Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20211122-202410_Instagram%20Lite.jpg
 
Mahakama ya usuluhishi wa Kimichezo Duniani (CAS) leo imetoa majibu ya kesi ya kimkataba iliyokuwa ina mkabili Mchezaji wa Simba SC raia wa Ghana Bernard Morrison dhidi ya Club yake ya zamani ya Yanga SC.

Kesi hiyo ilikuwa inahusiana na madai ya Yanga kwa CAS kuwa Morrison anapaswa kulipa fidia ya USD 200,000 (Tsh milioni 460.2) kwa madai ya kuvunja mkataba na Yanga bila kufuata utaratibu na kujiunga na Simba SC, CAS wameweka wazi Morrison alijunga Simba SC kama Mchezaji huru na mkataba wake na Yanga ulikuwa umeisha.
Screenshot_20211122-203438_Instagram.jpg
 
Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) imesema kuna ongezeko la maji kwa sasa ukilinganisha na awali na matokeo ya mapambano yanayoendelea yameanza kuonekana mitaani huku zoezi la kutoa upepo likiendelea litakalopelekea upatikanaji wa maji kwa maeneo ya Kinondoni, Mikocheni, Msasani, Oysterbay, Mwananyamala, Makumbusho na Kijitonyama, DAWASA imeendelea kuwakumbusha Wananchi kuhifadhi maji.
Screenshot_20211122-203637_Instagram.jpg
Screenshot_20211122-203700_Instagram.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla leo amezindua kampeni ya usafi Dar es salaam ambapo Msanii Harmonize, Alikiba na Steve Nyerere ni miongoni mwa waliotangazwa kuwa Mabalozi wa Usafi Dar es salaam leo.

Alikiba @officialalikiba ameongea wakati wa uzinduzi huo ambapo amesema ———"Usafi unaanza na wewe mwenyewe, nina imani kila Binadamu aliyekamilika kichwani kipaumbele cha kwanza ni usafi, usipofanya hivyo utaonekana wa tofauti na watakuuliza Watu"

"Nampongeza sana Mkuu wa Mkoa wa DSM kwa hii kampeni amejali Jamii, tumekua tukiona Wazazi wetu wakituchana nywele, ukiwa Shuleni la kwanza unafundishwa usafi unakwenda na fagio"

"Shule zilitufundisha vitu vingi sana sisemi kwamba walifeli kwa upande mmoja lakini somo la uzalendo lingekuwepo mashuleni hizi Kampeni zisingekuwepo leo maana tungekuwa ndani yetu tunaona kabisa kwamba ni lazima ninapolala, ninapoishi, katika Mkoa wangu ningetamani uwe msafi kama Nchi nyingine za wenzetu huko nje"

"Mimi ni Balozi lakini ningependa niwawakilishe Mabalozi wenzangu ambao ni Wananchi wanaoishi Dar es salaam ningependa tutambue kuwa usafi ni haki yako, usafi ni lazima, naomba RC kama kungekuwa na uwezo wa kushtakiana kwa Mtu akiangusha uchafu apelekwe kwasababu ni haki yako kutetea mazingira "
Screenshot_20211122-203822_Instagram.jpg
 
Msanii Staa wa Bongofleva Harmonize @harmonize_tz amesema kuna vijana wengi wanamfuatilia hivyo ni jukumu lake kuhamasisha suala la usafi jijini Dar es Salaam, Harmonize amempongeza pia Rais Samia Suluhu Hassan kwa jitihada anazo fanya ili kuifanya Tanzania kuwa bora.

Harmonize ambaye ni Balozi wa Usafi na Uhifadhi wa Mazingira Mkoa wa DSM, ameyasema hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa DSM, Amos Makalla wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usafi.

"Ningependa kuwahimiza vijana kwamba usafi ni suala letu la msingi, na najivunia kuwa kati ya vijana wanaohimiza usafi kwani ni haki yetu ya msingi" Harmonize.

Mbali na Harmonize, Wasanii wengine waliojitokeza katika uzinduzi wa Kampeni hiyo ni Alikiba, Steve Nyerere pamoja na Viongozi wengine wa Kiserikali wakiwemo Wakuu wa Wilaya.
Screenshot_20211122-204015_Instagram.jpg
 
Serikali ya Afghanistan ambayo inaongozwa na Wanamgambo wa Taliban imewapiga marufuku Wanawake kushiriki kuigiza Tamthilia na maigizo mengine yanayorushwa kwenye Televisheni nchini humo kupitia 'Miongozo ya Dini' ambayo imetolewa , Miongozo hiyo imezipiga pia marufuku TV kuonesha Tamthilia zilizoigizwa na Wanawake.

Wanamgambo wa Taliban kupitia miongozo hiyo wamepiga pia marufuku TV kurusha vipindi ambavyo vinaonesha Watu wameigiza kwa kuvaa uhusika wa Mtume Muhammad (SAW) na pia Taliban wamezifungia Filamu na vipindi vyote ambavyo vipo kinyume na Uislamu na Maadili ya Afghanistan "Hizi sio kanuni ni Miongozo ya Dini"
Screenshot_20211122-204118_Instagram.jpg
 
Naamini Wayne Rooney anaweza. Ana uzoefu wa kutosha tangu akiwa na umri mdogo kabisa na amepita kwenye changamoto nyingi ngumu kwenye maisha ya uchezaji lakini alifanikiwa kuzikabili. Ana mbinu za uongozi pia, kwa hiyo naamini anaweza kuwa kocha wa Man United siku zijazo.

- Ji Sung Park

Wanapoelekea hawa wanataka kutuua kabisa imeshakuwa team ya majaribio
Screenshot_20211122-204837_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

SIMU YA PROFESA LIGI YA TANZANIA

Ukikaa vijiweni utasikia haiwezekani Simba kubeba ubingwa mara tano mfululizo kivyovyote! Kwanini iwe dhambi? Kwanini kama ana uwezo asichukue?

Profesa anasema hii ni sumu iliyojengwa ambayo mwishowe tutaona mengi ya kutisha, tutaona mengi ambayo hayapo sawa kwakuwa ni dhambi Mnyama kuondoka na tano

Ni ugonjwa wa kidunia, mara nyingi binadamu ana tabia ya kukinai! Huenda watu wamekinai ubora wa Simba, huenda watu wanataka bingwa mpya! Mind you watu wanachukia CONSISTENCY

Profesa anasema "One thing about football is not about football" yani kitu kimoja kuhusu mpira wala hakihusu mpira, kuna vitu vya nje ya mpira vinaathiri mpira duniani kote

Profesa anasema, suala la waamuzi duniani kote ni kupita hatua kwa hatua! Unaweza kuchezesha ligi ya mabingwa mikoa, ukaja Daraja la pili kisha Championship na baadae Ligi kuu

Mna uhakika Waamuzi wetu wanapita kwenye ranks zote? Mna uhakika wana uzoefu wa kutosha? Mtakuja tena kuhoji kwanini Waamuzi wengi hawachezeshi michuano ya Afrika? Majibu mnayo

England hawakuwa na Mwamuzi yoyote WORLD CUP 2018, Walisema wazi hawakupeleka jina la Michael Oliver kwakuwa wanaona hajakidhi, je huku kwetu nani anaassess, je yupo fair? Tujiulize

Profesa anamaliza kwa kusema! Mnapoona Viongozi wanafukuza Makocha bila kuogopa basi mjue wanajua Ushindi unapatikana vipi! One thing about football is not about football

Professor
Screenshot_20211122-205939_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom