Makapuku Forum

Makapuku Forum

1630647724074.png
 
CECAFA Samia Women Cup 2021
.
FAD FC SIMBA Q
7:00 mchana.
Kasarani stadium.
.
MSIMAMO KUNDI A
1. Lady Doves - 4pts
2. Simba Queens - 4pts
3. PVP FC - 3pts
4. FAD FC - 0
.
Ushindi TU ndio unaitajika hii leo kutoka katika kikosi cha Simba Queens. Kila la Kheri Malikia wetu
Screenshot_20210903-091529_Instagram.jpg
 
CAF YAUKATAA CCM KIRUMBA, BIASHARA KUKIPIGA KWA MKAPA
.
Biashara United haitaweza tena kucheza mechi zao za Kombe la Shirikisho Afrika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza kama ilivyokuwa mipango yao baada ya CAF kuukata uwanja huo na sasa wawakilishi hao watakipiga jijini Dar es Salaam.
.
Tayari timu hiyo ilishaweka kambi jijini Mwanza kwa wiki mbili, lakini juzi wameambiwa mechi yao ya awali dhidi ya FC Dikhil ya Djibouti itapigwa Benjamin Mkapa, kwa vile Kirumba imeshindwa kukidhi vigezo vilivyotakiwa.
.
Meneja na mratibu wa Biashara amesema wamelazimika kubadili kila kitu kwani walikuwa Kirumba kwa zaidi ya siku 10 na wachezaji walikuwa wamezoea mazingira hayo hivyo wapo kwenye hatua za mwisho za kuhamishia kambi Dar ili kuanza upya maandalizi.
Screenshot_20210903-091706_Instagram.jpg
 
Wakazi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wamelilalamikia Shirika la umeme Tanzania TANESCO Mkoani humo kutokana katakata ya umeme kwa zaidi ya wiki mbili sasa bila kutoa taarifa kwa Wananchi.

Akiongelea malalamiko hayo Meneja wa TANESCO Kigoma Mukhsin Kijemkuu amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kwa sasa shirika linahudumia Wateja wengi mara 5 zaidi ya Wateja waliokuwepo kulikotokana na kushuka kwa gharama za umeme kutoka 300,000 mpaka efu 27,000.

Amesema Manispaa ya Kigoma Ujiji ina jumla ya mashie 5 zinazozalisha umeme wa kiasi cha 6.25 MW huku kiwango cha matumizi kwa Mkoa mzima kikiwa 8.9KW kiasi ambacho hakiwezi kukidhi haja kwani umeme wa Manispaa ya Kigoma ujiji unahudumia pia Wilaya ya Uvinza na maeneo ya wilaya ya Buhigwe.

Mukhsin amewashauri Wananchi waweke protection devices kama socket braker kwaajili ya kuweka usalama wa nyumba na mali zao na kuahidi kulitafutia suluhu tatizo hili ndani ya muda mfupi.
Screenshot_20210903-093447_Instagram.jpg
 
: • Ripoti za wiki hii Nchini Afghanistan zinasema Uchumi unazidi kuzorota baada ya Taliban kuchukua udhibiti wa taifa hilo ambapo sasa hivi Watu wanazuiwa kuchukua fedha nyingi kwenye akaunti zao.

Kiwango pekee Mtu anachoruhusiwa kukitoa Benki ni $200 kwa wiki sawa na pesa za Tanzania laki nne na elfu sitini na tatu.
Screenshot_20210903-093619_Instagram.jpg
 
“Mwaka huu tunakwenda na slogan ambayo inasema ‘Simba Day 2021 One Team One Dream’ lakini tunamaliza kwa kiswahili kwa kusema ‘Asubuhi tu twendeni wenye Nchi’ na One Team One Dream maana yake ni kwamba Mashabiki wa Simba tuko pamoja, tuna ndoto moja, timu yetu ni moja na sote tunajua wapi ambako tunataka kwenda” ———-Ezekiel Kamwaga, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano
Screenshot_20210903-103510_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom