Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20211006-072027_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20211006-072041_Opera%20Mini.jpg
 
Orodha ya hati za kusafiria (passport) zenye nguvu zaidi duniani kwa mwaka 2021 imetoka tayari na ifuatayo ni Top 10 ya Nchi hizo, nguvu yake ni idadi ya Nchi ambazo ukiwa na passport mojawapo unaingia kwenye Nchi nyingi bila VISA au ukapewa VISA baada ya kuwasili. (VISA on arrival).

10. Lithuania, Poland, Slovakia (Nchi 182)
9. Hungary (Nchi 183)
8. Australia, Canada (184)
7. Czech Republic, Greece, Malta, Norway, United Kingdom, United States (Nchi 185)
6. Belgium, New Zealand, Switzerland (186).
5. France, Ireland, Netherlands, Portugal, Sweden (187)
4. Austria, Denmark (188)
3. Finland, Italy, Luxembourg, Spain (Nchi 189)
2. Germany, South Korea (190)
1. Japan, Singapore (Nchi 192).

Unataka kufahamu kuhusu Tanzania kwenye orodha hii? list inakuja.
Screenshot_20211006-163330_Instagram.jpg
 
Baada ya kutangazwa Top 10 ya Nchi zilizo na passports zenye nguvu duniani ambalo Japan na Singapore zimeshika namba 1, imetoka orodha pia ya Nchi ambazo passport zake hazina nguvu kabisa duniani.

Nchi hizo ni Korea Kaskazini ambayo passport yake ina ruhusa ya kuingia Nchi 39 tu bila VISA au VISA wakati wa kuwasili, Nepal and Palestinian territories ( Nchi 37), Somalia Nchi 34.

Nchi nyingine ni Yemen Nchi 33, Pakistan Nchi 31, Syria Nchi 29, Iraq Nchi 28 na Afghanistan ndio ya mwisho kwa kuwa na ruhusa ya Nchi 26 tu.
Screenshot_20211006-163433_Instagram.jpg
 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limekanusha taarifa iliyosambazwa mitandaoni ikimuhusisha Rais wa TFF Wallace Karia na suala la uraia wa Mchezaji Kibu Denis.

Taarifa hiyo inamnukuu Rais Karia akisema TFF imemuombea uraia Kibu kwakuwa inamuhitaji na suala la Utaifa wake ni jukumu la Uhamiaji, TFF imesema taarifa hiyo sio ya kweli na Karia hajatoa kauli hiyo kokote na hivyo kuendelea kuisambaza ni kukiuka sheria za makosa ya mtandao.
Screenshot_20211006-163542_Instagram.jpg
Screenshot_20211006-163559_Instagram.jpg
 
Waziri wa Nishati January Makamba Amefika Kigoma baada ya agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Mpango kumuagiza Waziri wa Nishati hadi kufikia October 15, 2021 awe amefika Kigoma ili kutatua kero ya kukatikakatika kwa umeme mara kwa mara ambayo imedumu Mkoani humo kwa zaidi ya miezi miwili.

Mpango alitoa maagizo hayo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Wananchi juu ya kukatikakatika kwa umeme Mkoani kigoma September 22 katika ufunguzi wa maonesho ya tatu ya Shirika la Viwanda Vidogo ( SIDO ) 2021 ambayo Kitaifa yalifanyika Wilayani Kasulu Mkoani kigoma.
Screenshot_20211006-163703_Instagram.jpg
 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi Maafisa mapato watatu wa Halmashauri kwa kushindwa kusimamia mapato katika Wilaya ya Kilwa na kuiagiza TAKUKURU pia iwakamate.

Watumishi waliosimamishwa kazi ni Bahaye Shilungushela, Mohamed Samadu na Ally Kinyonge ambapo wakati Waziri Mkuu anatoa maagizo haya hawakuwepo eneo hilo, Waziri Mkuu Majaliwa leo yupo kwenye ziara ya kikazi Wilayani Kilwa Mkoani Lindi ikiwa ni muendelezo wa ziara zake za kupita kila kona ya Nchi na kufanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo na kutatua kero za Wananchi.
Screenshot_20211006-163756_Instagram.jpg
 
Mamlaka ya chakula na dawa Marekani (FDA) imetoa kibali kwa Maabara ya ACON kutengeneza na kusambaza kifaa cha Mtu kujipima ugonjwa wa covid 19 nyumbani na kwa haraka kiitwacho Flowflex.

Vipimo hivi ambavyo vinafanana na vile vinavyotumika kupima UKIMWI au ujauzito kwa haraka hata Mtu akiwa nyumbani, vina uwezo wa kutoa majibu kwa haraka ndani ya dakika chache tangu Mtu alipojipima.

Kifaa hiki kitasaidia kuongeza idadi ya Watu wanaopima na hivyo kupunguza usumbufu wa Watu kwenda mpaka Hospitali na vilevile vitapunguza gharama za upimaji lakini Wataalamu wa Afya wamesisitizwa umuhimu wa kuwapa elimu Watu ya jinsi ya kujipima.

Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu Maabara hiyo inatarajia kutengeneza zaidi ya vifaa vya kujipimia Milioni 100 na kufikia Mwezi February mwakani vitakuwa vimetengenezwa vifaa Milioni 200.
Screenshot_20211006-163909_Instagram.jpg
 
“Niko Kigoma na Kasulu na Ndugu Chande, MD-TANESCO kama alivyoelekeza Mh. Makamu wa Rais, tunamaliza tatizo, Kigoma ipo nje ya Gridi kwahiyo TANESCO inatumia Bilioni 3 kwa mwezi umeme wa dizeli kwa Wateja 63,000 wanaolipa Bilioni 1.5.tunaleta Gridi Kigoma mwakani” ——Waziri wa Nishati January Makamba
Screenshot_20211006-164011_Instagram.jpg
Screenshot_20211006-164042_Instagram.jpg
 
Hukumu ya kesi ya aliyekuwa Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na aliyekuwa makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ imekwama baada ya Aveva kushindwa kufika mahakamani.

Hukumu hiyo ilikuwa imepangwa kutolewa leo Jumatano, Oktoba 6, 2021 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Dar es Salaam, Kisutu, Thomas Simba.

Hata hivyo kutokana na Aveva kutokuwepo mahakamani, mahakama hiyo imeshindwa kusoma hukumu hiyo na badala yake imeiahirsha hadi Oktoba 21, mwaka huu.

Kaburu ambaye ndiye pekee aliyefika mahakamani kusikiliza hukumu hiyo ameieleza mahakama hiyo kuwa Aveva ameshindwa kufika kuwa yuko hospitalini kwa ajili ya kliniki.
Kaburu amesema kuwa Aveva anahudhuria kliniki hiyo kila Jumatatu, Jumatano na Ijumaa.
Screenshot_20211006-164302_Instagram.jpg
 
Wakati Mkurugenzi wa jiji la Mwanza, Selemani Sekiete akitoa tangazo la kuwataka wamachinga kuondoa biashara zao kwenye barabara zao kwenye maeneo ya waenda kwa miguu na mbele taasisi za Umma na binafsi hivi karibuni, wafanyabiashara hao sasa wameanza kuondoka katika maeneo hayo na kuingia katika soko la Mbugani jijini humo.

Mwananchi Digital imeshuhudia leo Oktoba 6, gari la matangazo likielekeza mama lishe wanaofanya biashara zao katika barabara, maeneo ya waenda kwa miguu na kwenye mitaro kuhamishia biashara hizo ndani ya maeneo yaliyoelekezwa.

Baadhi ya wafanyabiashara walionekana wakiondoa wakitii agizo hilo kwa kuondoa bidhaa zao kwenye maeneo yasiyoruhusiwa.
Screenshot_20211006-164406_Instagram.jpg
 
"Tuwe na utaratibu wa watu wanaofanya vizuri wapongezwe ili wafanye vizuri zaidi lakini wanaoharibu wapewe adhabu. Kinyume chake hapa kwetu mtu anaharibu lakini anapewa cheo siyo utaratibu mzuri.
Uongo uongo umekuwa mwingi sana nchini hasa simu zimekuwa kichocheo cha kuhari vijana," - Amesema Professa Assad
Screenshot_20211006-164547_Instagram.jpg
 
"Tofauti ya binadamu na kondoo ni kuwa Kondoo akipata maji na nyasi basi anasubiri kuchinjwa wakati binadamu anahitaji maendeleo na demokrasia.
Unaweza kutafuna chungwa na ukatembea na wakati huo ukamkonyeza binti mzuri," amesema Jenerali Ulimwengu
Screenshot_20211006-164636_Instagram.jpg
 
"Bado siamini kama katiba mpya inaweza kutoa suluhisho la mambo yanayolalamikiwa hadi wawepo watu wenye msimamo na taasisi na viongozi wawe na msimamo.
Katiba ya wananchi ndiyo Katiba isiwe ya wachache," amesema Profesa Mussa Assad
Screenshot_20211006-164817_Instagram.jpg
 
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) wa zamani, Profesa Mussa Assad amesema hapendi kuitwa mstaafu na neno hilo linamchukiza, akidai kuwa taratibu za kumwondoa hazikufuatwa.

Hata hivyo taarifa iliyotolewa na Serikali mwaka 2019 ilieleza kuwa Profesa Assad kipindi chake kilimalizika Novemba 4, 2019

Profesa Assad ameyasema hayo leo Oktoba 6 jijini Dodoma wakati wa mdahalo juu ya kitabu cha Rai ya Jenerali kinachozungumzia umuhimu wa Katiba Mpya.

"Sipendi sana kusikia neno mstaafu na kwamba neno hilo linaniudhi linapotamkwa mbele yangu," amesema Profesa Assad.

Profesa Assad aliteuliwa na aliyekuwa Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete kuwa CAG Novemba 5, 2014 na aliondolewa Novemba 4, 2019.

Kabla ya kuondolewa kwake, ulizuka mvutano kati yake na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Job Ndugai, uliosababisha Profesa Assad kufikishwa kwenye Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na madaraka ya Bunge akidaiwa kudharau mhimili huo kwa kauli yake kuwa Bunge ni dhaifu.
Screenshot_20211006-164915_Instagram.jpg
 
Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia mkataba na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuwa mdhamini wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa miaka mitatu (2021-24) ambapo kwa msimu wa 2021/22 mkataba utakuwa na thamani ya Sh2.5 bilioni kabla ya VAT na misimu miwili ijayo maongezi yanaendelea.

Sasa rasmi itatambulika kama NBC PREMIER LEAGUE / LIGI GUU YA NBC

Screenshot_20211006-165010_Instagram.jpg
 
Imeelezwa kuwa wanawake 474 wamefanyiwa ukatili wa aina tofauti mwaka 2020 Mjini Babati Mkoani Manyara, ikiwemo ukatili wa kimwili matukio 249, ukatili wa kingono 48 na kijinsia 117.

Ofisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri hiyo, Mathias Focus ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na wanawake na wasichana wa Kata ya Riroda waliopo kwenye mradi wa haki ya afya ya uzazi unaosimamiwa na klabu ya waandishi wa habari Mkoani Manyara (MNRPC) kwa ufadhili wa taasisi ya Women Fund Tanzania Trust (WFT).

Focus amesema watu wanaofanyiwa ukatili mwingi wa kimwili, wanawake wamekuwa wakivutwa nywele kwa kukosea kupika na wengine kuambulia kichapo.

Amesema ukatili wa kihisia unaharibu ubongo huku akisema mara nyingine kuna maneno ya fedheha wanafanyiwa akitoa mfano mtoto kutukanwa na baba yake pale anapokosea.
Screenshot_20211006-165105_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom