Makapuku Forum

Makapuku Forum

Watu watatu waliokuwa wakisafiri kutoka Kata ya Nzera kuelekea Geita Mjini wakitumia gari la abiria (hiace) wamefariki dunia papohapo na wengine 8 kujeruhiwa baada ya gari lao kugongana na Lori katika eneo la Pori la Mgodi wa GGM Wilayani Geita Mkoani Geita.

Akithibitisha uwepo wa miili hiyo iliyopokelewa katika chumba cha dharura Katika Hospitali ya Mkoa wa Geita Kaimu Mganga Mfawidhi katika Hospitali hiyo, Paschal Thumba amesema walipokea miili hiyo ya Watu 3 huku wengine wakipewa rufaa ya kupelekwa Bugando jijini Mwanza.

Jitihada za kumtafuta kamanda wa Jeshi la polisi Mkoa wa Geita zinaendelea ili kubaini chanzo cha ajali hiyo.
Screenshot_20211224-195105_Instagram.jpg
 
Serikali imesema itaendelea kuchukua hatua kali za kisheria kwa Mabasi yote ambayo yanapuuza agizo la Serikali na kuendelea kupandisha nauli msimu huu wa sikukuu ambapo kuanzia leo atakayepandisha nauli atatozwa faini ya Tsh. Laki tano.

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mwita Waitara amesema hayo leo alipotembelea Stendi Kuu ya Mbezi Dar es salaam na kusema hakuna yeyote anaeruhusiwa kupandisha nauli tofauti na ile iliyopangwa na LATRA.

Waitara alitembelea pia katika Stendi hiyo juzi na kutoa maagizo ya nauli kutopandishwa lakini amesema bado Kumekuwa na kupuuzia kwa agizo lake.
Screenshot_20211224-195200_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom