Imeandikwa na @swalehmawele

Hata katika maisha ya kawaida wapo watu ambao wanafanya mambo makubwa au kutengeneza ramani ya mafanikio lakini mwisho wa siku hawaonekani kama mashujaa, ni vile tumeamua kutowatazama kwa jicho la tatu.

Pichani ni Tyron Damons kocha wa makipa wa Simba, raia wa Afrika Kusini aliezaliwa miaka 44 iliyopita na uzoefu wake wa kufanya kazi katika klabu za TS Galaxy, Bidvest, Mbabane, Chippa United unamrahisishia kuchora ramani nzuri ya Simba katika eneo la magolikipa.

Bila ya kumkosea heshima Milton alietimkia Yanga, bila shaka aliifanya kazi yake ipasavyo na Damons anaendeleza yale mazuri yaliyoachwa na mtangulizi wake, fundi mzuri anahitaji malighafi sahihi ili kusimamisha jengo imara.

Tunaposifu ubora wa Aishi Manula tukumbuke kuwa nyuma yake kuna hiki chuma ambacho kinampiga msasa na hatimae tunamuimba kama shujaa, Manula wa sasa hana errors nyingi ambazo tulikuwa tukiziona misimu kadhaa ya nyuma, hiyo maana yake amekuwa coached vizuri.

Utasikia kauli huko kwenye vibanda umiza, ah! ile save hata mimi nafanya maana mpira umemgonga tu, guys huko kumgonga mpira maana yake alikuwa sehemu sahihi katika wakati sahihi na lazima umpe credit kwa hilo.

Mtazame Manula pale golini, achana na saves zake kisha tazama movement ambazo anazifanya anapojiandaa kuzuia shambulizi, hizo ndizo zinazomrahishia kufanya saves na haya mambo yanaanzia mazoezini, mazoezini kuna nani? yupo Tyron Damons.