

Farhan Jr
Kila nchi duniani Ina kitu kinaitwa Utamaduni, itakuja mifumo, itakuja mbinu na Kila Mabadiliko ya sayansi ya mpira ila utamaduni ni ule ule
Mfano Real Madrid miaka mingi waliamini Nahodha wao lazima awe Mhispania, ni mara chache Nahodha kutoka taifa lingine mfano sasa
Barcelona wanaamini Midfield yao inahitajika damu kutoka La Masia, piga uwa, lazima Mido moja wapo awe kapita kwenye shule yao ya soka
Kama ilivyo kwa Manchester United na damu za England, wanaamini ni sehemu muhimu kwa Mtoto wa England kucheza, ndio maana Beckham kutoka London alisafiri mpaka North East kucheza Manchester
Kama ilivyo kwa Waarabu na utamaduni wao mfano Al Ahly wanaamini sana kwenye damu zao, wanaamini sana baadhi ya maeneo uwanjani ni yao, kutafsiri mpira wao
Hata pale atakapokuja Mtu kutoka nje ya utamaduni wao sio rahisi kudumu kwa muda mrefu au kupewa uzito mkubwa! Ila hili limekuwa tofauti kwa Mwamba kutoka Mali, Aliou Dieng
Msumari huu unazidi kulitawala dimba na kutakatisha mioyo ya wahafidhina! Kutoka eneo la Kiungo na moyo wa Ahly ndipo alipo Fundi wa Mali aliegomewa kwenda kucheza soka Ulaya
Waarabu lazma wakubali Kuna mechi ilikuwa inapigwa kati ya Fabrice Ngoma na Aliou Dieng, ilikuwa ni Derby ya Wabantu ndani ya Ardhi ya Waarabu
Kuna muda Kuna Utamaduni na Kuna muda Kuna uhalisia