Ligi ya Mabingwa Afrika inaendelea kesho, unataka kuwashuhudia wawakilishi wa Tanzania pale kwa Mkapa? Kama jibu lako ni ndio kamata tiketi kutoka kituo kilicho karibu yako!
Ugeni wa mashindano unawasumbua Biashara United, hawana uzoefu wa michuano na safari zinakuaje. Kila kitu kwao ni kipya, likitokea tatizo utatuzi wake unachukua muda mrefu.
Kwa mujibu wa Zaka Zakazi, kocha wa Azam FC George Lwandamina amesema timu yake inafanya kama ambavyo anataka na maendeleo yanaongezeka kidogokidogo kadiri siku zinavyozidi kwenda. Anatarajia mchezo mzuri na matokeo yanaweza kupatikana.
Wachezaji wana ari na kila mmoja anautamani mchezo dhidi ya Pyramids FC huku wakiendelea kuhamasishana wao kwa wao
Thierry Henry amekataa kama Mo Salah ndiye bora zaidi duniani kwa sasa:
.
"Mabao ambayo Salah anafunga, kwa sasa, ni mazuri sana. Lakini unawezaje kumsahau Lewandowski? Unawezaje kumsahau Benzema? Unawezaje kusahau inahitajika kufanya hivyo katika mechi za kimataifa pia?"
.
Mnasemaje, nani Bora kwa sasa: Mo Salah; Benzema au Lewandowski ?? [emoji848]
Nabi afichua siri ya Kiwango Bora cha Feisal Salum Feitoto:
.
“Hamjui kwanini amekuwa bora (Fei Toto) nilipoanza msimu nilikaa naye nikamwambia nataka awe bora msimu huu nitakuwa nampanga namba 10, akiwa hapo awe anarudi kukaba pale kati kazi ambayo anaifanya, pia awe akichezesha timu vizuri,” aesema Nabi na kuongeza;
.
“Majukumu hayo anayafanya vizuri sababu ni kijana mdogo ambaye ana nguvu ya kujituma lakini pia nikamwambia kufanya hayo pekee haitoshi, nataka pia afunge mabao kwa mashuti. Najua ubora wa Feisal anajua sana kupiga mashuti makali, ila nilimwambia nataka mashuti yanayolenga lango akiweza afunge, naona sasa ameanza kufanya kile ninachotaka.”
.
“Najua yapo mashuti yatakosa kulenga lango, ila yale yatakayopanguliwa na makipa, najua kuna Mayele. Huyu ni mshambuliaji anayejua kukaa maeneo sahihi sioni kama atakosa kumalizia nyavuni na kuisaidia timu kupata matokeo mazuri,”
Barcelona yajitosa rasmi kwa Mbappe
.
Licha ya Real Madrid kuonekana ina nafasi kubwa ya kuinasa saini ya staa wa PSG na Ufaransa, Kylian Mbappe, 22, dirisha lijalo la majira ya kiangazi dili hilo lipo hatihati ya kufeli.
.
Hiyo inatokana na mabosi wa Barcelona kujitosa kwenye vita ya kuwania saini ya straika huyo ili kuboresha eneo la ushambuliaji. Mbappe ambaye mkataba wake unamalizika mwisho wa msimu alikuwa akitajwa kuwa na nafasi kubwa kujiunga na Madrid dirisha lililopita lakini PSG ilikataa ofa iliyotolewa.
.
Taarifa zinadai Barca inataka kutumia ushawishi wa Lionel Messi na Neymar ili kuipata huduma ya supastaa huyo.
Mo ni mwekezaji ndani ya Simba lakini pia ni shabiki. Kuna mahali anashindwa kutambua yeye ni nani ndani ya Simba. Anaposimama kuongea kama shabiki watu wanamhukumu kama mwekezaji sio kama Mwijaku.
Kwa hiyo Mo ana vitu viwili kwa wakati mmoja lakini akiibuka kama shabiki watu wanaendanae kama mwekezaji.
Timu ikifanya vizuri inakuwa fresh, timu ikifungwa anatafutwa wa kusukumiwa lamawa. Haiwajengi, inazidi kuwabomoa. Simba haijafika hatua ambayo haiwezi kufungwa, yani ikifungwa hadi kuwe kuna mtu kasababisha.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.