Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,926
EwaaaahNoma sana
Leo ni furaha day haswa .





Leo habari nyingine tofauti na simba na chama kwakweli sipost hata mtu anipe hela
EwaaaahNoma sana
Leo ni furaha day haswa .





Leo niKwetu rahaaaaaamwaka huu mashabiki wa simba tunanenepa tu





Mpira mtamu jamaniEwaaaah
Leo habari nyingine tofauti na simba na chama kwakweli sipost hata mtu anipe hela

Sanaaaaa jamaniiiiiiiiMpira mtamu jamani
Simba inatupa raha tu

Farhan Jr
CLATOUS CHAMA, EXTRA DETAILS
Watoto tayari wameandikishwa kwenye shule Moja ya kimataifa Jijini Dar Es Salaam, kwakuwa Chama anataka kukaa nao mwenyewe watoto wake
Mwishoni mwa mwezi December alikamilisha utaratibu wa form na vitu vingine vingi vya msingi, hivyo watoto watakuwa hapa Dar Es Salaam kwa masomo
Makazi mazuri pia Jijini Dar Es Salaam kwakuwa pale alipokuwa anakaa awali maeneo ya Mikocheni hivi sasa amepanga Mbunge mmoja Mkubwa
Rafiki yake wa karibu alikuwepo nchini mwezi mzima kufuatilia Makazi mazuri ya kuendana nao na hatimae wameshapata panapofaa
Moja ya sababu kubwa zaidi ukiachana na yeye kutoendana na maisha Berkane ilikuwa pia watoto wake kukaa nao mbali hakuwa tayari
Berkane walitaka kwenda kumpa Makazi Jijini Casablanca ambapo ilikuwa mwendo wa Masaa sita kutoka Berkane mpaka Casablanca hivyo bado aliona Kuna umbali Mkubwa
Berkane walifanya Kila kitu kumbakisha Triple C ila haikuwezekana na mara zote aliomba kuondoka na Simba ndio ilikuwa jibu lake
Kwa wanaoamini Chama ameisha basi mkumbuke kuwa mechi ya mwisho alikuwa Man of the match na kiwango bora sana ikiwa ni muda mchache baada ya kutoka kwenye majeraha

Farhan Jr
Kwanza kabisa ni kweli Simon Msuva yupo nchini Tanzania na hajarejea nchini Morocco ambapo timu imeshaanza mazoezi tangu January 5, huko Agadir, Morocco
Waandishi kadhaa kutoka nchini Morocco na vyanzo vyangu kutoka Casablanca vinadai kuwa Kuna shida ya kimaslahi kati ya Msuva na Wydad
Timu nyingi za Kiarabu Kuna utata kuhusu signing fee, Inasemekana Msuva licha ya kulipwa mshahara na marupurupu ila changamoto ni kuwa hawajamaliza signing fee yake
Kutokana na mvutano huo Msuva amegomea kurejea nchini Morocco mpaka pale jambo lao litakapokuwa sawa bin sawia Kabisa
Swali la kwanza kwa chanzo changu, je Msuva anaweza kuachana na Wydad na akarejea Tanzania? Jibu ni kuwa Hilo linawezekana ila kwa njia tatu kubwa
Ya kwanza ni Msuva kusaini timu yoyote Tanzania huku sakata lake likiendelea, hii ni kama Chama alivyosaini Simba akitokea Dynamos au Kichuya na ile klabu ya Misri, unaicheza karata ya hatari
Ya pili ni Msuva kukaa chini sasa na Wydad kisha kuvunja rasmi mkataba kwa makubaliano (mutual agreement) kama Chama na Berkane kisha akarejea nchini kucheza
Ya tatu, ni Msuva kwenda FIFA kudai haki yake, ijapo hii njia ni ngumu na huchukua muda, kama ilivyomtokea Shabaan Chilunda ikamlazimu akae nusu msimu bila kucheza na hawaoni Msuva akipita njia jii
Nikauliza Msuva ikitokea anasaini anaenda Simba au Yanga? Jibu ni kuwa wao wanatazama maslahi zaidi, klabu yoyote yenye maslahi mazuri itapewa nafasi, ila mpaka sasa focus ya Msuva ni kupata pesa yake na kurejea kucheza Wydad au sivyo arejee nchini
Msuva sio kama anashinikiza kuondoka Morocco bali anashinikiza malipo yake anayodai