Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,167
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo October 26,2021 amemtembelea Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa na kumjulia hali nyumbani kwake Oysterbay Jijini Dar es Salaam.
Itakumbukwa Mwezi September mwaka huu, Lowassa alimpongeza na kumshukuru Rais Samia kwa kuifanya vyema kazi ya kuijenga Nchi, ambapo alisema ——> "kupitia hotuba yake katika Baraza Kuu Umoja wa Mataifa, Mama Samia amelirejesha tena Taifa letu katika ramani ya dunia"
"Rais Samia amethibitisha pasi na shaka kwamba Tanzania imepata nyota ya jaha kwa kuwa na Kiongozi Mkuu Mwanamke Hodari na Shupavu ambaye leo hii tuna kila sababu ya kujivunia na kumuunga mkono" ——— alisema Edward Ngoyai Lowassa, wakati akimpongeza Rais Samia Mwezi September,2021.
Itakumbukwa Mwezi September mwaka huu, Lowassa alimpongeza na kumshukuru Rais Samia kwa kuifanya vyema kazi ya kuijenga Nchi, ambapo alisema ——> "kupitia hotuba yake katika Baraza Kuu Umoja wa Mataifa, Mama Samia amelirejesha tena Taifa letu katika ramani ya dunia"
"Rais Samia amethibitisha pasi na shaka kwamba Tanzania imepata nyota ya jaha kwa kuwa na Kiongozi Mkuu Mwanamke Hodari na Shupavu ambaye leo hii tuna kila sababu ya kujivunia na kumuunga mkono" ——— alisema Edward Ngoyai Lowassa, wakati akimpongeza Rais Samia Mwezi September,2021.