[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr
Wakati wachezaji wa Liverpool wanashangilia ubingwa wa Carabao uwanjani pale Wembley, kila Mchezaji alikuwa na namna ya kuonesha furaha yake baada ya kuifunga Chelsea kwa penati
Mchezaji mmoja alishika chupa ya pombe na akataka aifungue kisha aimwage, ila pembeni yake alikuwepo Sadio Mane nyota ambaye ni muumini wa dini ya Kiislam ambaye pombe kwake ni haramu
Mane kwa haraka sana alimwomba mwenzie asifungue chupa ile ya pombe mbele yake, uungwana mkubwa pia kwa Mchezaji mwenzake ambaye nae alimuelewa Mane na akaacha kuifungua
Wakati wapo vyumbani wakiendelea na sherehe za ubingwa, picha nyingi sana za ndani Mane hakuonekana ila kulikuwa na footage moja tu ambayo Mane alikuwa ameshika mswala (mkeka wa kuswalia)
Kwenye video hiyo Mane alionekana anatoka anaelekea kwenye chumba kingine kwa ajili ya kukamilisha ibada ya swala ya Magharib baada tu ya mechi kuisha, ndio maana hakuonekana kabisa mwanzoni mwa sherehe
Sadio Mane huyu huyu baada tu ya kubeba ubingwa wa AFCON 2021, Liverpool ilikuwa tayari kumuandalia sherehe wakati anarejea ila yeye alituma ombi maalum kuwa wasimfanyie sherehe yoyote kwa heshima ya MO Salah wa Misri
Ikaja tena kuwa Mane na Senegal yake wamefuzu fainali za kombe la dunia, ni yeye tena akatuma ujumbe kuwa wasimfanyie sherehe yoyote kwakuwa ana heshima yake kwa Mohamed Salah na wachezaji wengine wa Afrika kikosini
Huyu ndie Sadio Mane ambaye Jurgen Klopp anasema sababu ya kumtumia Mane moja kwa moja kikosini akitoka michuano ya kimataifa ni kuwa, Mane hanywi kabisa pombe hivyo hana shida kwenye fitness
Niwatakie mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa hisani ya Ndugu yetu katika imaan, Ustadh Sadio Mane[emoji120]
We all dream to have the attitude like Sadio Mane