Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220115-104814_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20220115-104831_Opera%20Mini.jpg
 
WANANCHI mmemsiki hii? Afisa Habari wa Simba amesema hivi::
.
“Mnadhani Chama amesahau Boli?? December 29 2021 alicheza mechi yake ya mwisho kati ya Barkane dhidi Youssofia Berrechid na akawa nyota wa mchezo
.
“Sisi tumerudisha mtu kutoka RS Barkane nyie mlimrudisha mtu kutoka Singida United”
Screenshot_20220115-114314_Instagram.jpg
 
PABLO KUHUSU USAJILI WA CHAMA

: “Nilipomuona Chama katika video mbalimbali nilikubali uwezo wake na ndio maana sikutaka kuweka kikwazo katika urejeo wake.
.
“Ni mchezaji mzuri sana, naamini ataisaidia timu kwa kushirikiana na wenzake, uwezo anao mkubwa tu na nina imani naye,”
.
“Angekuwa mchezaji wa kawaida asingezungumzwa kiasi kile ilinifanya hata mimi kumfuatilia sana ili kuona uwezo wake." amesema Pablo Franco.

........……
Screenshot_20220115-114900_Instagram.jpg
 
SAKHO: NAMPA JEZI YAKE CHAMA
.
Simba jana walimtambulisha nyota wao wa kimataifa, Clatous Chama ambaye amerejesha kwenye klabu yake ya zamani huku Pape Sakho anayetumia jezi namba 17 iliyokuwa ikivaliwa na Mzambia huyo akisema yupo tayari kuiacha kiroho safi.

: “Sina tatizo na hii jezi kumwachia kwani sikuja Simba na hii jezi, nimemsikia Chama na ninaamini ni mchezaji mzuri ingawa sijawahi kumuona,” amesema Pape Sakho via [Mwanaspoti]
Screenshot_20220115-115103_Instagram.jpg
 
YANGA YAMALIZANA NA USHINDI
.
Yanga ipo katika hatua za mwisho kumshusha straika Chico Ushindi DRC anayekuja kufunga usajili wa timu hiyo akitokea TP Mazembe huku Mukoko Tonombe akipelekwa kwa mkopo TP Mazembe.
.
Yanga inamchukua Ushindi ambaye alikuwa katika hesabu zao kwa muda anatua Yanga kwa mkopo akitokea Mazembe kuja kuziba nafasi ya Yacouba Sogne ambaye bado ni majeruhi.
Screenshot_20220115-115833_Instagram.jpg
 
MUKOKO APELEKWA MAZEMBE KWA MKOPO
.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga ni kwamba kiungo Mukoko Tonombe ataondoka leo na wiki ijayo atarudi Tanzania kuchukua familia yake tayari kuanza maisha mapya lakini amewaambia rafiki zake ndani ya Yanga kwamba hatasaini mkataba Mazembe zaidi ya miezi sita na punde atarejea kukiwasha Tanzania katika klabu itakayompa mataji na kucheza level ya kimataifa ili kuendelea kulinda nafasi yake katika timu ya taifa.
Screenshot_20220115-120221_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Hata pale ambapo Hassan Dilunga alionekana ameisha kwenye makutano ya Twiga na Jangwani, alipotua Manungu stori ikawa tofauti sana na mpaka sasa yupo Simba

Pichani ni Said Khamis Juma Ndemla, kwenye kiwango bora sana katikati mwa dimba la Mtibwa, anapiga Kila aina ya pass na kufunga pia, kikubwa zaidi ni ile confidence yake

Ukizungumzia Viungo wenye Vipaji halisi kabisa ndani ya hii ardhi, huwezi kosa kumtaja! Unless umtazame kwa jicho la kishabiki au la Kiudalali uamue tu kumkataa, ila he is gifted

Yupo Manungu kwa mkopo ila anaonesha nidhamu kubwa sana, sitoshangaa akienda timu yoyote nchini ikitokea mkataba wake umekwisha kwa kiwango chake pale Manungu

Amekuwa Kioo kwa Vijana wadogo wanaotoka Academy, amekuwa Kioo kwa wakina Joseph Mkele, Nassor Kiziwa na wote wanamtazama kama sehemu ya kujifunza kitu
Screenshot_20220115-120429_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

HANCE MASOUD NA UTATA WA USAJILI

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye vyanzo vyangu ni kuwa Hance Masoud ambaye ni beki wa zamani wa Coastal Union yupo kwenye utata mkubwa wa usajili

Hance alisaini mkataba wa awali na klabu ya Dodoma Jiji wakati akielekea mwisho wa mkataba wake na Coastal Union, huku akipokea sehemu ya fedha za usajili huo

Lakini baadae kulitokea na sintofahamu juu ya Hance kuripoti Dodoma, Kutokana na pia na sababu mbalimbali, ikasemekana atabaki Coast na watampa mkataba mpya

Kutokana na kuwa Dodoma hawakuhitaji kuharibu mahusiano yao na Coast walikubali na wakaomba kiasi chao cha fedha kwa Mchezaji Ili wamuache huru na waendelee na taratibu zingine

Lakini wakati Dodoma wameomba fedha yao, Hance pia alishindwana na Coast kwa issue ya maslahi hivyo isingewezekana kwa Hance kusaini tena Coast

Katikati ya issue hii, wakati Dodoma wanasubiri mzigo wao, wakapokea simu kutoka kwa Viongozi wa Coast kuwa wanaweza kuendelea na utaratibu wao wa kumsaini Kijana, Hivyo Dodoma kwakuwa tayari wana precontract wakatuma details zote TFF

Na mfumo wa TMS umempitisha Hance kuwa ni Mchezaji Halali wa DODOMA JIJI huku taratibu za leseni zikiendelea hivi sasa

Wakati haya yote yakiendelea, KMC na Hance Masoud wamefikia makubaliano ya kusaini mkataba, ila kwenye system anasoma kuwa ni Mchezaji wa Dodoma, hawawezi kufanya kitu bila kumalizana na DODOMA JIJI

Wakati huo Mchezaji anadai yeye ni Free Agent, Dodoma wanasema kama yupo free basi waendelee na taratibu zingine! Dirisha pia linaelekea mwisho usiku wa leo
Screenshot_20220115-135757_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

SIMON MSUVA UPDATES

Taarifa kutoka kwa vyanzo vyangu ni kuwa tayari Msuva alipeleka madai yake FIFA tangu December, 2021 kuhusu malipo ya signing dhidi ya Wydad Casablanca

FIFA wamepokea madai hayo ila huchukua muda kuanzia miezi mitatu mpaka sita Ili kutuma taarifa kwa Klabu husika (Wydad) waanze kutoa utetezi wao

Baada ya huo utetezi ndipo FIFA watakaa chini kupitia wanasheria wake kutazama upande wa Msuva na wa klabu kuhusu hayo madai yake kisha kutoa maamuzi

Msuva yupo Bado nchini kwasasa na FIFA huwa inapenda Wachezaji waendelee kucheza hata kama Wana kesi ili kulinda viwango, Msuva ni mnufaika anaweza kusaini popote akitaka

Ikitokea amesaini au ameshasaini basi FIFA watatuma ITC Ili kumruhusu Mchezaji aendelee kucheza mpira popote anapotaka, mpaka kesi yake itapopata majawabu
Screenshot_20220116-104205_Instagram.jpg
 
Shaffih Dauda

Mtu wa diin sana, Mtu wa Watu sana na mnyenyekevu sana

Mane ni moja kati ya Watu ambao hufika mapema msikitini Jijini Liverpool kwa ajili ya kufagia na kusafisha vyoo Kwa mujibu wa Imaam

Hapo pichani akiwa Bambali kijijini kwao Senegal akila maembe na Marafiki zake

Katoboa maisha, ila hajifungii Masaki wala Mikocheni za Senegal, bali Kijijini kwake ambapo mitaa ilimlea
Screenshot_20220116-122046_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom