Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambae kwa Sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge leo May 19 amekabidhi ofisi kwa Mkuu Mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla ambapo amewashukuru Watumishi wote wa Mkoa huo kwa ushirikiano mkubwa waliompatia wakati wa uongozi wake.
RC Kunenge amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa imani kubwa aliyomuonesha kwa kumteua kuongoza Mkoa wa Pwani.
RC Kunenge amesema ushirikiano wa kazi baina yake na Watumishi wote wa Mkoa viliwezesha kupatikana kwa mafanikio makubwa ambapo ametoa wito kwa Watumishi hao kuendelea kumpa ushirikiano huohuo Mkuu wa Mkoa Mpya ili aweze kutimiza maono ya Rais Samia Katika Mkoa huo.
Kwa upande wake Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amempongeza RC Kunenge kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanya Katika Mkoa huo na kueleza kuwa anaamini uwezo alioonesha Dar es salaam ataupeleka Mkoa wa Pwani.
Makabidhiano ya Ofisi yamefanyika mbele ya Viongozi wa Mkoa huo akiwemo Katibu Tawala wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wastaki Meya, Viongozi wa Usalama, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakuu wa Idara.
View attachment 1791056