Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waamuzi wa Tanzania Ramadhani Kayoko, Frank Komba, Soud Lila na Elly Sasii wameteuliwa na caf kuchezesha mchezo wa Kombe la Shirikisho barani Afrika kati ya Cffa (Madagascar) na Grupo Desportivo Interclube (Angola) utakaochezwa kwenye Uwanja wa Mahamasina, Madagascar, Oktoba 17,2021.
Screenshot_20211004-151100_Instagram.jpg
 
Septemba 2020, Ronald Koeman alimpigia simu Luis Suarez kumwambia kuwa hayupo sehemu ya mipango yake

Oktoba 2021, Luis Suarez anaweka kamba na Assist dhidi ya Barcelona

Maisha yanaenda kasi sana
Screenshot_20211004-151205_Instagram.jpg
 
Kampuni ya Facebook imethibitisha kwamba Mitandao yake ya Facebook,Instagram na WhatsApp imerudi hewani baada ya kupata tatizo na kufanya baadhi ya Watumiaji kushindwa kufanya chochote kwenye Account zao, kwenye taarifa yao wameomba radhi Wateja wao wote Duniani.
Screenshot_20211005-074813_Instagram.jpg
Screenshot_20211005-074904_Instagram.jpg
 
Mchezaji wa Simba SC Kibu Dennis ambaye hivi karibuni Kocha Mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen alimuacha kikosini kwa madai ya kushughulikiwa kwa suala la utata wa uraia wake, leo amerejeshwa kikosini ikiwa ni siku chache zimepita toka mamlaka zitangaze kuwa amepatiwa uraia, Kibu leo amejumuika na Wachezaji wenzake wa Taifa Stars wanaojiandaa na michezo miwili ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar dhidi ya Benin.
Screenshot_20211005-104526_Instagram.jpg
 
Utajiri wa Mwanzilishi na C.E.O wa Facebook, Mark Zuckerberg umeanguka kwa wastani wa USD 5.9 B hadi 7 kwenye saa ambazo mitandao ya Facebook, Instagram na WhatsApp ilipata tatizo la kimtandao, kwa sasa Mark yupo No. 6 kwenye orodha ya Matajiri Duniani akiwa na utajiri wa USD 116. 8 B kwa mujibu wa Forbes.View attachment 1963534
Screenshot_20211005-104838_Instagram.jpg
 
Siku moja baada ya wakazi wa Mbezi Makabe wilayani Ubungo kueleza namna wanavyotumia saruji na majivu kusafisha maji, wataalamu wameeleza kwa undani.
Suala hilo liliibuka juzi katika hafla ya utilianaji saini utekelezaji wa mradi wa maji wa Mshikamano uliofanyika kituo cha Mbezi Makabe jijini Dar es Salaam.

Mradi huo wenye thamani ya Sh5.4 bilioni unatekelezwa na kusimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (Dawasa).

Wakati hali ikiwa hivyo baadhi ya wataalamu wa maji akiwemo Mhandisi Herbert Kashilila wa Shirika la Shahidi wa Maji alisema matumizi ya saruji na majivu hayana shida kwa kuwa hayo ndio yanatumiwa kusafisha maji kwenye mito kwenda kwenye matumizi ya binadamu.

Wakazi wa Mbezi Makabe wanategemea maji wanayochota kwenye mashimo ambayo mengi yamekauka.

Imeelezwa kuwa wanaamka saa kumi alfajiri kuwahi maji kwani ikifika saa nne yanakuwa yameisha.

Screenshot_20211005-105754_Instagram.jpg
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe, limemhoji Mbunge wa Mbozi, George Mwenisongole kwa tuhuma za kumpiga na kumjeruhi, Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya Mbozi, Ignas Kinyowa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Janneth Magomi ameyasema hayo jana Jumatatu Oktoba 4, 2021.
Screenshot_20211005-105929_Instagram.jpg
 
Huduma za mitandao ya kijamii ya Facebook, WhatsApp na Instagram zimerejea baada ya kutopatikana kwa saa nane.

Kupitia taarifa ya Facebook imeeleza kuwa sababu ya kutoweka kwa mitandao hiyo ni mifumo kutofanya kazi.

Huduma zote tatu zinamilikiwa na Facebook na hazikuweza kupatikana kwenye wavuti au kwenye programu za simu za mkononi.

Katika taarifa hiyo iliyotumwa usiku wa kuamkia leo Jumanne Oktoba 5,2021 imesema mabadiliko mabaya ya usanifu yaliathiri zana na mifumo ya ndani ya kampuni hiyo.
Screenshot_20211005-110031_Instagram.jpg
 
Sure Boy, Mudathir, Moris wapigwa Stop Azam
.
"Ni mwezi sasa tangu tusimamishwe na kifupi hakuna ambaye anajua kati yetu ni kwa nini labda tumesimamishwa yaani unavyoona huko mitandaoni watu wakiongea na sisi tunaona hivyo hivyo hatujui chochote na hakuna ambaye
kati yetu anajua sababu ya kusimamishwa kwa muda usiojulikana,"
.
Kwa upande wa Mtendaji Mkuu wa zamani wa Azam, Saad Kawemba kuhusu wachezaji Aggrey Morris, Mudathir Yahya na Sure Boy:
.
“Unaposimamisha mchezaji inbidi ujiangalie je Unafaidika au unamnufaisha uliyemsimamisha? Kwa sababu ukiangalia Azam wanashindwa kunufaika kutokana na matokeo wanayopata, hivyo viongozi walipaswa kutumia njia mbadala kwenye adhabu ili kupata kilicho bora kwao.”
Screenshot_20211005-112312_Instagram.jpg
 
Morrison Ampa Jeuri Gomes
.
Kocha Mkuu wa Simba, Didier Gomes, amefunguka kuwa kurejea kwa kiungo mshambuliaji wake, Bernard Morrison hususani katika mchezo wao ujao wa Ligi ya Mabingwa Afrika ni miongoni mwa vitu vinavyowapa matumaini makubwa ya kufanya vizuri.
.
Gomes amesema: “Michezo mitatu iliyopita imekuwa ya faida kubwa kwetu kutuandaa na mashindano mbalimbali tutakayoshiriki mwaka huu, kwa namna ninavyokiona kikosi changu nashawishika kusema Tupo tayari.
.
"Tuna mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika michuano ambayo ni muhimu kwetu, lazima tujiandae kufanya vizuri katika hatua hii na ni jambo zuri kuona tuna nafasi ya kumtumia tena Bernard Morrison katika mashindano hayo.
Screenshot_20211005-112458_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom