Makapuku Forum

Makapuku Forum

Bondia ambaye nitapigananae Ijumaa September 3, 2021 [Julius Indongo] amesha pigana kwenye ring kubwa ambazo mimi pia nina ndoto nazo. Amecheza na watu wakubwa ambao natamani siku moja nichezenao.

Kwa hiyo sio mechi rahisi kwangu lakini sio rahisi kwake pia kwa sababu mimi sio rahisi kama ambavyo anafikiria.
Screenshot_20210901-180227_Instagram.jpg
 
Kwa udhati wa Moyo wangu naomba niwashukuru Kuanzia Uongozi wote wa Yanga chini ya mwenyekiti wetu Dk. Mshindo Mbette Msolla na Kaimu Katibu Mkuu Mpya Senzo Mbatha Mazingiza, wafanyakazi wenzangu wote kwa upendo wenu kwa kipindi chote cha miaka miwili niliyoitumikia Yanga kwa moyo Mkunjufu na kujitoa kwangu, Mungu awabarik, awalinde na awape kila hitajio la nafsi zenu ili tuweze kuipeleka mbele Brand ya Yanga.

Wanachama,wapenzi na mashabiki wa Yanga ninyi mumekuwa na mimi kwa moyo mmoja Ahsanteni sana Nawapenda sana na niatendelea kuwa nanyi.

Tutaonana tena hivi Karibuni. Insha Allah.

.
Screenshot_20210901-181551_Instagram.jpg
 


MIKONO YA KIHAMU YA FARHAN JR

Wakati Cesc Fabregas anahitajika na Arsenal alikuwa na umri wa miaka 16 tu! Alikuwa kijana mdogo sana sana

Mama yake mzazi anaitwa Nuria Fabregas, alisema wazi kuwa hakuweza kukubali mtoto aondoke kirahisi, lakini akasema alikuwa anajua ni Mtoto lakini ni Mwanaume pia

Baada ya Fabregas kutua Jijini London, Kwenye baridi kali sana na maisha tofauti na mitaa ya kwao huko Arenys der Mar, Catalunya

Klabu ya Arsenal kupitia Profesa Arsene Wenger, walifahamu vyema kuwa Kijana wao bado mdogo sana! Wakaajiri Mama wa Kiingereza awe anamlea kama Mwanae, klabu ilikuwa inalipa mishahara yake

Kama hivyo haitoshi, klabu ya Arsenal ilimpa kazi ya ziada Gwiji ambaye ni Marehemu sasa, Jose Antonio Reyes awe Kaka yake wa hiyari na amfanye ajisikie nyumbani, nae alikubali! Mwisho ikawa historia

Nimesema hayo yote kwakuwa nataka kusema jambo kuhusu kijana PETER BANDA, usajili mpya wa klabu ya SIMBA ana umri wa miaka 20 tu, amezaliwa September 22, 2000

Niliwahi kufanya tafiti yangu nyepesi nikagundua Banda alikuwa na wakati mgumu wakati mwingine huko Moldova kutokana na umri wake na mazingira, ili Mtoto ajisikie nyumbani kuna namna klabu ya Simba ikubali gharama

Kitu cha kwanza! Ule usajili wa DUNCAN NYONI kutoka Malawi licha ya ubora wake mkubwa sana ila nyuma ya pazi pia Simba walimsajili kwa ajili ya Kijana Peter Banda, wote Wamalawi na wote wajisikie nyumbani

Anachofanya Simba ndicho alichowahi kufanya Arsenal juu ya Fabregas ili Mtoto awe anajisikia nyumbani, hii ndio maana halisi ya uwekezaji na projects za wachezaji kwenye mpira wa miguu

Mwisho, Peter Banda ni Kijana mwenye imaan ya Kilokole! Wakati naandika hii ni kuwa klabu ya Simba imepambana kumsaka Mama wa Kilokole kwa ajili ya kumlea Kijana na Familia yake, Klabu pia inalipia gharama hizo! Hii pia Arsenal waliwahi kufanya hivyo

Hivyo ndivyo klabu kubwa duniani zinalinda projects za wachezaji wa muda mrefu, wachezaji wenye potential kubwa! Unaingia gharama kwa mafanikio ya muda mrefu
Screenshot_20210901-181756_Instagram.jpg
 
MORRISON AMFUNZA MANARA HEKIMA
.
"Niliondoka Yanga wakati tuna mgogoro na bado hadi sasa tunamvutano, lakini sijawahi kusema chochote kibaya dhidi ya klabu au Injinia Hersi Saidi au antonio Nugaz wala mashabiki, unajua ni kwanini ?? Kwasababu wale wamenilisha, walinipenda na walinitendea mazuri mengi hivyo siwezi kuwavunjia Heshima eti kisa nina mgogoro nao. Hii ni akili ya kawaida sana kaka.
.
"Kamwe using'ate mikono inayokulisha au iliyokulisha kabla Kuna msemo: "busara ni kawaida lakini sio kwa watu wa kawaida". Ni ushauri wangu tu kwa kaka mkubwa. Ukweli huumiza lakini hakuna chuki binafsi . HEKIMA NA ITAWALE.

- Bernard Morrison

Screenshot_20210901-182633_Instagram.jpg
 
Watatu Yanga waachwa Taifa Stars
.
Kocha wa Taifa Stars amewaacha mastaa watatu wa Yanga, Bakari Mwamnyeto, Ramadhani Kabwili na Zawadi Mauya kwa sababu za kiufundi.
.
Mwamnyeto mbadala wake ni Lusajo Mwaikenda ambaye ameongezwa kikosini na ameonyesha kiwango kizuri akiwa na kikosi chini ya miaka 23.
.
Kabwili ambaye ameitwa baada ya kukosekana kwa muda mrefu eneo lake halina shida kutokana na uwepo wa Aishi Manula na Metacha Mnata na Willbol Maseke.

................
Screenshot_20210901-182801_Instagram.jpg
 
Bocco aachwa Taifa Stars
.
Kikosi cha Taifa Stars kimeondoka nchini jana jioni kwenda DR Congo kwa ajili ya mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia Qatar 2022, utakaopigwa Septemba 2 Lubumbashi,Congo.
.
Stars iliondoka na wachezaji 23 huku ikimuacha nyota wake John Bocco ambaye ameachwa kutokana na kuwa majeruhi.Kukosekana kwa Bocco nafasi yake inachukuliwa na Simon Msuva na Mbwana Samatta ambao watacheza pamoja eneo la ushambuliaji.

.................
Screenshot_20210901-183019_Instagram.jpg
 
VINI JR BAHATI YAKE, AMEITWA BRAZIL

Nyota wa Real Madrid, Vinicius Junior ambaye hakuwa sehemu ya kikosi cha kwanza kilichoitwa cha timu ya taifa ya Brazil kwa ajili ya michezo ya kuwania nafasi ya kufuzu Kombe la Dunia amejikuta akikumbana na bahati ya mtende.

Kanuni za baadhi ya mataifa kuhusiana janga la virusi vya corona zimemfanya kocha wa timu ya taifa hilo, Adenor Leonardo Bacch maarufu Tite kupangua kikosi chake na kuwaita mastaa wengine tisa wapya akiwemo kinda huyo.

Mbali na Vinicius Jr walioangukiwa na bahati hiyo wengine ni makipa wawili Everson na Santos, mwingine ni beki Miranda ilhali viungo ni Edenilson, Gerson na Matheus Nunes huku washambuliaji ni Hulk na Malcom.
Screenshot_20210901-183401_Instagram.jpg
 
DEAL.DONE | Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta amejiunga na klabu ya Royal Antwerp ya Ubelgiji akitokea Fenerbahce ya Uturuki.
.
Imeripotiwa kuwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Tanzania uhamisho wake umeigharimu Antwerp kitita cha Euro milion 4 ambazo ni zaidi ya Sh. 10.9 Bilioni.
Screenshot_20210901-183559_Instagram.jpg
 
Spika wa Bunge Job Ndugai ameomba radhi Wakristo na Watanzania wote kwa ujumla waliokwazika na kauli yake aliyoitoa jana Bungeni akieleza mstari wa Biblia na kumtaja Yesu badala ya Yusufu.

“Nawaomba radhi sana, naomba radhi sana, naomba radhi sana na huu ndio mfano tulikuwa tunasema, ukikosea unasahihisha, ukisahihisha hakuna tatizo, haikufanyi uwe mnyonge wala haikuoneshi wewe ni mjinga na mimi nilikosea nimesahihisha” ——— Spika Ndugai.
Screenshot_20210901-185802_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom