

Farhan Jr
Nimekuwekea picha tatu za Kocha mpya wa Simba, Mhispania Pablo Martin katika harakati zake za Ualimu wa mpira wa miguu
FRAME 1- NEYMAR JR NA KOCHA WA SIMBA
Hapo kipindi hicho alikuwa anafundisha Getafe klabu ya Ligi Kuu nchini Hispania! Hapo alikabiriana na Barcelona dume ya MSN (Messi, Suarez na Neymar)
Huu ulikuwa msimu wa 2014/15! Getafe walipoteza mchezo pale Nou Camp lakini hii ni CV kubwa ya Kocha! Kupambana na Barcelona iliyobeba ubingwa wa UEFA Msimu huo wa 2014/15
FRAME 2- DIEGO SIMEONE NA KOCHA WA SIMBA
Mchezo huo ulikuwa wa La Liga! Ni Getafe dhidi ya Atletico Madrid kwenye dimba la Vicente Calderon! Hapo ilikuwa kabla ya mchezo wakisalimiana
Kumbuka hii ilikuwa Atletico Madrid dume iliyotoka kucheza fainali ya UEFA dhidi ya Real Madrid dume chini ya Carlo Ancelotti! Lakini huyu Kocha alicheza nayo kwenye Ligi Kuu!
FRAME 3- WACHEZAJI WA REAL MADRID NA KOCHA WA SIMBA
Hii picha ni msimu wa 2014/15 baada ya dakika 90 pale Santiago Bernabeu ambapo Kocha aliingia kusalimiana na wachezaji baada ya mchezo na kuwapungia Mashabiki
Kumbuka hii ilikuwa Real Madrid chini ya King Carlo Ancelotti ambae alitoka kutwaa nao UEFA, nae pia akiwa amefanya makubwa barani Ulaya, ila yeye alicheza nao
FRAME 4- ZINADINE ZIDANE NA KOCHA WA SIMBA!
Niwakumbushe tu kuwa kwenye mechi za Vijana, Zinedine Zidane alikuwa na timu ya Real Madrid Castilla na Kocha wa Simba alikuwa na Getafe B
Mechi iliisha kwa Getafe kuondoka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Castilla ya Zizzou yenye Mastaa Kama Martin Odegaard, Fede Valverde na mafundi wengi kikosini
Mkumbuke mafanikio yake GETAFE B ndio yalimpeleka GETAFE A na alipoondoka timu ya Getafe ikaenda mikononi mwa Escriba alietoka Elche!
CV nzuri na imeshiba let’s wait and see the football