Makapuku Forum

Farhan Jr

CLATOUS CHAMA UPDATE|

Taarifa za kuwa Simba wamemalizana na Wakala wa Chama Jijini Lusaka Zambia sio za kweli na wala hawakukutana

Chama Bado ni Mchezaji wa Berkane kwasasa, hivyo Mawasiliano ya timu yoyote inayomtaka Chama ni lazima yapitie kwenye klabu yake

Ni klabu moja pekee mpaka sasa iliyojaribu kuhitaji huduma ya Chama kupitia kwa Wakala na klabu yake moja kwa moja ila Mchezaji huyo hayupo tayari kujiunga nao

Chama anaendelea kuheshimu mkataba wake na suala lake la kutaka kuvunja mkataba kwa makubaliano ya pande mbili ameendelea kulifanya kwa ufasaha mpaka sasa

Chama Bado ana Mawasiliano na Simba ya karibu na tayari aliwaelezea Nia yake ya kurejea nchini na wao wamebariki hilo kama nilivyosema mwanzo

Ila dau la Chama sokoni ni kubwa hivyo Kuna kete mbili tu za kusukuma, kete ya kwanza ni mutual agreements kisha Chama awe huru ajiunge na Simba ama kete ya pili wamchukue kwa mkopo

Mpaka sasa kete ya kuvunja mkataba kwa makubaliano ya pande mbili yapo vizuri sana ijapo ugumu upo kidogo kwa upande wa Berkane haswa Viongozi ambao wanamtazama Chama kwa picha kubwa sana

Simba wanajitahidi sana kukaa mbali na hilo Ili lisiwatibue Waarabu kuhisi Wana mkono nalo, Chama pia anajitahidi kulifanya private

Akili na moyo wake ni Simba pekee, only Simba is the destination kwa taarifa za Watu wake wa karibu sana!

It is going to happen and it will surely happen
 
Shaffih Dauda

TUPO KWENYE DUNIA YA CHIEF MANGUNGO WA MSOVERO? #FREEBODIYALIGI

Binafsi nimesikia sekeseke la Simba dhidi ya nembo ya Mdhamini GSM kuhusu kukaa begani, kupitia sauti ya CEO wa Simba Barbara (voicenote ya WhatsApp)

Kupitia maelezo yake kwa haraka kwa wenye akili timamu lazima ung'amue kuwa Kuna shida ya mgawanyo wa kimadaraka (Separation of power) kati ya vyombo vya mpira wa miguu, Kuna mmoja anaimba nje ya key

Nimegundua TFF na TPLB (Bodi ya Ligi) Kuna mmoja hayupo huru! TFF ni Baba wa mpira, ila Bodi ya Ligi ni Muwakilishi wa klabu za Ligi Kuu na Championship mpaka First League, ambaye ndie mdau Mkuu

Inakuwa vipi mikataba inasainiwa wakati Klabu ambao ndio Wadau au watekelezaji wakuu hawajui?? Mmewahi kukaa nao chini na kujadiliana kwa maslahi ya mpira wetu hata kama Ligi yetu haina pesa? Kwanini wakose uhuru wao

GSM ana mkataba na TFF, na TFF walisema mkataba unawahusu wao, imekuwaje leo mkataba unawahusu Klabu? Ipi nafasi ya bodi ya Ligi? Ipo huru kwa misingi ipi kwenye hili??

Leo hii kutokaa chini round table na kujadili pamoja mnasababisha migongano ya kimaslahi, mfano si tunatambua GSM ni kit Supplier wa Yanga? Na tunafahamu VUNJABEI ni kit Supplier wa Simba?

Hivi katika Hali ya kawaida NIKE na ADIDAS wanakaaje jezi moja? Kama mnapitisha kuwa GSM sio Kit Supplier wa Yanga basi tuambieni yeye ni nani ndani ya Yanga?? Hivi kwanini tuonekane tuna haraka sana bila kureason?

Sikieni niwaambie! Baada ya Newcastle kununuliwa na Waarabu wa Saudi Arabia, mnakumbuka klabu za EPL chini ya Bodi yao ya Ligi (English Football League) karibia 17 zilipiga kura ya kupinga Utendaji wa moja kwa moja kabla uchunguzi sahihi wa mikataba kufanyika??

Huku kwetu kwanini Klabu zionekane kuwa Passive na sio Active?? Kwanini mnaleta mikataba ya Chief Mangungo dunia ya leo??

FREE BODI YA LIGI #FreeBodiYaLigi

When DIGALA speaks you have to listen
 
Kwahiyo TFF wanahusika na timu za taifa tu?

Fantastic!

Na hiyo Bodi ya ligi inafanya kazi chini ya mamlaka gani?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…