Makapuku Forum

Makapuku Forum

“Kulikuwa na maelekezo ya Rais kwamba kodi ya miamala itazamwe upya, kodi ile iliwekwa kwa mujibu wa sheria ya Bunge kwahiyo kuna namna ya kiuangalifu Sana inatakiwa ifanyike bila kuvunja sheria, tayari Kamati iliyoundwa ikiongozwa na Waziri Nchemba na Ndugulile ilifanya kazi ikawasilisha taarifa yake ya kwanza kwa Waziri Mkuu”

“Waziri Mkuu akaagiza marekebisho zaidi yakafanyike, marekebisho yamefanyika na taarifa hii itatolewa August 31, 2021 kwahiyo mwisho wa mwezi huu itatolewa taarifa ya nini sasa Serikali imeamua kuhusiana na namna ambavyo tutakwenda na tozo hii” ——— Gerson Msigwa, Msemaji Mkuu wa Serikali.
Screenshot_20210829-042654_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Miaka ya 1970 nchini England kupitia FA yao waliwahi kupiga marufuku matangazo kwenye jezi za wachezaji (Kit Sponsors) lakini baada yakabatilishwa

Yote hayo ni mabadiliko ya biashara ya mpira na sasa MERCHANDISING ni sehemu kubwa zaidi!

Kwenye wadhamini wa jezi (KIT SPONSORS) kuna Main Sponsor huyu ni Mdhamini Mkuu anaetoa pesa ndefu kuliko wote kisha kuna CO-SPONSORS ambao ni Minor wanaotoa pesa ndogo

Hakuna kanuni ya kudhibiti idadi ya Wadhamini kwenye jezi bali kuna vigezo na Masherti ya udhamini kulingana na Sheria za nchi au FA haswa kwenye mgongano wa kimaslahi

Kwanini watu wanasema jezi ya Simba ina Wadhamini wengi?

Kabla sijajibu nadhani tukaitazame jezi ya Santos ya Brazil, Al Ahly ya Misri na kidogo Fiorentina ya Italia yenye wadhamini watano, sahau kidogo kuhusu timu za Sudan maana zipo mbali kimpira ni dhambi kuwatumia kama mfano, mifano nimekupa ya nchi za kimpira

Well Simba kwenye jezi yake ana SPORTPESA, MO EXTRA, MO PROTECTOR SABUNI, MO SIMBA FOUNDATION jumlisha na free of charge Ad ya VISIT TANZANIA! Hapo matangazo ya pesa yapo matatu tu

Sportpesa anaweka pesa inayokadiriwa juu ya Million 900, MO EXTRA na MO SABUNI ni million 400 kwa Mwaka, hiyo MO SIMBA FOUNDATION ni Asasi ya Kijamii ni ya Simba haiwezi kutoa pesa kwakuwa ni msaada kwa Jamii

Tuje kwenye VISIT TANZANIA, Kutokana na CAF kuwa na Kampuni nyingine ya ubashiri, haikuwezekana Simba kwenda na Sportpesa kama Main Sponsor, hapa kwa heshma ya kimkataba klabu ikaona itangaze nchi yake

MO angekuwa mbinafsi ile nafasi pale kifuani si ingekaa Bidhaa yake? Wangekuwa wabinafsi kwenye idara ya Masoko ya CAF si wangepeleka matangazo yao binafsi? Hapa tukubaliane wameheshimu mkataba, hakuna kitu cha bure pale

Labda watu waseme kuhusu FONT SIZE inayotumika ni kubwa kwenye matangazo, again sio mbaya pia kuinadi biashara ya anaeweka pesa yake plus VISIBILITY

Screenshot_20210829-044136_Instagram.jpg
Screenshot_20210829-044155_Instagram.jpg
 
TRANSFER UPDATE | Paris St-Germain inafuatilia kimya kimya uwezekano wa kuipata saini za wachezaji kibao barani Ulaya ikiwa pamoja na kiungo wa Manchester United na Ufaransa, Paul Pogba, 28, sambamba na straika wa Borussia Dortmund na Norway, Erling Braut Haaland, 21, katika dirisha hili ama lijalo.
Screenshot_20210829-051500_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom