa Idara yeyote ama Mtumishi aliyechukuliwa hatua kufuatia maagizo hayo, aidha Waziri Bashungwa ameendelea kuwataka Wakurugenzi wa Halmashuri zote nchini kuendelea kusimamia miradi ya maendeleo kikamilifu na kuchukua hatua za haraka pale wanapobaini ubadhifu wa fedha za umma.
Screenshot_20220420-143104_Instagram.jpg
 
Shirika la Umoja wa Mataifa linalowashughulikia Wakimbizi (UNHCR) linasema Watu milioni tano wameikimbia Ukraine hadi sasa kufuatia uvamizi unaofanywa na Urusi nchini humo.

Akizungumza nchini Hungary ambako karibu Waukraine nusu milioni wamekimbilia, Naibu Kamishina wa Shirika hilo, Kelly Clements amelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuweka kando tofauti tofauti zilizoko kwa sasa katika Baraza hilo na kutafuta njia ya kufikisha mwisho vita hivyo. Afisa mmoja wa Shirika la Kimataifa la Wakimbizi IOM Antonio Vitorino amesema watu wengine zaidi ya Milioni 7 ni Wakimbizi wa ndani nchini Ukraine.
Screenshot_20220420-143203_Instagram.jpg
 
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema limekamilisha matayarisho ya kuiandaa transfoma yenye uwezo wa MVA 30 ambayo imesafirishwa rasmi kuelekea kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Msamvu Mkoani Morogoro.

Transfoma hiyo itasaidia kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme kwa Wakazi wa Mkoa wa Morogoro na baadhi ya maeneo jirani ikiwemo mkoa wa Tanga ambao kwa sasa unapata changamoto ya upungufu wa umeme.
Screenshot_20220420-143332_Instagram.jpg
 
Shirika la Ndege la Rwanda limesema katika tukio la kuacha njia kwa ndege yao leo katika uwanja wa Entebbe nchini Uganda hakuna mtu aliyepata majeraha na abiria wote wametoka wakiwa salama.

Ndege hiyo ambayo ilikuwa na abiria wanaotajwa kuwa 60 imeachia njia leo Aprili 20, 2022 saa 11 alfajiri wakati ikijaribu kutua ikitokea Kigali kupitia Nairobi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Rwanda Air, ndege hiyo ilitoka katika njia yake wakati wa kutua kutokana na hali ya hewa mbaya, lakini Abiria wote na wahudumu ndani ya ndege waliokuwemo wametoka wakiwa salama.
Screenshot_20220420-143445_Instagram.jpg
 
Mambo yanazidi kumwendea kombo rapa maarufu duniani, Kanye West baada ya msanii mwenzake, Kid Cudi kutangaza kuwa hatafanya naye tena kazi baada ya kushirikiana naye katika kibao cha "Rock N Roll".

Wimbo huo uko katika albamu ya rapa mwingine, Pusha-T inayosubiriwa kwa hamu na inayokwenda kwa jina la "It’s Almost Dry". Albamu ya "It’s Almost Dry" imetayarishwa na Kanye West na rafiki yake mwingine, Pharrell Williams na inatoka Ijumaa hii.

Katika akaunti yake ya Twitter, Kid Cudi ameandika ujumbe huo kuwataarifu mashabiki wake kuwa wimbo huo ni wa mwisho kufanya kazi na West, ambaye anaonekana kusumbuka tangu mkewe wa zamani, Kim Kardashian aanze mahusiano na mchekeshaji Pete Davidson
Screenshot_20220420-143550_Instagram.jpg
 
KERRY AWAPA MBINU SIMBA
.
Kocha wa Moroka Swallows, Dylan Kerr ambaye aliwahi kuifundisha Simba, amewapa madini Wekundu wa Msimbazi mbinu za kuwamaliza Orlando Pirates katika mechi yao ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Jumapili hii.
.
Kerry akiwa na Swallows katika mechi TANO zilizopita dhidi ya Orlando ameshinda moja, sare tatu na kapoteza mechi moja.
.
“Nakumbuka mara mwisho kucheza dhidi ya Orlando nilitumia mfumo wa 4-3-3, tulitengeneza vizuizi vitatu kila pembe, haikuwa rahisi kufika eneo letu, tulifunga njia, kila mpira ambao tulikuwa tukiupata tulihakikisha unakuwa na madhara kwao,” alisema na kuongeza.
.
“Haikuwa rahisi kupata pointi dhidi yao lakini kasi ilitubeba. Mkishambulia kwa kasi mnawavuruga,” alisema.
Screenshot_20220420-143734_Instagram.jpg
 
Kocha Mkuu wa timu ya Simba, Pablo Franco amewaondoa wasiwasi mashabiki wake kuhusu mechi ya ugenini dhidi ya Orlando Pirates huku akiwataka kujiamini kwani tayari amewasoma wapinzani wake na ataanza mipango ya kuwabana nyumbani kwao.

“Tuna nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali, tunapaswa kufurahia ushindi huu kwani ilikuwa muhimu kushinda, kuanzia Jumanne (leo) tutaingia mazoezini kuhakikisha tunajipanga vizuri kwaajili ya mechi ya marudiano ugenini,” alisema Pablo na kuongeza;

“Nawapongeza wapinzani wetu kwa mchezo mzuri, walikuwa bora lakini tulikuwa bora zaidi yao nadhani mechi ijayo itakuwa ngumu lakini tunaenda kujipanga kupata matokeo rafiki na kusonga mbele.”
Kikosi cha Simba kinafurahia kurudi kwa nyota wake wawili, beki Joash Onyango na kiungo Sadio Kanoute ambao walikosekana mchezo wa juzi kwani walikuwa wanatumikia kadi za njano.
Screenshot_20220420-144747_Instagram.jpg
 
Mwanariadha wa Kenya, Damaris Muthee Mutua amekutwa akiwa amefariki nyumbani kwa mpenzi wake usiku wa kuamkia leo Jumatano.

Polisi nchini Kenya wanamsaka mpenzi wake Damaris ambaye pia ni mwanariadha wa Ethiopia aliyetambulika kwa jina la Koki Fai.

Mkuu wa polisi kaunti ya Keiyo Tom Maruko alisema mpenzi huyo anashukiwa kumuua Damaris na inaaminika ameshatoroka nchini humo.

Screenshot_20220420-144925_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom