Makapuku Forum

Meya wa Manispaa ya Temeke Abdalla Mtinika amemtangaza Mchekeshaji wa Kenya Eric Omondi kuwa Balozi wa kuitangaza Temeke Mkoani Dar es salaam, haya yanajiri kuelekea Tamasha la Comedy ambalo limeandaliwa na Omondi kwenye Uwanja wa Uhuru, Temeke June 17, 2021.

“Nimepewa jukumu kubwa sana maishani la kuwa Balozi wa Temeke, nitayatekeleza majukumu haya kwa umakini sana” ———Omondi
 
Mbunge wa Ilala (CCM), Mussa Azzan Zungu akizungumza bunge alipokuwa akichangia mjadala wa kupitisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/2022, jijini Dodoma leo.

Zungu amewataka wanaoponda mtandaoni kuhusu tozo mpya ya simu kufahamu kila wanapotuma ujumbe wa kukashifu au kutukana viongozi wanalipa tu kodi huku akisisitiza yeye haogopi kupigwa madongo kuhusu jambo hilo.
 
Kwahiyo unataka kugundua nini jamani kurudi kwenye ujana acha mimi niendelee na uzee wangu
Ulipo wewe nami niwepo hapohapo, kama ni kwa ujana niwepo kama ni kwa uzee niwepo ili kama ni ugunduzi tugundue pamoja we Shunie Shunie kipotabo ize tu keri shangazi (chibonge wa uongo
) mtoto mlito ~ hivi ni wa kidigo au wa kisambaa?
 
Hapo kwa kabila aje kunijibia smart Smart911

me mzee mwenzio na ujana siutaki kabisa acha niendelee kujizeekea
 
Uongozi wa Yanga SC umetangaza kumsimamisha golikipa wake Metacha Mnata ikiwa ni saa chache zimempita toka umalizike mchezo wa Yanga 3-2 Ruvu Shooting katika uwanja wa Benjamin Mkapa.

Yanga wamemsimamisha Metacha kwa tuhuma za utovu wa nidhamu alizozionesha baada ya kuzomewa na mashabiki kutokana na kutoridhishwa na aina ya goli la pili alilofungwa na Ruvu Shooting
 
Beki wa Real Madrid Sergio Ramos leo ameweka wazi kuwa alitaka kubaki Real Madrid lakini alinyimwa mkataba mpya tofauti na wengi walivyodhani, Ramos amekuwa Real Madrid kwa miaka 16.

"Chaguo langu la kwanza lilikuwa kubaki Real Madrid nilipewa ofa ya kusaini mwaka mmoja na kupunguziwa mshahara, pesa haikuwa ishu, nilitaka mkataba wa miwili kwa ajili yangu na familia yangu, baadae nilikubali ofa ya mwaka mmoja lakini club ikanijulisha kuwa ofa hiyo haipo tena” ——— Ramos
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…