Ed Sheeran ameshinda kesi ya hakimiliki nchini Uingereza iliyokuwa imefunguliwa kuhusu wimbo wake wa mwaka 2017 wa “Shape of You” ambao ulidaiwa ku-copy sehemu ya wimbo wa "Oh Why" uliofanywa mwaka 2015 na Sami Switch.
"Ingawa tunafurahishwa na uamuzi huu, ninahisi kama madai kama haya ni ya kawaida sana sasa na yamekuwa utamaduni huku yakifanywa kwa mawazo kwamba suluhu itakuwa nafuu kuliko kupelekana mahakamani hata kama madai yenyewe hayana msingi" alisema Sheerhan.
Andrew Sutcliffe ambaye ni Wakili wa Waandishi-wenza wa "Oh Why'' alisema kulikuwa na "ufanano usiopingika kati ya nyimbo hizo mbili na kudai kwamba Sheeran alikuwa na "Oh Why" wakati akiandika "Shape of You" mwaka 2016 wakidai kiitikio cha "Oh I, Oh I, Oh I" kwenye "Shape Of You" kilikuwa "kinafanana sana" na mstari "Oh why, Oh why, why" katika wimbo wao.
Wakati wa kesi hiyo ambayo ilidumu kwa siku 11, Jaji wa Mahakama Kuu Antony Zacaroli alihitimisha kwa kusema kwamba Sheeran "si kwa makusudi au kwa ufahamu" alinakili kifungu cha maneno kutoka "Oh Why" alipokuwa akiandika wimbo wake.
Sheeran na wenzake ambao ni McDaid na Mac walisema katika taarifa yao kwamba gharama ya kesi hii ilikuwa zaidi ya pesa kwa sababu ya stress za kujua kwamba wanatakiwa Mahakamani na hiyo inaumiza ubunifu na kuathiri hisia.