DEAN REFA WA KADI [emoji817]
.
🟥 — 114
🟨 — 2026
.
Refa Mike Dean ametoa kadi nyekundu nyingi (114), za njano (2026), na ametoa penalti nyingi (184) zaidi ya refa yeyote katika historia ya Ligi Kuu ya England.
EDO KUHUSU HATMA YA INJINIA SIMBA !!
.
Thadeo Lwanga Injinia ana staili yake ya kipekee katika timu na ni mchezaji ambaye Simba wanapaswa kumbakisha lakini huku wakitumia tahadhari fulani kuanzia sasa hadi mwishoni mwa msimu.
.
Simba inabidi wachunguze kama injinia ameendelea kuwa mchezaji yuleyule au vinginevyo. Wakati mwingine wachezaji wakikaa nje kwa muda mrefu kasi yao huwa inaathirika na hawarudi kuwa bora kama walivyo.
.
Kama injinia akirudi katika ubora wake basi wampe mkataba mpya. Anajua kunusa hatari na kukata umeme. Ni kitu muhimu ambacho pacha wake wa uwanjani Jonas Mkude hana. Lakini kama asiporudi katika ubora wake nafasi yake anaweza kutafutwa mtu mwingine.
KABWILI KUHUSU SKENDO SASA !!
.
Uongozi wa Yanga Disemba 19, 2021, ulimsimamisha Kabwili na kuondolewa kwenye kikosi cha timu hiyo kutokana na masuala ambayo alihusishwa nayo ambayo ni kinyume na tamaduni za Kiafrika.
.
“Nimejisikia vibaya, lakini kwa bahati nzuri wapo ambao wameanza kurejesha imani kwangu. (Hata hivyo) siwezi kurudishwa nyuma na mapito,” anasema Kabwili.
.
“Mitihani tumeumbiwa wanadamu hakuna jambo gumu ambalo nimekumbana nalo kwenye maisha yangu ya mpira kama hilo. Kila mtu anasema lake, mimi ndiye ninayeujua ukweli. Nashukuru Mungu kwa sasa natazama mbele.”
Timu ya taifa ya Morocco ndio timu pekee ya bara la Afrika iliyofuzu kucheza kombe la dunia ikiwa na kocha ambaye sio mzawa.
Vahid Halilhodžić ni raia wa Bosnia na ndiye kocha mkuu wa timu hiyo.
Timu nyingine zilizofuzu ni;
Senegal-Aliou Cisse
Cameroon-Rigobert Song
Tunisia-Jalel Kadri
Ghana-Otto Addo
Kuna story iliwahi kutembea sana kwamba, ukipigana na bondia Francis Cheka kuna muda unakuwa humuoni jambo ambalo lilihusishwa na imani za kishirikina! Leo bondia Twaha Kiduku amesema, kuna wakati bondia unapigwa ngumi kali na kuhisi huoni
“Hata mimi zamani nilikuwa nasikia kwamba ukipigana na Francis Cheka muda mwingine humuoni, hakuna lolote siku moja nilikuwa na pambano Zambia, nilipigwa ngumi moja nikawa nahisi kama nimefumba macho.”
“Wakati mwingine inatokea bondia anapigwa ngumi anayumba kama mlevi lakini kumbe hajaonja hata pombe kabla ya kupanda ulingoni.”
FIFA WORLD CUP| Shabiki maarufu wa timu ya taifa ya Mexico, Hector Chavez Ramirez amembebea Rais wa FIFA Gianni Infantino zawadi kutoka Mexico kwenye droo ya kombe la dunia
FIFA WORLD CUP| Gregg Berhalter alienda kwenye kombe la dunia miaka 20 iliyopita kama mchezaji wa timu ya taifa ya Marekani na sasa anaenda akiwa kama Kocha wa timu hiyo ya taifa
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.