Makapuku Forum

Makapuku Forum

WAKONGO WAWILI WATIMKA YANGA
.
Winga Jesus Moloko aliyefunga bao lake la kwanza tangu atue Yanga ametimka juzi usiku sambamba na beki Djuma Shaban wakirejea kwao DR Congo.
.
Inaelezwa kwamba wachezaji hao wawili wamerejea kwao kupata pasi mpya za kusafiria baada ya zile za awali kujaa ambapo wakirejea wataungan na wenzao kambini Karatu Arusha kabla ya kurudi tena kwenye pilikapilika za mechi za Ligi Kuu, wakiwafuata KMC mjini Songea.
.
KMC imeamua kulipeleka pambano lao wakiwa kama wenyeji litakalopigwa Oktoba 19 mjini Songea.
Screenshot_20211005-112627_Instagram.jpg
 
Kibwana aitwa Stars
.
Beki wa Yanga, Kibwana Shomari amejumuishwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa kinachojiandaa na mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la Dunia dhidi ya Benin utakaopigwa Oktoba 07.
.
Awali kocha wa timu ya taifa, Kim Poulsen aliita kikosi cha nyota 25 huku jina la beki huyo likikosekana na sasa rasmi atakuwa miongoni wa wachezaji watakaoshuka katika dimba la Benjamin Mkapa.
.
"Tumepokea taarifa ya wito wa Kibwana. Na kwa heshima tumemruhusu akajiunge na timu ya Taifa,"amesema Hassan Bumbuli.
Screenshot_20211005-112755_Instagram.jpg
 
[emoji3578][emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

KWANINI TIMU NYINGI ZINAPATA TABU MWANZONI MWA MSIMU?

Nilipofika Jijini Dodoma kwenye mchezo wa Dodoma Jiji na Simba nilipata wasaa wa kukaa na Watalaam mbalimbali, kuna Kocha mmoja mkubwa nilimuuliza swali

Kocha kwanini Simba huwa wanaanza msimu wakiwa hawapo imara, misimu zaidi ya mitatu sasa! Mwalimu yule wa timu tofauti na Simba akaanza kunipa elimu yake

Kwanza hoja ya KUTUMIKA! akaniambia 80% ya wachezaji wa Simba ni wa timu za taifa, 80% ya wachezaji wa Simba wamecheza mechi zaidi ya 40 hapo uchovu ni lazima ndio maana waaanza taratibu

Hii ni hoja ya uchovu, akaniambia ina maana kubwa sana! Hivyo Mwalimu analazimika kufanya rotation mpaka maeneo hatarishi ili kubalance vyema mzigo huo! Wachezaji wao wametumika sana

Hapo nikamuelewa Mwalimu yule kwenye hoja hiyo, yeye anasema suala sio chemistry, anasema ni suala la muda tu watapick kuanzia game ya tano

Nikataka kujua kwanini wachezaji wa Simba wanaumia sana? Safari yangu Dodoma ilinipeleka kwa Daktari mmoja wa timu ya Ligu kuu maeneo ya shule ya Sekondari, John Mallen baada ya stori kadhaa nikamuuliza hilo swali

Akaanza kwa kucheka kidogo na kuniambia hapa nakujibu kama Mwanataaluma sio Daktari wa timu flani, kisha akaanza kutoa nondo "ukiona Wachezaji wanaumia sana na wanaanza kwenye gia ndogo maana yake hao wamefanya Pre season ya kweli kabisa"

Akaniambia kuna kitu kinaitwa WATER THERAPY kitaalamu kabisa! Akaniambia Wachezaji wanapoingizwa sana kwenye barafu ni kuwa wanafanyiwa Natural healing, yani kujua sehemu mbalimbali za majeraha yao mwilini

Akaniambia Simba wanafanya sana WATER THERAPY, ikumbukwe hata kama una maumivu ya miaka 10 iliyopita kupitia hii itagundulika na utapewa tiba sahihi, sasa ile tiba huwa ina muda kabla wachezaji kukaa sawa

Nikahoji hapo hapo!.....

ITAENDELEA
 
[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

YUSUPH ATHUMAN NA MAKAMBO, SIMULIZI YA MWALIMU NA MWANAFUNZI

Wakati nyasi za Allianz Arena pale Munich zinafuka moshi ya ukungu wa baridi kali sana, ni fainali ya UEFA hiyo ni Chelsea hao dhidi ya Bayern Munich ilikuwa 2012

Kinda Ryan Bertrand alionekana kama anapitia magumu eneo la kushoto, akatoka Frank Lampard mchezaji Mwandamizi akamuuliza Bertrand! "Kijana hii ni nini?" Ryan akajibu hii ni fainali ya UEFA

Lampard akamwambia "play the game not the ocassion" akimsihi asahau kuwa ni fainali ya UEFA, acheze kama mechi zingine, baada ya hapo Ryan alikuwa bora sana baada ya Legend kusema nae

Wakati Ronaldo anapitia magumu sana ilikuwa United vs AC Milan 2005 hiyo! Ronaldo anakula viatu kutoka kwa Gatusso mpaka anapanic! Ndipo Keane alimpa ule msemo maarufu zaidi England

Keane alimfuata Ronaldo na kumwambia "This is football Kid, either go hard or go home" alimwambia akomae ama aende nyumbani, Magwiji wana namna yao ya kuwaelekeza vijana wadogo kwenye soka

Nikurejeshe mpaka nchini Tanzania kwenye stori ya Kinda Yusuph Athuman na Heritier Makambo siku moja pale Avic Town Kigamboni kwenye mazoezi ya kila siku

Wakati Makambo na Yusuph wapo timu moja, zikipigwa ndefu Yusuph anacontrol anamsubiri Makambo kwenye njia anamuwekea kisha Makambo anaweka, hii ilijirudia kama mara nne hivi

Makambo akamuita Yusuph akamwambia njoo ucheze napocheza kisha niende unapocheza! Ulipigwa mpira mrefu, Makambo akaucontrol, on space yupo Yusuph, Makambo akaweka kambani mwenyewe

Kisha akamuita Yusuph kama Mdogo wake na kumwambia "Mdogo wangu napenda kitu chako cha kwanza cha kuichezesha timu, nataka pia uwe imara zaidi na zaidi kwenye hiki cha pili, nifuate"

Yusuph anapokea darasa zuri sana kutoka kwa Mayele na Makambo, wanampenda kama Mdogo wao na wanafanya kazi kama Kaka zake, hii ni faida kwa Yanga na Taifa letu
Screenshot_20211005-113341_Instagram.jpg
Screenshot_20211005-113408_Instagram.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan ameelekeza kupunguzwa kwa tozo zinazotozwa na Taasisi mbalimbali katika bidhaa za mafuta hapa nchini zenye thamani ya shilingi Bilioni 102 kwa mwaka ili zifanye bei za mafuta kupungua na kuwapa unafuu Wananchi, ametoa haya maagizo leo wakati akipokea taarifa kutoka kwa Waziri wa Nishati, January Makamba kuhusu utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa kwa Wizara hiyo kupitia mwenendo wa biashara ya mafuta na bei zake.

Taasisi zinazoguswa na maelekezo ya kupunguzwa kwa tozo hizo ni Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (tozo ya udhibiti), Mamlaka ya Bandari (tozo ya miundombinu), Mamlaka ya Mapato Tanzania ( tozo ya kuchakata taarifa), Shirika la Viwango Tanzania ( tozo ya kupima ubora wa mafuta kwenye meli na gharama ya uwekaji wa vinasaba kwenye mafuta), Wakala wa Vipimo Tanzania (tozo ya uhakiki wa ujazo wa mafuta melini), Wakala wa Usimamizi wa Meli (tozo ya forodha) na Mamlaka ya Serikali za Mitaa (ushuru wa huduma kwenye Halmashauri nne zenye maghala ya kupokea mafuta kwa jumla).

Halmashauri hizo ni Kigamboni na Temeke za Jijini Dar es Salaam, Tanga na Mtwara, Rais Samia ameagiza ufanyike mchakato wa haraka wa kupeleka marekebisho ya Sheria Bungeni endapo zipo Sheria nyingine zinazohitaji marekebisho ya haraka katika kukabiliana na kupanda kwa bei za mafuta.
Screenshot_20211005-142411_Instagram.jpg
 
“Tumepokea maelekezo ya Mh. Rais na leo tuta-gazette upunguzaji wa tozo 8 za Serikali zinazochangia kwenye bei za mafuta ili kupunguza makali ya ongezeko la bei za mafuta duniani, kuanzia kesho Taasisi kadhaa zitaacha kukusanya jumla ya Bilioni 101 ili kutoa nafuu kwa Wananchi” ——— asema Waziri wa Nishati January Makamba.
Screenshot_20211005-144626_Instagram.jpg
 
Eti kazini kwangu anaichanganye kichwa [emoji1787]
Mmh weeh sio kweli
Weeh beer tamu [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Maisha mafupi babe [emoji8] ukikunja sura utazeeka

Usikunje sura utazeeka
Usikunje sura utazeeka

Usibane bane sana utazikwa nalo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Asikwambie mtu tu tu beer tamu
Beer beer mitungi beer tamu
Ah beer tamu. [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom