Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais wa Barcelona anasema bado ana imani na Ronald Koeman huku akiweka wazi kuwa Kocha huyo ni Shabiki wa Barcelona hivyo pia anaumia

Neno la mwisho ni kuwa watu waipe timu muda na watakuja na kitu bora
Screenshot_20211003-122151_Instagram.jpg
 
Club ya Azam FC imeonesha basi lake jipya la kisasa aina ya Mercedes Benz watakalokuwa wanatumia kwa safari mbalimbali za Timu yao.
Screenshot_20211003-123145_Instagram.jpg
Screenshot_20211003-123204_Instagram.jpg
Screenshot_20211003-123247_Instagram.jpg
 
Ambundo arejea Yanga
.
Baada ya kupata majeraha ya mkono, kiungo mshambuliaji wa Yanga, Dickson Ambundo, mapema wiki ijayo anatarajia kuanza mazoezi na kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi.
.
Ambundo aliumia mkono wakati timu hiyo ikifanya mazoezi ya kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba uliochezwa Septemba 25, mwaka huu.
.
Ambundo anasema kuwa: "Kwa sasa ninaendelea vizuri, nimeanza mazoezi ya gym, ila nategemea kuanza mazoezi na timu Wiki ijayo."
Screenshot_20211003-123908_Instagram.jpg
 
FEISAL SALUM FANYA YAFUATAYO ILI UWE BORA ZAIDI
:
Imeandaliwa na Gen FUMBWE
:
Feisal SALUM kwasasa ndiyo kiungo mzawa Watanzania tunajivunia kuwa naye kwa uwezo wa kiufundi na kimbinu uwanjani.

Pamoja na yote hayo ila amekuwa akipata tabu pindi akutanapo na viungo wanaotumia ukabaji wa karibu (MAN TIGHT MARKING), wepesi na wenye kasi kwenye kukaba.

Mfano wa viungo hao ni Sadio KANOUTE wa Simba SC. Tafuta mkanda wa video mechi ya SIMBA vs YANGA uone FEISAL alivyopata tabu kipindi cha kwanza wakati KANOUTE akicheza kwenye majukumu ya ulinzi (DEFENSIVE ROLES).

Mfano mwengine ni jana vs GEITA. Mwl. NDAIRAGIJE alipoona Feisal na FARID wametawala katikati, dakika ya 30+ aliamka na kutoa maelekezo kwa viungo wake wafanye "MAN TIGHT MARKING" ambapo Yusuf KAGOMA alifanikiwa kumkaba FEISAL na kusababisha UBUNIFU na MIKOGO yake tuliyoizoea kutoonekana.

Kuna muda FEISAL alipaniki hadi alikataa kupokea mkono wa FAIR PLAY FEISAL baada ya kukutwa na KAGOMA.

USHAURI
Feisal ili awe bora zaidi inampasa ajifunze kucheza na viungo wa aina hii kwa kufanya yafuatayo:

1). Afanye mazoezi ya kuongeza "reaction speed". Hii itamsaidia kufikia mpira haraka hata ikitokea akipigwa "MAN TIGHT MARKING".

2). Aongeze kasi ya "side movements" ili kuwakimbia wapinzani na kutengeneza nafasi kati yao (SPACE CREATION).

3). Afanye upokeaji wa mpira kwa kugeuka haraka na kumuangalia mpinzani wake.

HITIMISHO
Endapo akifanya hayo na kuongeza na aliyonayo, hakika hakuna kiungo mkabaji wala beki atathubu kumkaba FEISAL hata wakimkamia kwa kiwango gani.
:
:
Imeandaliwa na Gen FUMBWE
Screenshot_20211003-124005_Instagram.jpg
 
Manchester City imejipanga vilivyo kuhakikisha inaipiku Chelsea na kuipata saini ya beki wa Villarreal na Hispania, Pau Torres, 24, katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi. Mkataba wa sasa wa beki huyo unamalizika 2024.
.
Pau ni miongoni mwa mabeki tegemeo kwenye kikosi cha Villarreal, ambapo amekuwa akikitumikia kwa muda tangu alipochipukia. Msimu huu amecheza mechi sita za michuano yote.
Screenshot_20211003-124304_Instagram.jpg
 
Nabi kuhusu kutumia washambuliaji wawili Mayele na Makambo:
.
"Natamani kuona wanacheza kwa pamoja (Mayele na Makambo), lakini lazima timu iwe na uwiano wa kuwa na watu watakaoongeza uzito katika ukabaji kabla ya mabeki wa kati. Pia tuwe na watu watakaokuwa bora kusukuma mashambulizi mbele.
.
"Nina washambuliaji bora sana. Makambo, Yusuf na Mayele ni watu wanaojua kufunga lakini lazima nichague kuanza na mmoja. Kama kocha nimechagua kuanza na Mayele. Soka huwezi kucheza na wachezaji wote, lakini haina maana wale wanaoanzia benchi ni wabovu utakuja wakati hata Makambo atakuja kuingia baadaye, soka liko hivyo.
Screenshot_20211003-124403_Instagram.jpg
 
[emoji3578][emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

Nimewatazama Young Africans kwenye game tatu za mwanzo, Ngao dhidi ya Simba na mbili za TPL, specifically Kagera na hii Geita Gold

Ni hivi dakika 90 za mchezo zimegawanyika kila Mwalimu ana focus yake! Wengine 15 za mwanzo na wengine 30 za mwanzo katika kuamua matokeo

Hawa Yanga wamefanikiwa kitu kimoja kutokana na kikosi chao! Napenda kukiita kikosi mseto, kutokana na aina ya wachezaji walionao na Mataifa yao!

Ni sahihi kusema ni Cosmopolitan Squad! Hivyo Mwalimu anatumia ubora wa wachezaji kupata matokeo kirahisi kupitia uwezo wao wa kuusoma mchezo! INSIGHT (UFAHAMU)

Yanga wakianza game wanakupress kwenye kila eneo, wanatumia faida ya presha yenu ili wao wapate matokeo, wanajua ndani ya 30 za mwanzo wanahitaji matokeo

Wamefanikiwa hilo dhidi ya Kagera dakika ya 24, dhidi ya Simba ni dakika ya 11 na leo dhidi ya Geita ni dakika ya 16! Hii ndio plan yao muhimu sana Wananchi, baada ya hapo ni ngumu kusawazisha

Wana Khalid Aucho huyu ndio kama Server! Mkija kwa kasi yeye ndie anapooza mchezo wenu na mtacheza kwa speed ya Yanga, mkipungua kasi wao wanakuja kwa kasi! Wamefanikiwa sana eneo hili

Screenshot_20211003-124754_Instagram.jpg
 
[emoji3578][emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

Nimeitazama mechi ya Simba na Dodoma, ukiachana na Tactical issues hii Simba pia nje ya uwanja wana ushirikiano Mkubwa

Erasto Nyoni wakati Simba inapigwa presha kubwa sana alisimama kutoka kwenye bench na kumuita Kennedy Juma alitumia dakika chache kumuelekeza

Hii ndio Maana ya team work, haijalishi mnacheza ama la ila lazima utoe support kwa ajili ya timu, hapo alikuwa anamueleza kuhusu POSITIONING alikuwa anafatana sana na Wawa

Kutoka kwenye bench tena kuna clip nitaipost ya Meddie Kagere alimuita Hassan Dilunga na kumpa maelekezo kadhaa kwa ajili ya timu

Uzuri wanasikilizana na wanafanyia Kazi Maelezo

Kuna wakati Wachezaji wanaona vitu ambavyo Mwalimu haoni na hii ndio Maana ya UKOMAVU

Ni Mara chache sana huwa naenda viwanjani ila nikifika ni mwendo wa PAYING ATTENTION TO MICROSCOPIC DETAILS
Screenshot_20211003-125150_Instagram.jpg
 
Maelfu ya Watu wameandamana katika Miji kadhaa nchini Marekani kupinga kampeni ya kihafidhina inayolenga kudhibiti au kuzuia huduma za kutoa mimba.

Mjini Washington, takriban Waandamanaji 10,000 walijitokeza karibu na Ikulu ya Rais, kabla ya kuelekea katika majengo ya Mahakama ya juu ambayo itatoa uamuzi wa mwisho kuhusu suala hilo lenye utata, Waandamanaji Wanawake walibeba mabango yenye maneno kama "Halalisha utoaji mimba, mwili wangu, chaguo langu"

Suala hilo limekuwa tete zaidi tangu September Mosi wakati jimbo la Texas lilipopitisha sheria ya kupiga marufuku utoaji mimba, hatua iliyozusha upinzani mkali katika Mahakama mbalimbali na Bungeni.

Siku mbili tu kabla ya Mahakama ya juu kuanza kushughulikia kesi hiyo, kumekuwa na maandamano katika zaidi miji 600, Katika eneo la Mahakama ya juu, Waandamanaji hao walikabiliwa na Waandamanaji wengine wanaounga mkono sheria inayopiga marufuku utoaji mimba na ilibidi Polisi kuingilia kati na kutenganisha makundi hayo mawili.
Screenshot_20211003-133916_Instagram.jpg
Screenshot_20211003-133945_Instagram.jpg
 
Umewahi kusikia Mgonjwa kawafanya Madaktari washangae na wajiulize maswali mengi ya imekuaje? basi huyu Mgonjwa wa Nchini Lithuania atakua miongoni mwa Wagonjwa waliowashangaza Madaktari mwaka huu baada ya kukutwa na kilo moja ya misumari na skruu tumboni mwake.

Imeelezwa kwamba Mgonjwa huyu alikua akilalamika sana kwamba tumbo linamuuma na mpaka akaingizwa kwenye chumba cha Wagonjwa mahututi (ICU) na alipofanyiwa oparesheni ndio akakutwa na hivyo vitu kama inavyoonekana kwenye picha.

Inaelezwa kwamba Mgonjwa huyu ambae kwa sasa anaendelea vizuri Hospitalini amekuwa akimeza misumari hiyo na skruu zikiwemo zenye urefu wa sentimita kumi kwa kipindi cha mwezi mmoja baada ya kuacha kunywa pombe…… swali ni Je alimezaje vyote hivyo?
Screenshot_20211004-043652_Instagram.jpg
 
Tanzania imepata nafasi ya kupeleka Washiriki sita kwenye Fainali za Urembo, Mitindo na Utanashati kwa Viziwi ya ngazi ya Dunia yatakayofanyika Aprili 2022 nchini Brazil kufuatia ushindi wa kishindo wa washiriki wake wawili waliofanya vizuri kwenye Fainali za Afrika zilizomalizika Jijini Dar es Salaam Oktoba Mosi mwaka huu.

Msemaji wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni, na Michezo John Mapepele amesema katika shindano hilo la kwanza kufanyika Afrika na Tanzania kuwa mwenyeji, washiriki wa Tanzania walioshinda ni Khadija Kanyama aliyeshika nafasi ya pili Afrika (Kundi la Miss Deaf Afrika 2021) na Carloyne Mwakasaka (Kundi la Miss Deaf Africa - Fashion) aliyekuwa mshindi wa kwanza.

Mapepele amesema kutokana na ushindi huo Kamati ya Kimataifa ya Mashindano hayo imetoa taarifa ya washiriki wengine wanne kutoka Tanzania ambao sasa nao wamekidhi vigezo vya kushiriki mashindano hayo kwa ngazi ya dunia kuwa ni Surath Mwanis, Rajani Ali na Russo Songoro upande wa Mavazi na Mitindo huku Joyce Denis akipata nafasi ya kushiriki katika eneo la urembo.

Jumla ya Washiriki 8 wa Tanzania waliungana na washiriki wengine zaidi ya 30 kutoka nchi nyingine 12 za Afrika.
Screenshot_20211004-044346_Instagram.jpg
Screenshot_20211004-044404_Instagram.jpg
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kwenye kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2021/2022 imekusanya Tsh. Trilioni 5.15 sawa na ufanisi wa 94.3% ya lengo la kukusanya Tsh. Trilioni 5.46, imesema makusanyo hayo yamekua kwa 17.4% kutokana na mambo mbalimbali ambapo jambo la kwanza walilolitaja ni Watu kulipa kodi kwa hiari hususani kwenye shughuli za uchimbaji madini, mawasiliano na uchukuzi.
Screenshot_20211004-044508_Instagram.jpg
 
Wakati kanuni za kitabibu zikielekeza majibu ya ugonjwa wa homa ya matumbo (typhoid) yatolewe ndani ya saa 24 baada ya kupitia hatua mbili za upimaji, uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa vituo vingi vya upimaji hutoa majibu hayo kati ya dakika 30 hadi saa moja.

Kutokana na sintofahamu hiyo ya vipimo vya typhoid, baadhi ya taasisi zinazojihusisha na utoaji wa bima ya afya, ukiwemo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) zimekataa kutambua na kulipia vipimo vinavyotolewa kwa muda mfupi.

Baadhi ya maabara hupima na kutoa majibu ya ugonjwa huo kwa wagonjwa kuwa au kutokuwa na vidudu vya typhoid katika hatua ya awali ya upimaji bila kwenda kwenye hatua ya pili.

Kwa mujibu wa mtaalamu wa afya ya binadamu, Dk Patrick Ntakisigaye, ili kuthibitisha uwepo na kiwango cha wadudu wa ugonjwa wa typhoid, sampuli inatakiwa kupitia hatua mbili, moja ikiwa ya awali ya kuangalia matokeo baada ya kuweka vitendanishi kwenye sampuli ya mgonjwa.

“Kukiwa kuna antibody reaction (mwitikio wa kingamwili), sampuli husika hufanyiwa incubation ambayo majibu yake yanatoka baada ya saa 18. Hapo ndipo mtaalamu atajua iwapo mwitikio ulioonekana kwenye hatua ya awali umetokana na uwepo wa wadudu au la,” alisema Dk Ntakisigaye.
Screenshot_20211004-044629_Instagram.jpg
 
Ni kesi yenye msisimko mkubwa Afrika Kusini. Inamhusu Nomia Rosemary Ndlovu, ambaye ni askari polisi wa zamani nchini humo. Tuhuma dhidi yake ni kuua watu sita. Wote ni ndugu zake.

Mwendesha mashitaka wa kesi hiyo, Riana Williams, ameshasoma mashitaka yote na kumtuhumu Rosemary kuwa aliwapa kazi wauaji, Lakhiwe Mkhize na Njabulo Kunene, kwa ajili ya kutekeleza kazi hiyo.
Ndugu waliouwa ni wafuatao; wa kwanza ni Witness Madala Homu.

Huyu ni binadamu wa Rosemary. Aliuawa mwaka 2012. Halafu, mwaka 2013, ikawa zamu ya dada wa Rosemary, Audrey Samisa Ndlovu.
Mwaka 2015, aliyekuwa mpenzi wa Rosemary, Maurice Mabasa aliuawa.

Maurice na Rosemary walifanikiwa kupata mtoto mmoja. Mwaka 2016, 2017 na 2018, Rosemary kwa kuwatumia Mkhize na Kunene, aliwaua watoto wawili wa ndugu zake, Zanele Motha, Mayeni Mashaba na Brilliant Mashego.
Screenshot_20211004-044731_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom