Makapuku Forum

Makapuku Forum

Watu zaidi ya 20 wakiwemo Watumishi watatu wa Wizara ya Ardhi wamenusurika kifo baada ya kushambuliwa na Wafanyakazi wa Wavamizi wa shamba la aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu Marehemu Daudi Balali ambapo shambulio hili lilitokea wakati wakiendelea na zoezi la upimaji wa shamba hilo ambalo kwa sasa linamilikiwa na Familia ya Balali katika Kijiji cha Melela, Halmashauri ya Mlimba Wilaya ya Kilombero.

Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Morogoro Frank Minzikuntwe amesema vurugu hizo zimetokea baada ya maamuzi ya Serikali ya kulipima eneo hilo ili liweze kupangwa upya baada ya kutelekezwa kwa muda mrefu huku Wananchi wanaolizunguka wakikosa maeneo ya kilimo.

Kamishna huyo amesema hali za Watumishi pamoja na Wananchi wengine zinaendelea vizuri baada ya kufikishwa katika vituo vya kutolea huduma za afya katika halmashauri hiyo.

“Dereva aliokolewa na Bodaboda wa pale Kijijini huku nyuma wale Watu (Wafanyakazi wa Wavamizi) wakachoma gari, pikipiki tatu, vifaa vya upimaji, laptop tatu zilizokuwa kwenye gari na mali nyingine, Wataalamu kwa kushirikiana na Wajumbe na Mgambo walikimbia kutoka eneo la shamba na kujiokoa.
Screenshot_20210808-183532_GBInsta.jpg
 
Saudi Arabia itaanza kuwapokea Wageni waliopata chanjo ya Covid-19 katika mji mtakatifu wa Kiislamu wa Mecca ikiwa kama sehemu ya Ibada ya hija ya umrah ikiwa ni takribani miezi 18 baada ya mipaka yake kufungwa kutokana na kirusi corona.

Shirika la habari la Saudi limesema Wizara ya Hijja na Umrah imetangaza kuanza kupokea Raia wa taifa hilo wenye nia ya kutaka kushiriki ibada ya Umrah lakini pia kwa awamu watapokea maombi kutoka mataifa mbalimbali.

Taarifa hiyo imeongeza kusema Mamlaka zitaanza kukubali maombi ya kusafiri kuanzia kesho Jumatatu ambapo hatua hiyo itafanya uwezo wa kupokea Wageni katika mji ya Mecca na Madia kuongezeka na kufikia watu milioni 2 kutoka 60,000 ya sasa.

Ibada ya Umrah ambayo kwa kawaida inafanyika katika kipindi chochote cha mwaka, ilifunguliwa tena Oktoba kwa Mahujaji wa ndani baada ya kufungwa kabisa kutokana na mlipuko corona.
Screenshot_20210808-184430_GBInsta.jpg
 
"Japo Corona imeathiri uchumi wetu Serikali haijachukua hatua yoyote kuwalinda Watu na sekta zilizoathirika, naisihi Serikali kuwasilisha Bungeni mpango maalumu wa kunusuru sekta ambazo zimeumizwa na corona hususani sekta ya utalii”

“Corona pia imeathiri biashara na ajira, 35% ya Makampuni yamefungwa kati ya January 2020 na January 2021 na 17% ya Wafanyakazi katika sekta ya Utalii wamepoteza kazi zao hali iliyopelekea biashara ya utalii kuanguka kabisa”

“Ninafarijika kwamba baada ya Rais mpya kuingia madarakani kumekuwa na mwelekeo mpya wa kisera wa namna ya kukabiliana na janga hili la Covid-19 nchini”

“Takwimu zimeanza kutoka japo sio kwa ukamilifu na baadhi ya hatua za kujikinga zimeanza kuchukuliwa, ingawa bado hatua hizo haziridhishi lakini si haba, napenda kuipongeza Serikali kwa maamuzi hayo muhimu” ———Zitto Kabwe akiongea na Waandishi wa Habari leo Zanzibar.
Screenshot_20210808-185122_GBInsta.jpg
 
“Napongeza maamuzi sahihi ya Serikali ya kuruhusu chanjo ziingizwe nchini ili kuwapa kinga Watanzania na kuulinda mfumo wetu wa afya dhidi ya wagonjwa wengi ambao bila kinga hautaweza kuhimili”

“Hata hivyo, bado kuna kazi kubwa zaidi ya kufanya kwenye uhamasishaji wa watu kujitokeza kupata chanjo, nitoe rai kwa kila mmoja wenu, nikianza na Wanachama wa ACT Wazalendo kufuata taratibu na kupata chanjo
mapema iwezekanavyo”

“Napenda kuwahakikishia kuwa nimejiridhisha kuwa chanjo zilizoruhusiwa kuingia nchini ni salama na mimi pia nimekwisha chanjwa na niko salama salimini”

"Ninapenda kuwaasa kuwa kuchanjwa ni swala la hiari lakini tunapoangalia usalama wa wapendwa wetu, jamii yetu na Watanzania wenzetu basi hatuna budi kuhakikisha tunafanya maamuzi sahihi” ——— Kiongozi wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe
Screenshot_20210808-185258_GBInsta.jpg
 
“Lazima kuwa na mkakati maalum wa uhamasishaji utakaongozwa na Watu wanaoaminika kwenye jamii na si Watu walewale ambao walituambia kuwa Tanzania imeishinda Corona ama walewale ambao walituaminisha malimao na tangawizi ni tiba ya Corona”

“Hatuwezi kuwa na utekelezaji bora wa sera mpya za kupambana na Corona iwapo tutaendelea kuwa na sura zilezile zilizotuaminisha kutumia njia zisizoshauriwa kisayansi”

"Ni muhimu sana kwa Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari zote ikiwemo kuepuka mikusanyiko, kuvaa barakoa, kunawa kwa maji tiririka na sabuni kila wakati pamoja na kutumia vitakasa mikono ili kujikinga na kuzuia kusambaa kwa maambukizi”

“Kwa Serikali zote mbili, hatua madhubuti zichukuliwe kuongeza elimu kwa Wananchi kwani kwa mwaka mzima walikuwa wanaambiwa hakuna corona, hivyo kuwaambia kuwa sasa ipo sio jambo rahisi kueleweka, jitihada zifanyike kwenye kutoa elimu sahihi kwa Umma”——— Zitto Kabwe
Screenshot_20210808-185432_GBInsta.jpg
 
“Baada ya kupata Rais mpya wengi wetu tuliona ipo haja ya kurejesha mazungumzo ya Kitaifa pamoja mchakato wa Katiba mpya ili tuutumie kujadiliana kama Taifa juu ya athari za miaka mitano na nusu iliyopita”

“Pia tuliona ipo haja ya kutafuta muafaka wa Kitaifa juu ya namna njema ya kuendelea kutoka hapa tulipo, lengo hasa likiwa ni kurejesha umoja wa Kitaifa ambao ulimomonyoka”

“Serikali mpya imefanya mambo kadhaa tangu iingie madarakani ambayo ni kinyume na yale mabaya yaliyomomonyoa umoja wa kitaifa ya miaka mitano na nusu iliyopita ikiwemo kuruhusu uhuru wa habari, kuondoa ukusanyaji wa kodi kwa kutumia mabavu na vikosi kazi”

“Serikali mpya pia imezifuta kesi kadhaa walizobambikiwa Watu pamoja na kuwaachia huru Wahusika n.k….. hatua hizi si haba lakini kwa uharibifu uliofanyika hazitoshi”

“Jambo kubwa ambalo Serikali mpya ya JMT haijalifanyia vizuri kazi ni uhuru wa kisiasa, bado Sheria ya Vyama vya Siasa ni ileile ya mwaka 2019 bado Sheria za uchaguzi ni zilezile zilizotumika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020”——— Zitto Kabwe
Screenshot_20210808-185550_GBInsta.jpg
 
“Sisi Viongozi, Wanachama na Wafuasi wa Vyama vya Upinzani tuliishi kwa mateso sana ndani ya miaka mitano na nusu iliyopita, tukifilisiwa mali na kufungiwa akaunti zetu……. Ndugu Freeman Mbowe akiwa ni kielelezo cha hili”

“Tulipigwa risasi zaidi ya 30 na mpaka leo hakuna hata uchunguzi dhidi ya vitendo hivyo vya kinyama, Ndugu Tundu Lissu ni kielelezo cha hili, tulibambikiwa kesi na kuhukumiwa Mahakamani (Mimi na mamia ya Viongozi wenzangu wa kisiasa ni kielelezo cha hili)”

“Mamia ya Wanachama wetu wakipata vilema vya kudumu kwa vipigo (humu kwenye Kamati Kuu tunao kina Jussa na Mazrui), unaweza kusema bila kupepesa maneno kuwa Wapinzani walitendewa ugaidi mkubwa mno na vyombo vya Dola”

“Kesi ya Ugaidi dhidi ya Mbowe ni jambo linalokumbusha machungu makubwa sana ya awamu iliyopita, Watu waliofungua mashtaka hayo hawamkomoi Mbowe wala hawatuvunji moyo wa kupambania Tanzania yenye usawa wa kisiasa na kuheshimu utofauti wetu wa mawazo, wanalichelewesha tu Taifa letu kupata Umoja na Maendeleo ya Kiuchumi, wanataka turudi kulekule ambapo hatupaswi kurudi”

“Wito wangu na Viongozi wenzangu kwa ndugu Rais Samia ni kuingilia kati na kumaliza jambo hili la kisiasa kwa njia za kisiasa, Rais asikubali jambo hili, awazuie Wasaidizi wake wanaotaka tuendelee kuishi kama ilivyokuwa ndani ya miaka mitano na nusu iliyopita, tunajua anao uwezo huo, tunajua akitaka anaweza kulizuia jambo hili, tunajua yeye hataki tuendelee kuishi kigaidi” ——— asema Zitto Kabwe leo akiwa Zanzibar.
Screenshot_20210808-185657_GBInsta.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma leo August 08, 2021 wakati akitokea Jijini Dar es Salaam katika shughuli za kitaifa.
Screenshot_20210808-185822_GBInsta.jpg
Screenshot_20210808-185841_GBInsta.jpg
Screenshot_20210808-185855_GBInsta.jpg
 
Wizara ya Afya imesema itatoa kadi za kielektroniki kwa watu wote waliopata chanjo ya #COVID19, ambazo zitakuwa na taarifa zote za mhusika (chanjo aliyopata, kituo, muda). Kwa utaratibu huo, wizara imesema itawabaini watakaojipatia vyeti kwa njia ya udanganyifu, na imewaonya.
Screenshot_20210808-190155_GBInsta.jpg
 
Lionel Messi abubujikwa na machozi mbele ya familia yake, wakufunzi na wachezaji wa Barcelona wakati akiaga familia yeke ya camp Nou aliyojiunga nayo rasmi tangu mwaka 2003.

Kulia kwa Messi kulifanya wengi wa marafiki na wachezaji wenzie kudondosha chozi kwa sababu mchezaji aliyekaa Barcelona kwa miaka mingi zaidi.

“Nimejaribu kuishi kwa uvumilivu na heshima kubwa na naamini hiyo ndio kumbukumbu mtabaki nayo”.

Hata hivyo Alithibitisha kuwa ni timu nyingi zimeweka dau kuwa zinamuhitaji ila bado hajafanya maamuzi.
Screenshot_20210808-190349_GBInsta.jpg
Screenshot_20210808-190404_GBInsta.jpg
Screenshot_20210808-190419_GBInsta.jpg
 
Spurs waingilia dili la Arsenal
.
Tottenham wamekubali kutoa dau la uhamisho wa staa wa Inter Milan Lautaro Martínez mwenye thamani ya zaidi ya pauni milioni 60, wakiipiku Arsenal
.
Fowadi huyo wa Inter Milan anatarajiea kucheza pamoja na Harry Kane, ambaye Spurs wamesisitiza kuwa HATAUZWA
.
Screenshot_20210808-190827_GBInsta.jpg
 
"Habari za kwamba niliomba pesa zaidi ni uongo, Hatua hii ni ngumu sana kwangu na bado ni ngumu hadi sasa. Hata bado nikirudi nyumbani hali yangu itabaki kuwa mbaya. Sijiskii vizuri kabisa kwa hiki kinachoendelea" - Leo Messi.
Screenshot_20210808-190952_GBInsta.jpg
 
Baada ya maongezi kati ya PSG na upande wa Lionel Messi yaliyoanza tangu Alhamisi iliyopita, rasmi leo wameupokea mkataba kutoka Paris

Kilichosalia ni Messi na watu wake wake kuupitia kisha kupaa mpaka Paris kwa ajili ya vipimo vya afya kisha kutambulishwa rasmi kwenye mnara wa Eiffel

Atasaini miaka miwili na nyongeza ya mwaka mmoja mpaka June 2024
Screenshot_20210808-191633_GBInsta.jpg
 
UTATA KUHUSU MESSI

Kuna mengi tangu juzi yanaongelewa kutoka kwa waandishi nguli nchini Hispania, wameibua maswali mengi juu ya mkataba wa Messi na Barcelona

Swali la kwanza, ikiwa LA LIGA wanatoa kiwango cha juu cha mshahara kwa kila klabu pale tu dirisha limefunguliwa, yawezekana vipi Barca wasijue?

Swali la pili, inawezekana vipi Messi yupo Ibiza anakula bata akijua anarudi Barca, siku anafika baada ya kukubali mpaka kupunguza mshahara, ndio siku hiyo Viongozi wanagundua mkataba hauwezekani?

Je? Haikuwa tu agenda ya Joan Laporta kumtumia Messi ili arejee kwenye kiti cha uongozi? Maana alisema wakimchagua basi Messi atasalia Barcelona

Ni wazi Lionel Messi kaamua kukaa kimya kwa maslahi ya klabu, ni wazi kuwa Barcelona walitaka kuanza project mpya bila Messi
Screenshot_20210808-191801_GBInsta.jpg
 
MESSI ANAZUNGUMZA| NOU CAMP, BARCELONA

"Nilitamani kubaki hapa, hapa ni nyumbani na hapa ni nyumbani kwetu sote, mpango ulikuwa ni kubaki ila leo napaswa kusema KWAHERI, kusema neno hilo ni gumu kwakuwa hii ndio klabu niliyocheza kwa maisha yangu yote"

Lionel Messi, anazungumza
Screenshot_20210808-192026_GBInsta.jpg
 
MESSI ANAZUNGUMZA| CAMP NOU, BARCELONA

"Sina neno zaidi, asanteni na kwaherini nyote, Barcelona ilifanya ndoto yangu itimie"

____

Mnaona namna Messi anazungumza?? Licha ya rekodi zote na historia zote lakini amesema "ASANTENI BARCA MMEFANYA NDOTO YANGU ITIMIE"
Screenshot_20210808-192026_GBInsta.jpg
 
MESSI ANAZUNGUMZA| CAMP NOU, BARCELONA

Wakati Lionel Messi anazungumza alisimama kwa dakika moja na sekunde kadhaa, akishindwa kutoa maneno huku akilia.

Wachezaji wenzake wote wakasimama, wakawa wanampigia makofi na kumpa moyo Nahodha wao amalize maneno, amalize neno kwa ajili ya klabu aliyoipigania.
Screenshot_20210808-192251_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom