
Profesa mmoja kwenye chuo cha mpira pale Johan Cruyff jijini Barcelona aliwauliza Wanafunzi wa regular classes, aliuliza “What are the timer indicators for being a Champion”
Alitaka tu kujua viashiria vya timu kuwa bingwa, ilikuwa ni Homework kwa wanafunzi wake ambao wengi walikuwa ni Wachezaji wa zamani ambao sasa wanataka kuwa Maafisa wa mpira
Mwanazuoni wa kwanza alisimama na kujibu, UNPREDICTABILITY SIR, yes ni kama ambavo Yanga haitabiriki, hujui wataingia kwa mfumo gani na kwa wachezaji gani kwenye mechi husika
Uliwahi kutabiri tu kuwa Farid Mussa atacheza beki ya kushoto?? Uliwahi kuhisi tu kuwa Kibwana Shomari angecheza kulia na kushoto?? Uliwahi kuhisi Dickson Job atacheza kati na pembeni? The answer is NO
Viashiria moja wapo vya kuwa bingwa ni kuwa huwapi watu nafasi ya kutabirika, hujulikani utakujaje kwenye mazingira gani
Mwanazuoni wa pili alijibu, UNCERTAINTY SIR! Akimaanisha kutopewa uhakika ama kutoaminiwa, yani unaenda kutwaa ubingwa mpaka dakika ya mwisho watu bado hawaamini
Iliwahi kutokea kwa Lille pale France, Leicester pale England, hata ule msimu Liverpool anabeba ubingwa, watu walikuwa na nadharia nyingi sana kuwa Liver habebi ila hatimae alibeba
Ndicho unachoona kwa Yanga hivi sasa, ilianza mara pumzi, mara wataumia wachezaji, mara raundi ya pili ila mpaka sasa gari linawaka tu, hakuna kupumzika hajapoteza
Mwanazuoni wa mwisho alimaliza, EMMANUEL SIR! Darasa sote likashangaa, Emmanuel!? Kivipi?? Tafsiri ya Emmanuel ni Mungu pamoja nasi, YES wakati mwingine ni bahati njema huleta ubingwa
Mnakumbuka Liverpool na maamuzi ya VAR? Manchester City na VAR? Au bao la jioni la Aguero? Ama Real Madrid na kamba za Ronaldo? Basi ndivyo kama Yanga, inafika wakati kila kitu kinakuwa upande wako na unakuwa bingwa mteule! EMMANUEL
Ikifikia hapo basi sio Wanadamu tena ni Mungu tu maana Yanga kashinda sehemu nyingi ambazo hatukutarajia
Walimaliza Wanafunzi na Profesa akawapigia makofi, akasema “Today lets end here, we will continue tackling more problems tomorrow concerning this case” WABHEJA SANA
