“Niwaambieni bila kupepesa macho kazi ya Urais ni ngumu lakini kwasababu Urais ni Taasisi yenye vyombo kadhaa vinavyosaidia ndipo urahisi wake ulipo, Rais hafanyi kazi pekee yake”
“Nikisikia Watu kwa kundi kubwa mnasimama mnasema Mama kafanya mazuri, inanipa moyo ndio maana tunazungumza na makundi, Watanzania ni Watu wa moyo ukiwafanyia kidogo wanashukuru, maombi kila pembe Misikitini na Makanisani, shukrani inanipa moyo”
“Tuchukue tahadhari dhidi ya Corona ukihisi nyungu inakusaidia fanya, ukihisi dawa gani sijui yakusaidia tumia, ila sisi tunasisitiza zile ambazo Wataalamu wanatuambia kunawa mikono kwa maji tiririka, kutumia barakoa n.k”
“Tiba asili zimetibu generation to generation na ndio maana Serikali imeweka Bodi, Wataalamu wakae watazame zile wanazoona zinakidhi vigezo zitumike, kuna wakati tunabeza lakini zinasaidia, hatuwezi kubeza moja kwa moja, Wanasayansi tu watusaidie”
“Kuhusu kuihamishia Idara ya Habari kwenye Wizara ya Teknolojia ya Habari tutakaa tuangalie kwa pamoja tukijiridhisha vya kutosha tunaweza kuangalia vinginevyo”———Rais Samia akizungumza na Wahariri Dar es salaam leo.