Makapuku Forum

Makapuku Forum

"Mh. Rais tunakutana leo hapa ili kuipongeza Twiga Stars kwa kutwaa Kombe la COSAFA huko Afrika Kusini tunashukuru kwa Upendo wako kwa kutupa heshima kufika hapa Ikulu tujipongeze pamoja na Wanamichezo wetu"

"Kwa kipindi kifupi cha uongozi wako matokeo chanya kwenye michezo tunayaona , Timu zetu zinaposhinda unatualika hapa Ikulu kwenye mchapalo unafurahi na sisi jambo hili ni kubwa sana Timu zetu zinapata hamasa kukaa na wewe kama hivi na kupata lunch pamoja, tunakushukuru kwa namna unavyotujali Mh. Rais"

"Mh. Rais ulielekeza tuangalie Michezo ya Wanawake, Tamasha la Michezo la Wanawake la Tanzanite lilifanyika kwa Mara ya kwanza September 16-18, 2021 akina Mama walionesha uwezo wao na kuonesha Dunia kuwa wakiwezeshwa wanaweza"

"Tuliweka mkakati wa kurejesha mashindano ya Taifa Cup, hatimaye baada ya Mashindano haya kusimama kwa muda mrefu sasa yatarudi na yataendelea kila mwaka, kwa mwaka huu yatafanyika DSM na kwa uzito wa Mashindano haya na kwa kutambua dhamira yako njema Mh. Rais Samia ya Kuendeleza Michezo tunapendekeza yaitwe Samia Taifa Cup au Kombe la Taifa la Mama Samia" ———
Waziri Bashungwa mbele ya Rais Samia Ikulu Dar es salaam leo
Screenshot_20211028-044116_Instagram.jpg
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameungana na Rais Samia Suluhu kuishukuru Serikali ya Marekani kwa kuipa Tanzania jumla ya dozi 1,058,400 za chanjo aina ya Johnson and Johnson (J&J) kupitia mfumo wa kuwezesha Mataifa yote Duniani kupata chanjo za covid 19 kwa usawa (COVAX Facility) ambapo amesema hadi kufikia jana Oktoba 26, 2021 zilikuwa zimetumika chanjo 1,057,400 sawa na 99.9%, chanjo 1,000 zilizobaki zinaendelea kutumika

Majaliwa ameyasema hayo leo wakati akizindua mradi wa mpango wa Kanisa Katoliki wa mapambano dhidi ya covid 19 katika Hospitali ya Cardinal Rugabwa iliyopo Ukonga Dar es salaam October 27,2021 ambapo amesema dozi nyingine 1,065,600 za chanjo aina ya Sino-pharm zimepokelewa na Serikali ya Tanzania na nyingine dozi 500,000 za chanjo aina ya Pfizer zinatarajiwa kupokelewa siku za karibuni ambapo hadi October 20 2021 Wananchi 20,977 walikuwa wamechanjwa chanjo ya Sinopharm sawa na asilimia 2 ya chanjo hizo zilizosambazwa.
Screenshot_20211028-044241_Instagram.jpg
 
Polisi wa dini ya Kiislamu Hisbah, katika jimbo la Kano Nigeria imemkamata Aliyu Na Idris ambaye alitangaza kuwa anataka anunuliwe kutokana na "umasikini".


Kamanda wa kikosi cha Hisbah, Harun Ibn Sina ameithibitishia BBC kukamatwa kwake, na kuongeza kuwa vitendo vya Aliyu Na Idris ni haramu.

‘’Ndio tulikamata na amekuwa pamoja nasi usiku, kile alichokifanya kinazuiwa katika dini ya Uislamu, huwezi kujaribu kujiuza hata uwe katika hali gani ."


Idris aligonga vichwa vya habari baada ya kutangaza kuwa anajiuza mitandaoni.


"Nitawapa wazazi wangu Naira milioni10 ($24,000; £18,000).
Pia nitalipa naira milioni tano kama kodi ya jimbo kama wataninunua($12,000), nitampatia naira milioni 2 ($5,000) mtu aliyenisaidia kutangaza kuuzwa kwangu. Na pesa zitakazobaki nitazitumia kufanya biashara kwa ajili ya kujikimu katika maisha yangu ya kila siku ."
Screenshot_20211028-045059_Instagram.jpg
 
Hatimaye Bintimfalme wa Japan Mako ameolewa na mpenzi wake aliyesoma naye chuoni Kei Komuro . Ndoa hii inamaanisha amepoteza hadhi yake ya kifalme.


Chini ya sheria ya Japan, mwana mfalme hunyang’anywa mamlaka na hadhi za kifalme anapoolewa na "mtu wa kawaida" ingawa wanafamilia wa kiume hawapotezi hadhi hizo.


Alisusia taratibu za kawaida za harusi ya kifalme na kukataa fidia ya dola milioni $1.3m ambayo kwa kawaida hutolewa kwa wanafamilia wa kike wanapoondoka kutoka familia hiyo.


Amekuwa mwanamfalme wa kwanza wa familia ya ufalme huo wa Japan kukataa hayo yote.


Wawili hao wanapanga kuhamia nchini Marekani-ambako Bw Komuro anafanya kazi kama wakili. Hatua hii imepelekea watu wengi kumlinganisha na wanafamilia ya ufalme wa Uigereza Mwanamfalme Harry, na mkewe bi Meghan Markle na kupewa majina bandia ya "Japan's Harry and Meghan".
Screenshot_20211028-045655_Instagram.jpg
Screenshot_20211028-045714_Instagram.jpg
Screenshot_20211028-045732_Instagram.jpg
Screenshot_20211028-045751_Instagram.jpg
Screenshot_20211028-045808_Instagram.jpg
 
Tesla amejiunga na kundi ndogo la makampuni yenye thamani ya soko ya angalau dola trilioni moja $1t.


Hisa za kampuni ya kutengeneza magari ya kielektroniki zilipanda kwa 12.6% baada ya kufikia makubaliano ya kuuza magari 100,000 kwa kampuni ya kukodisha magari ya Hertz.


Tesla amekuwa mtengenezaji wa magari wa thamani zaidi duniani kwa muda mrefu, lakini makampuni ya kutengeneza magari ya petroli kama Ford na GM zinatengeneza magari mengi zaidi.


Apple, Microsoft, Amazon na wamiliki wa Google, Alfabeti pekee ndio kampuni zenye hisa za thamani ya dola trilioni moja $1tn.


Kampuni hiyo iliyoasisiwa na Elon Musk pia ni kampuni ya pili iliowahi kufikia hatua hiyo muhimu kwa kasi zaidi, ikichukua takriban miaka 11.


Aidha utajiri wa Elon Musk pia umeongezeka hadi kufikia thamani ya zaidi ya dola bilioni 280, akimpiku mwanzilishi wa Amazon Jeff Bezos, kulingana na Bloomberg Billionaires Index.

Screenshot_20211028-050012_Instagram.jpg
 
Mahakama Kuu ya Tanzania, imemuamuru Mmiliki wa Gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba kumlipa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe kiasi cha Sh.Bilioni 6 kama fidia ya kumchafua kupitia vyombo vyake vya habari.

Hukumu hiyo ni ya shauri la kesi namba 220 ya mwaka 2018 na imetolewa na Jaji Joacquine De Mello ambapo amesema mbali na mambo mengine Musiba amlipe Sh.Bilioni 6 Membe, pia inatoa zuio la kudumu la kutomkashifu Membe au kusema uongo dhidi yake na kulipa gharama za kesi.

Mahakama imesema Sh.Bilioni 5 ni fidia ya hasara halisi na Sh. Bilioni 1 hasara ya jumla, katika kesi hiyo Membe alimshtaki Musiba, Mhariri wa gazeti la Tanzanite na wachapishaji wa gazeti hilo ambapo aliwadai Sh. Bilioni 10 kwa kumchafua.

Musiba katika kesi hiyo alishtakiwa kwa kumtuhumu Membe kuwa anamhujumu Rais John Magufuli asitekeleze majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo huku akidai kwamba mbinu mojawapo ya kukamilisha hujuma hizo ni maandalizi anayofanya kugombea urais mwaka 2020 kupitia CCM.
Screenshot_20211028-125657_Instagram.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemhukumu kifungo cha nje cha miezi sita aliyekuwa Rais wa Simba, Evans Aveva kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi huku Godfrey Nyange maarufu Kaburu akiachiwa huru baada ya mahakama hiyo kutomkuta na hatia
Screenshot_20211028-130718_Instagram.jpg
 
Mahakama Kuu (Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi), imeahirisha kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu baada ya shahidi wa tatu wa Jamhuri kushindwa kufika mahakamani.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando ameeleza hayo leo, Oktoba 28, 2021, muda mfupi baada ya shahidi wa pili katika kesi hiyo, Justine Kaaya, kumaliza kuhojiwa na mawakili wa utetezi.

"Mheshimiwa Jaji, shahidi tuliyetarajia kuja kutoa ushahidi hajafika na leo ndio anasafiri kuja, hivyo tunaomba ahirisho la kesi hii hadi kesho, Oktoba 29, 2021" amedai wakili Kidando mbele ya Jaji Joachim Tiganga.
Screenshot_20211028-130825_Instagram.jpg
 
Ronald Koeman OUT |

Klabu ya Barcelona imemfuta Kazi Kocha Ronald Koeman na muda wowote kuanzia leo wataanza mchakato wa kumpata Kocha mpya

Wakati huo Xavi anapigiwa chapuo la kubeba mikoba ya Mholanzi huyo
Screenshot_20211028-131323_Instagram.jpg
 
Mahakama Kuu ya Tanzania, imemuamuru Mmiliki wa Gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba kumlipa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe kiasi cha Sh.Bilioni 6 kama fidia ya kumchafua kupitia vyombo vyake vya habari.

Hukumu hiyo ni ya shauri la kesi namba 220 ya mwaka 2018 na imetolewa na Jaji Joacquine De Mello ambapo amesema mbali na mambo mengine Musiba amlipe Sh.Bilioni 6 Membe, pia inatoa zuio la kudumu la kutomkashifu Membe au kusema uongo dhidi yake na kulipa gharama za kesi.

Mahakama imesema Sh.Bilioni 5 ni fidia ya hasara halisi na Sh. Bilioni 1 hasara ya jumla, katika kesi hiyo Membe alimshtaki Musiba, Mhariri wa gazeti la Tanzanite na wachapishaji wa gazeti hilo ambapo aliwadai Sh. Bilioni 10 kwa kumchafua.

Musiba katika kesi hiyo alishtakiwa kwa kumtuhumu Membe kuwa anamhujumu Rais John Magufuli asitekeleze majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo huku akidai kwamba mbinu mojawapo ya kukamilisha hujuma hizo ni maandalizi anayofanya kugombea urais mwaka 2020 kupitia CCM.View attachment 1989522
ongezea na za fatma karume ....
 
Back
Top Bottom