

Farhan Jr
Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Real Madrid chenye Wafanyakazi takribani 50 ambao kila Mtu ana majukumu yake, kazi yao kubwa ilikuwa kuleta maudhui bora kwa Mashabiki wa Real Madrid
Hii ilikuwa Mei 27, 2018! Ni mandhari ya joto kidogo na jua limeanza kuzama Jijini Kiev, siku moja kabla ya fainali ya UEFA kati ya Real Madrid na Liverpool
Wakati wanafanya mazoezi ya kupiga mashuti, nyuma ya goli walikuwepo Wanahabari wakitazama mazoezi hayo ya mwisho, kila Mtu camera yake ikiwa on standby
Wakati pia macho na masikio ya Wanahabari ni kwa Legends wa Madrid kama Christian Karembeu, Claude Makelele, Alberoa, Roberto Carlos na The Prince of Madrid Raul Gonzalez “El Capitano”
Mpiga picha mmoja wa klabu anaitwa Raul Sanz, aliiweka vyema camera yake waliopewa kutoka kwa Kampuni ya Canon tawi la Concha Espina, Madrid! Tayari kwa ajili ya kupiga picha bora ya maisha yake
Cristiano Ronaldo akiwa amevalia vyema viatu vyake vya Mercurial Vapor Superfly CR7 Chapter 7 brand ya NIKE, alipokea pande zuri kutoka kwa Kocha Zinadine Zidane na golini alikuwepo Kaylor Navas Gamboa
Ronaldo alitumia mguu wake wa kushoto kupiga mpira uliopewa jina la ADIDAS FINALE 18’ ambao ndio ulitumika kwa ajili ya fainali, hakuna aliejua huu ndio mpira wake wa mwisho mazoezini na hatokuwepo hapo tena
Sanz aliwajaza vyema kwenye frame wachezaji wote wa Madrid, akamvuta vyema na Marcelo ambaye alisimama nyuma kabisa wakati Swahiba wake anapiga, akijua siri fulani kubwa kati yao
Ilikuwa picha ya mwisho Ronaldo akiwa mazoezini jioni ile, ilikuwa kama chakula cha mwisho cha Massih Issa bin Mariam na Wanafunzi wake! Hakuna aliefahamu zaidi ya hisia kali za mpiga picha Sanz
Inasalia kuwa picha bora zaidi ya vizazi na vizazi kwa Madridistas! The last supper
Picha ni siri kubwa sana, picha ni kumbukumbu kubwa sana, picha ni maagano kati ya mpigaji na camera yake! Mpe tano Mwanao mpiga picha