Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20211007-064408_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20211007-064420_Opera%20Mini.jpg
 
Alhamisi ya leo, Nchi ya Finland imetangaza kusitisha utumiaji wa chanjo ya Moderna (MRNA.O) ya COVID-19 kwa Wavulana kwa sababu ya ripoti za athari nadra za moyo na mishipa zinazoweza kusababishwa na chanjo hiyo, hata hivyo Finland haitokuwa Nchi ya kwanza kusitisha kwani Sweden na Denmark nazo zimetangaza usitishaji kama huo jana.

"Utafiti wa Nordic uliohusisha Finland, Sweden, Norway na Denmark uligundua kuwa wanaume walio chini ya umri wa miaka 30 ambao walipokea Moderna Spikevax walikuwa na hatari kubwa kidogo kuliko wengine wa kupata myocarditis," alisema.

Maafisa wa afya wa Sweden na Denmark walikuwa wametangaza jana Jumatano kwamba watasitisha matumizi ya chanjo ya Moderna kwa Vijana wote na Watoto huku wakitolea mfano wa utafiti huohuo ambao haujachapishwa.
Screenshot_20211007-205342_Instagram.jpg
 
Mtanzania Abdulrazak Gurnah ambaye ni Mtunzi maarufu wa vitabu ameshinda Tuzo ya Nobel ya Fasihi, tuzo hii imetangazwa Stockholm Nchini Sweden na Mats Malm ambaye ni Katibu wa Kudumu wa Swedish Academy.

Gurnah alizaliwa Zanzibar mwaka 1948 na ni Profesa wa Chuo Kikuu cha Kent, Uingereza ambapo ameandika riwaya takribani 10 na kitabu chake cha kwanza kinaitwa 'Memory of Departure' ambacho kilichapishwa mwaka 1987, vitabu vingine ni pamoja na 'Paradise' n.k ambavyo vinatajwa kuchochea mabadiliko makubwa kwenye Jamii ikiwemo kuelezea athari za ukoloni na hatima ya Wakimbizi.
Screenshot_20211007-205728_Instagram.jpg
Screenshot_20211007-205747_Instagram.jpg
 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ambae siku zote pamoja na mambo mengine husifika kwa misimamo na uzingatiaji wa ubora wa miradi mbalimbali ya Serikali, leo akiwa katika siku ya Pili ya ziara yake Mkoani Lindi amegoma kuzindua barabara ya Liwale Mjini ya kilometa 1.2 kwa sababu haijawekwa taa za barabarani.

“Mkataba ni kujenga barabara za kiwango cha lami zenye taa, leo mnaniambia nizindue barabara haina taa, hii haijakamilika, leo sizindui sababu hamna taa, hayo ni maelekezo ya Rais Samia barabara ya kilometa 1.2 iwe na taa, siku yoyote nitakuja leo siwezi kuzindua”

Taa za barabarani ni moja ya vitu muhimu vinavyopendezesha miji kama inavyoonekana kwenye Miji mbalimbali ikiwemo Lindi mjini kwenyewe ambako kumewekwa taa hizo ambazo licha ya kupendezesha mji, pia zinasaidia usalama na kuruhusu Watu kufanya shughuli zao hadi usiku.
Screenshot_20211007-205857_Instagram.jpg
Screenshot_20211007-205915_Instagram.jpg
 
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeidhinisha rasmi kuanza kutumika kwa chanjo ya Malaria kwa Watoto wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara na katika maeneo yaliyo hatarini hususani Afrika ambako Malaria inaua zaidi ya Watoto 260,000 walio chini ya miaka mitano kila mwaka.

Tangu mwaka 2019, Nchi tatu za Kusini mwa Jangwa la Sahara, Ghana, Kenya na Malawi, zilianza kutumia chanjo hiyo kwa majaribio katika maeneo yaliyochaguliwa ambapo maambukizi ya Malaria yamekuwa yakiongezeka.

Chanjo nyingine iliyotengenezwa na watafiti katika Chuo Kikuu cha Oxford na Burkina Faso imeonekana kuwa na ufanisi wa 77% katika majaribio ya awamu ya 2, awamu ya 3 itakamilika katika miaka miwili.

Mbunge wa Kigamboni ambaye pia ni Daktari, Dr. Faustine Ndugulile amepongeza hatua ya chanjo ya Malaria kutolewa Afrika na anasema Ifakara Institute walihusika kwenye mchakato wa majaribio.
Screenshot_20211007-210107_Instagram.jpg
 
"Nilitaka kuboresha Uwanja wa Karume lakini ilitokea siasa ila namshukuru ndugu yangu Paul Makonda alinipa kiwanja Kigamboni kwa kushirikiana na Serikali ya wilaya ya Kigamboni kwahiyo tukaamua Karume nisiparekebishe nitengeneze mpango mwingine"

"Kwasababu bado nilikuwa naona michakato haiishi nikaamua kujenga kituo cha Kigamboni kitakuwa kimefanana na kile cha Mkwakwani Tanga lakini Kigamboni itakuwa ni Centre kubwa zaidi ya kimichezo ya kuiunganisha mikoa yote" ——— asema Wallace Karia, Rais wa TFF.
Screenshot_20211007-210257_Instagram.jpg
 
Club ya Azam FC imethibitisha rasmi kuwa imewafungia kwa muda usiojulikana Wachezaji wake watatu ambao ni Nahodha Aggrey Morris na Wasaidizi wake Mudathir Yahya na Salum Abubakar.

Sababu za maamuzi hayo katika taarifa ya Azam FC inaeleza kuwa hiyo inatokana na Wachezaji hao kwa umoja wao kumtolea maneno yasiyo na staha Meneja wao timu Luckson Kakolaki kwa nyakati mbili tofauti September 18 2021 siku ya mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika wa Azam FC vs Horseed SC ya Somalia.
Screenshot_20211007-211022_Instagram.jpg
Screenshot_20211007-211045_Instagram.jpg
 
Rais wa Zanzibar Dk Hussein Mwinyi atapokea ndege mbili mpya aina ya Airbus zitakazowasili kesho Ijumaa Oktoba 8, 2021 visiwani Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Arusha leo Waziri wa ujenzi na uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema ndege hizo zitakuwa na uwezo wa kubeba abiria 132, na kati ya hao 12 wa daraja la biashara na 120 daraja la uchumi.

Ndege hizo mpya moja itapewa jina la Zanzibar na nyingine Tanzanite.
Screenshot_20211007-211458_Instagram.jpg
 
Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura) mkoa wa Dar es Salaam, Geofrey Mkinga amesema wataweka vibao vya alama kwenye maeneo tatanishi ili wananchi waelewa vema maegesho ya magari.

Hatua hiyo, imetokana na malalamiko kutoka kwa baadhi ya watu wanaodai kutojua maeneo sahihi ya maegesho ya magari yanayomilikiwa Tarura na hivyo kutozwa ada za maegesho ya gari kupitia mfumo mpya wa malipo tofauti na ule wa awali walipokuwa wakilipa fedha taslimu wakiwa eneo la tukio.

Maelezo hayo ameyatoa leo, Alhamisi Oktoba 7, 2021 wakati akizungumza na Mwananchi Digital kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo malalamiko ya watumiaji wa maegesho yanayomilikiwa na taasisi hiyo katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Dar es Salaam.

“Tuna mpango huo katika bajeti ya mwaka huu, tumetenga fedha ajili ya maboresho hayo ikiwemo kuweka vibao yale maeneo tatanishi. Lakini maeneo mengine ni uelewa mfano nje ya uzio wako sio eneo lako bali ni hifadhi ya barabara na kama kuna eneo basi ni maegesho,” amesema Mkinga.
Screenshot_20211007-211635_Instagram.jpg
 
Timu imecheza vizuri ila Benin walikuwa bora kwa Mchezaji mmoja mmoja ikaamua matokeo.

Tanzania tumejitahidi wachezaji wametengeneza nafasi ila Benin wameoneka kama wamekuja kwa lengo moja kutafuta alama moja, Kadri muda ilivyokuwa unaendelea plan yao ndani ya Uwanjani ikabadilika, class ya kwao na class yetu ni tofauti

Wakatumia ubora wao, tamaza yule Mchezaji aliyetufunga alipata nafasi moja tena akiwa mbali na nafasi hiyo ilikuwa ni Moja ya nafasi ngumu kwake hiyo hiyo ikaamua mchezo,

Kwaiyo Mimi naamini class, mbinu na hamasa za timu zinaamuliwa na ubora za wachezaji

Mwisho wa siku Benin wametumia ubora wao wa Mchezaji mmoja mmoja sasa hatupaswi kuanza kumlaumu Mwalimu na kuilaumu timu tutakuwa tunakosea

Timu imecheza vizuri lakini Class imeamua, nafasi waliyoipata Benin ni Moja ambayo iliamua mchezo, sisi tulipata nafasi ambazo tulishindwa kuzitumia ndo kama hivyo.

Mwandishi wa Habari za Michezo Charles Abel akielezea mchezo wa kufuzu kombe la Dunia Qatar, Tanzania dhidi ya Benin.
Screenshot_20211007-211913_Instagram.jpg
 
Fikayo Tomori baada ya maisha magumu London akaelekea Milan na sasa ameitwa National team

Tammy Abraham baada ya maisha magumu London akaelekea Roma na sasa ameitwa National team

Kuna wakati unapaswa kusafiri ili ufikie lengo
Screenshot_20211007-212341_Instagram.jpg
 
"Nisingependa kuliongelea sana hili suala la mchezaji Kibu Denis kwa sababu lipo kwenye taasisi ya Serikali lakini mchezaji huyu alionekana kwenye usajili wetu kwa maana ya kwa kwamba alichezea timu ya Geita.

"Tunapokwenda kwenye mashindano wachezaji wetu mara nyingi kitambulisho chao ni passport tukaanza michakato ya kuwatafutia wachezaji passport sio yeye tu na wengine hawakuwa navyo bahati nzuri tulimkuta na kitambulisho cha Taifa tukapeleka uhamiaji na kule uhamiaji kuna vitu wanataka kama udhibitisho wa wazazi wake.

Tukamuuliza wazazi wake wako wapi? Alituambia. Kwahiyo Uhamiaji walifanya kazi yao wakapata taarifa wakatujibu kuwa sio raia wa Tanzania na kama inawezekana kama Serikali ina nia ya kumpa uraia basi apewe. Na Kibu hazuiwi kuchezea Simba.”

- Wallace Karia, Rais TFF
Screenshot_20211007-212435_Instagram.jpg
 
“Kuna vitu nilidhamiria kufanya wakati naingia na sikuwaangusha na vilifanyika. Vingine vinatakiwa bado viendelee. Wamenipa tena ridhaa hiyo nami naahidi nitafanya na mengi niliahidi kuyafanya nitayafanya ili mpira ufike kule mbali ambapo tunatarajia ufike" Wallace Karia, Rais TFF.

- Wallace Karia, Rais TFF.
Screenshot_20211007-212616_Instagram.jpg
 
“Hongera sote lakini tupongeze mpira wa miguu Tanzania kwamba una bahati. Kwanza nawashukuru wajumbe wa mkutano Mkuu walionesha imani kubwa kwangu.

Kutokana na katiba yetu tuna taratibu mbalimbali kama kupata udhamini, nilipata wadhamini wa kutosha lakini wapo wengine walikataa kutoka udhamini kwa wengine wakisema hawaoni mtu mwingine kwakuwa waliona nastahili niendelee kuwepo kwenye uongozi"

"Nashukuru ingawa kulikuwa na kelele nyingi lakini michakato yote ilienda vizuri na mambo yote yalikwisha"

- Wallace Karia, Rais TFF.
Screenshot_20211007-212717_Instagram.jpg
 
Nilitaka kuboresha uwanja wa Karume lakini ilitokea siasa ila namshukuru ndugu yangu Paul Makonda (aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam) alinipa kiwanja Kigamboni kwa kushirikiana na Serikali ya wilaya ya Kigamboni.

Kwa hiyo tukaamua Karume nisiparekebishe nitengeneze mpango mwingine na ile fedha ya viwanja bado nilikuwa nayo na kwa sababu bado nilikuwa naona michakato haiishi nikaamua kujenga kituo cha Kigamboni kitakuwa kimefanana na kile cha Mkwakwani Tanga lakini Kigamboni itakuwa ni Centre kubwa zaidi ya kimichezo ya kuunganisha mikoa yote.

- Wallace Karia, Rais TFF.
Screenshot_20211007-212717_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom