Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi ameitaka kampuni ya SINO HYDRO inayofanya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Iringa kuhakikisha inakamilisha ujenzi huo kwa viwango na kwa wakati.
Hapi ameyasema hayo alipotembelea mradi wa ujenzi huo unaogharimu Tsh. Billion 41 na unatarajiwa kukamilika June 23, 2022.
“Wakandarasi wababaishaji natuma salamu kwao hawatakuwa na nafasi kwenye Mkoa wetu wa Iringa na hawatakuwa na nafasi kwenye Serikali hii, habari za kuomba kuongezewa muda kuchelewesha miradi,kufanya miradi chini ya kiwango hayo hayatakuwa na nafasi tutakuwa wakali zaidi tulivyokuwa jana”———Ally Hapi
Awali ujenzi huo ulisimama kutokana na kuchelewa kwa malipo ya fidia za mali za Wakazi wa Kata ya Nduli ambapo upanuzi huo umehusisha maeneo yao.
View attachment 1747360View attachment 1747362