Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210519_055219.jpg
20210519_055237.jpg
 
Keko kila mtu dalali...halafu hichi ni cha upepo
Heee! ni hivi kila mahali Bongo! kila mtu ni dalali!! ndo maana tunasema uishi kwa Bongo= Bongo land, pia ndo maana ikaitwa Bongo land!! sikutegemea jibu hili kwa Mwenyeji wa Bongo!! ..... unaujua Ubongo ???

Ni kikochi cha upepo??? Mwambie hivo hivo fundi kuwa ni cha upepo! Tube za magari zimejaa kule keko dogo tena bei rahisi tu! hawashindwagi kitu wale! Wewe mwenyeji wa wapi kijana????
 
“Kuna mabadiliko madogo nimefanya, Kafulila nilimteua kuwa RC Arusha na Mongella RC Simiyu, nimeamua Mongella kwasababu ulikuwa unaongoza Mkoa mkubwa basi ukawe RC Arusha na Kafulila kwasababu ndio anaanza alikuwa RAS basi akawe RC Simiyu”———Rais Samia Ikulu leo
20210519_135847.jpg
 
Kutokana na janga la Corona Simba SC kupitia kwa Afisa habari wake Haji Manara imetangaza kuwa CAF imeruhusu Mashabiki 10,000 tu kuingia uwanjani kutazama mchezo wa Simba SC vs Kaizer Chiefs.

"Mpaka sasa tumeruhusiwa Mashabuki 10,000 lakini tunaendelea kuomba kuongeza, naomba uwanjani rangi iwe nyekundu na nyeupe”———Haji Manara
20210519_140155.jpg
 
Afisa habari wa Simba SC, Haji Manara ameeleza kuwa licha ya Simba SC kupoteza 4-0 dhidi ya Kaizer Chiefs ugenini katika mchezo wa kwanza wa Robo Fainali ya Club Bingwa Afrika lakini wao wanataka kufuzu tu.

"Wanasimba wanataka kufuzu, hatutaki kujitahidi, Simba sio Timu ya kujitahidi, ni Timu ya kufuzu. Mashabiki wanaiamini Timu yao inaweza”———Haji Manara
20210519_140257.jpg
 
“Baada ya shughuli hizi za kuapishana na kupiga picha Wakuu wa Mikoa na Wateuliwa wengine mtarudi hapa na tutakuwa na kikao cha kazi kwahiyo kwasababu nina mambo mengi ya kuongea na nyinyi leo tuishie hapa tutakutana kwenye kikao cha kazi”———Rais Samia Ikulu Dar es salaam leo
20210519_140403.jpg
 
“Wapo Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wanaamini kule waliko wao ni Marais, utasikia Mimi Rais wa Mkoa huu au Wilaya hii nani kasema?, Rais wa Nchi hii ni mmoja tu, Samia Suluhu Hassan, ukijivisha koti ambalo si lako ukajidanganya kuwa wewe ni Rais, matokeo yake unaweza kufanya mambo ukidhania wewe ni Rais”———Spika Ndugai mbele ya Rais Samia wakati wa shughuli za uapisho Ikulu Dar es salaam leo
20210519_140501.jpg
 
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambae kwa Sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge leo May 19 amekabidhi ofisi kwa Mkuu Mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla ambapo amewashukuru Watumishi wote wa Mkoa huo kwa ushirikiano mkubwa waliompatia wakati wa uongozi wake.

RC Kunenge amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa imani kubwa aliyomuonesha kwa kumteua kuongoza Mkoa wa Pwani.

RC Kunenge amesema ushirikiano wa kazi baina yake na Watumishi wote wa Mkoa viliwezesha kupatikana kwa mafanikio makubwa ambapo ametoa wito kwa Watumishi hao kuendelea kumpa ushirikiano huohuo Mkuu wa Mkoa Mpya ili aweze kutimiza maono ya Rais Samia Katika Mkoa huo.

Kwa upande wake Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amempongeza RC Kunenge kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanya Katika Mkoa huo na kueleza kuwa anaamini uwezo alioonesha Dar es salaam ataupeleka Mkoa wa Pwani.

Makabidhiano ya Ofisi yamefanyika mbele ya Viongozi wa Mkoa huo akiwemo Katibu Tawala wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wastaki Meya, Viongozi wa Usalama, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakuu wa Idara.
20210519_192203.jpg
 
Heee! ni hivi kila mahali Bongo! kila mtu ni dalali!! ndo maana tunasema uishi kwa Bongo= Bongo land, pia ndo maana ikaitwa Bongo land!! sikutegemea jibu hili kwa Mwenyeji wa Bongo!! ..... unaujua Ubongo ???

Ni kikochi cha upepo??? Mwambie hivo hivo fundi kuwa ni cha upepo! Tube za magari zimejaa kule keko dogo tena bei rahisi tu! hawashindwagi kitu wale! Wewe mwenyeji wa wapi kijana????
keko napita sana ni karibu na nilipofikia mjin
 
Mbunge wa Jimbo la Konde kwa tiketi ya ACT -Wazalendo, Khatib Said Haji amefariki dunia leo asubuhi Alhamisi May 20, 2021 akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mazishi yatafanyika leo saa 10 Alasiri Pemba.
20210520_121351.jpg
 
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambae kwa Sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge leo May 19 amekabidhi ofisi kwa Mkuu Mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla ambapo amewashukuru Watumishi wote wa Mkoa huo kwa ushirikiano mkubwa waliompatia wakati wa uongozi wake.

RC Kunenge amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa imani kubwa aliyomuonesha kwa kumteua kuongoza Mkoa wa Pwani.

RC Kunenge amesema ushirikiano wa kazi baina yake na Watumishi wote wa Mkoa viliwezesha kupatikana kwa mafanikio makubwa ambapo ametoa wito kwa Watumishi hao kuendelea kumpa ushirikiano huohuo Mkuu wa Mkoa Mpya ili aweze kutimiza maono ya Rais Samia Katika Mkoa huo.

Kwa upande wake Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amempongeza RC Kunenge kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanya Katika Mkoa huo na kueleza kuwa anaamini uwezo alioonesha Dar es salaam ataupeleka Mkoa wa Pwani.

Makabidhiano ya Ofisi yamefanyika mbele ya Viongozi wa Mkoa huo akiwemo Katibu Tawala wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wastaki Meya, Viongozi wa Usalama, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakuu wa Idara.View attachment 1791056
Jamani hii si sawa kabisa mbona mimi sichaguliwi kuwa Mkuu wa MKoa wowote hapa nchini!!! Elimu, uwezo, wasaa, Ubunifu na hamu ya kuifanya hiyo kazi ninayo! Tangu nikiwa shule ya Msingi Bwana Nsa kaisy, Lawrance Gama

Hawa Marafiki zangu wakubwa wale wakiwa wakuu wa Mikoa niliyopita kimasomo Tabora, na Manispaa ya Mtwara walinishawishi Pakubwa sana kwa hizi nafasi mno!o mpaka kichwa kinauma!! hasa

walipokuwa wakikagua Gwaride, la vyombo vya ulinzi na Usalama Mjini Tabora hapo. daa nalipata burudiko la Moyo haswa! kama maji 823 KJ weee!! OP Progaramme ya chama! jamani Mweee!!

Lile gwaride la kijeshi bana la ajabu kidogo hata usipokula wala kunywa swafi tuu!! unatemebea Mwendo kama umekula tuu nashangaa watu wanazimia au kujifanya kule?? sijiui wana jeshi tulikuwa tunapewa nini kwa chakula?? tuyaache hayo

Sasa jamani wengine wakipewa naomba sana unikumbuke Mama yangu ! nilitegea uteuzi kwa Jiwe!! akanitosa tena makavu kabisaa, watu wake wa karibu na jiwe wakanitumbua kwa kunionea tu!! tena akazidisha msumari huyu nae ananipita tuuuu!!!

jamani Dunia si sawa yaani navo itamani kazi hii mpaka bichwa linaumaga hadi kesho Mama Samia unipe tu ka Ukuu wa Mkoa, ukikosa saaana basi ka wilaya,

kusema hivi mimi sitaki uwaziri sijui katibia Mkuu la hasha hizi kazi mbili!! uangalie km ikikupendeza yaani huwa nina ziota kabisaa!! nikilala naweweseka sana, Ukiona vipi Mama Samia nijaribu kama mwaka hivi uone!! nafanya kazi bure kwanza, kiisha isipokupendeza unitoe!!

Naomba uteuzi mimi Mwanao tufanye kazi Mama mbona umehangaikia Maishani kama mimi tu!! nalijifunza mengi kutoka kwako sana sana mpaka ukafikia hapo!! ulifanya tu maamuzi Najua humu unapita pita naomba tu unichungulie Mama yangu mimi kijana wako!!
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amemuagiza Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani asiishie kuwasimamisha kwa siku kumi tu Meneja wa TEHAMA wa TANESCO na Wasaidizi wake, bali wakae pembeni hadi hapo uchunguzi zaidi utakapokamilika.

Ametoa agizo hilo leo Mei 20, 2021 alipozungumza na Menejementi na Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwenye Makao Makuu ya Zamani ya Shirika hilo jijini Dar es Salaam.

“lazima tufundishane kuwa makini, kila siku lazima tukague vifaa vyetu ili huduma ipatikane muda wote, hakuna kuwasimamisha kwa siku 10, wakae pembeni hadi timu inayochunguza itakapotoa matokeo, inawezekana sio wao tu, Waziri endelea na uchunguzi”———Majaliwa

Waziri Mkuu ameliagiza pia Shirika hilo kuhakikisha wanakuwa na mfumo wa dharura ‘backup’ utakaotumika pindi kunapotokea changamoto za kimfumo———-“Mmetengeneza usumbufu mkubwa sana, mlijua lazima kuwe na backup lakini hakuna, toka pale tulipoanza kutoa huduma mpaka leo kwanini hakuna backup, hilo ni jukumu lenu”
20210520_130256.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom