Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20211109-050322_Instagram.jpg
 
UKIZINGUA YANGA INAKULA KWAKO
.
Uongozi wa Yanga umesisitiza msimu huu una jambo lao na kwamba hawana muda wa kubembeleza mchezaji, kama akipigiwa simu halafu asipokee au akikosa mechi ajue namba inachukuliwa na wengine.
.
Hayo yamewekwa wazi na mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Hersi Said alipokuwa akihojiwa ambapo alisema hawana nafasi ya kumbembeleza mchezaji kama atashindwa kufuata matakwa na miongozo ya timu kwa sasa kikosini.
.
“Nyie si mmeona kuna mchezaji juzijuzi alifunga bao akamwaga machozi, si mmeona wenyewe. Hakuna anayetaka kupoteza nafasi yake kikosini,” alisema Hersi.
.
“Yanga inalipa mishahara yenyewe. Ina mifumo yake ya kuajiri watu sisi tunasapoti tu. Yanga ni timu kubwa huwezi kufananisha na wengine. Huwezi kumleta mchezaji kama Bangala (Yanick) halafu hajui mshahara analipwa na nani.”

………………
Screenshot_20211109-051008_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom