Kisa ndoa, Makambo huyo arejea Congo
.
Siku chache baada ya kusaini mkataba ya kazi ndani ya Yanga, staa mpya wa DR Congo, Heritier Makambo jana usiku aliondoka nchini kurudi kwao kujiweka sawa tayari kwa kazi.
.
Makambo alitua nchini hivi karibuni bila begi lolote ili kuja kukamilisha dili lake, lakini jana viongozi wa Yanga walieleza anakwenda kuoa fasta na Kocha Nabi Mohammed amempa siku tano tu awe amerejea Dar tayari kwa mazoezi ya msimu mpya.
.
Awali inadaiwa kwamba mchezaji huyo aliomba kupewa wiki mbili za mapumziko lakini Nabi akamkatalia na kumsisitiza kwamba anawataka arudi haraka na wakakubaliana kila kitu akasepa zake.
.
View attachment 1880464