[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr
Ikatokea tu mfano Simba anatolewa kule Afrika Kusini na Orlando Pirates
Ikatokea tu timu zote nne ambazo zimefuzu kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao kutokana na mafanikio ya Simba zote nne zikafanya tu vibaya
Ikatokea kwa mfano zote nne zimetoka raundi ya kwanza, ikatokea Libya wamesogea na Nigeria wakatuzidi alama wakapeleka timu nne sisi tukazidiwa, unaonaje hiyo?
Yani sote tukishakuwa wa hapa hapa, tunapishana humu humu, unahisi kuna uwekezaji wa maana utaendelea kwenye sehemu hakuna faida?
Ziko wapi leo hii Gor Mahia na FC Leopards? Leo hii wapo kwenye ramani ya soka la Afrika? Zipo wapi tambo za Wakenya kwenye michuano ya Afrika? Zipo tena?? Vipi thamani ya ligi yao, ipo tena? Vipi kuhusu mpira wao kwa ujumla?
Mfano tu tukaipiga vita Simba kisha Mungu akaitikia dua zetu, kwahiyo tupo tayari kuwa kama Majirani? Tupo tayari kuona hata Wadhamini wanaoongezeka kisa thamani waondoke? Tunatamani hicho?
Leo hii Real Madrid na Barcelona wamesaini mkataba wa kuungana pamoja kwa kila kinachoitwa maslahi, leo hii PSL (Bodi ya ligi ambao ni mjumuiko wa klabu) pale Afrika Kusini, jambo la Pirates ni jambo la wote
Hakuna cha maana kwenye chuki, mwisho wa siku sote tukibaki hata kicheko kitaisha, hata tambo zitaisha, zitasalia Majuto mengi ambayo ndio Mjukuu
Jitazame tu unayo nafasi yako kwenye mpira wa hii nchi, kama huwezi kwa ajili ya Simba basi fanya kwa ajili ya bendera na nembo ya Visit Tanzania kifuani mwao
Unaweza kuniona Mshamba, unaweza kuniita Mshabiki sana au wa mchongo ukipenda ila hujachelewa sana kuutazama mpira kwa jicho yakinifu
“Dhambi ya ubaguzi haiwezi kuisha ni sawa na kula nyama ya Mtu” Mwalimu Julius Kambarage Nyerere