Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais Magufuli anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku tatu katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam February 24 hadi February 26,2021, ambapo miongoni mwa atakayoyafanya ni kuzindua miradi ambayo tayari imekamilika.

Mkuu wa Mkoa wa Dare es salaam Aboubakar Kunenge @abubakar_kunenge amesema JPM ataanza ziara yake February 24 Kwa kuzindua Daraja la juu la Ubungo (Ubungo Interchange) kisha ataenda kuzindua Stand mpya ya Mbezi Luis.
20210222_183252.jpg
20210222_183240.jpg
20210222_183223.jpg
 
“Uchumi wa Tanzania umeendelea kuimarika katika kipindi cha miaka mitano iliyopita(2015-2019), uchumi ulikua kwa wastani wa 6.8% kwa mwaka na kuiweka Tanzania miongoni mwa Nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi zaidi Afrika baada ya Ethiopia na Rwanda”-Aristides Mrema, Mchumi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), wakati wa semina ya mafunzo kwa waandishi wa habari za uchumi na biashara Mkoani Mtwara leo

“Sekta zilizochangia zaidi ukuaji wa uchumi wa Tanzania kwa wastani wa 6.8% kwa mwaka katika kipindi cha mwaka 2015 hadi 2019 ni pamoja na ujenzi (25%),kilimo (20%), viwanda (9.6%),usafirishaji na uhifadhi mizigo (8.3%) na biashara (7.3%)”
20210222_183533.jpg
 
“Watuhumiwa hawa wanne tunaowashikilia Frank Nyange na wenzake, pamoja na wengine ambao tunawatafuta, licha ya kueneza uvumi wa vifo vya Watu wakidai wamekufa kwa Corona, pia wanatia hofu Mitandaoni kwa kudai Watanzania walio wengi watakufa kwasababu Serikali haichukui tahadhari dhidi ya Wananchi wake”-Wankyo Nyigesa, RPC Pwani

“Polisi Mkoani Pwani tunatoa rai kwa Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Corona kwa kufuata maelekezo ya Wataalamu wa Afya na kujiepusha na matumizi mabaya ya Mitandao ikiwemo kutoa taarifa za uvumi kuhusu vifo vya Watu ambazo zinatia hofu Wananchi wengi, hatua za Kisheria zitachukuliwa kwa watakaofanya hivyo” - RPC Pwani
20210222_183733.jpg
 
Serikali imesema imechukua hatua za kutumia ndege kunyunyiza viuatilifu (sumu) ili kuua makundi ya nzige wa jangwani ambao wamevamia maeneo ya Wilaya za Simanjiro na Longido na kuhatarisha ustawi wa mazao na malisho ya mifugo kwenye maeneo hayo.

Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda ametembelea eneo la Wilaya ya Longido ambalo limevamiwa na nzige wa jangwani ambapo amesema kuwa kuanzia leo ndege maalum itafanya kazi kupulizia viuatilifu kuua nzige hao.

Prof. Mkenda amewaeleza Wananchi na Viongozi kuwa wasiwe na hofu nzige wote watadhibitiwa kupitia Wataalamu wa Wizara ya Kilimo waliopo kwenye maeneo yote yenye dalili za uwepo wa wadudu hao nchini.
20210222_184133.jpg
20210222_184115.jpg
 
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema inaendelea kusimamia na kusisitiza utekelezaji wa tahadhari ya magonjwa mbalimbali yasiyoambukiza na ya kuambukiza yakiwemo ya milipuko ikiwemo tishio la ugonjwa wa COVID-19 linaloikabili Dunia kwa ujumla.

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumapili, February 21, 2020 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali WAMJW-Afya, Gerard Chami.

”Wizara ya Afya inawasihi Wananchi kupata lishe bora ikiwemo matunda na mbogamboga, pia matumzi ya Tiba Asili zilizosajiliwa na Baraza la Tiba Asili na kama inavyoelimishwa na Wataalamu husika”
20210222_184448.jpg
 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amezikosoa vikali nchi ambazo zinatumia kisingizio cha janga la COVID-19 kuwakandamiza wapinzani, vyombo vya habari na wakosoaji wa serikali.

Akizungumza kwenye kikao kikuu cha kila mwaka cha Baraza la Haki za Binaadamu la Umoja huo mjini Geneva hivi leo, Guterres amesema kwamba serikali za mataifa kadhaa zimetumia vikwazo ambavyo viliwekwa kudhibiti kusambaa kwa virusi vya corona kudhoofisha upinzani wa kisiasa.

Bila ya kuzitaja nchi kwa majina, Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa amesema baadhi ya wakati vikosi vyenye silaha kali vimetumwa kwa wapinzani, huku uhuru wa kujieleza ukigeuzwa kuwa ni tendo la kihalifu, na wakati huo waandishi na jumuiya za kiraia zikizuiwa kuripoti juu ya maradhi ya COVID-19. Guterres amewakosoa vikali viongozi wakuu wa nchi wanaotumia upotoshaji kulielezea janga hilo.
20210222_185024.jpg
 
Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila ameondolewa kikosi maalumu cha wanajeshi waliokuwa wakimlinda na kupelekewa polisi wa kawaida. Siku moja baada ya hatua hiyo, kiongozi huyo ameonekana akielekea Dubai hali iliyoibua minong'ono juu ya kuibuka mtafaruku zaidi baina yake na rais Felix Tshisekedi. Je hatua ya kupunguzwa walinzi inamaanisha nini? Zaidi kuhusu hilo, sikiliza
20210222_185239.jpg
 
Shirika la umeme la Kenya, KPLC limelazimika kubadili mfumo wa nyaya za umeme zinazopita katika hifadhi ya wanyama ya Soysambu Nakuru, baada ya twiga wawili kufa baada kugusa nyaya hizo.


Shirika la wanyama pori la Kenya KWS lilijulishwa kuhusu vifo vya twiga hao adimu wa spishi ya Rothschild waliofariki kwa kupigwa na moto mkubwa hiyo jana 21 Februari.


Ripoti za awali zilisema twiga hao wamekuwa warefu na kumefika kimo cha nyaya za umeme Lakini wanaharakati wa mazingira wanadai nyaya za umeme ziliwekwa kwenye kimo cha chini kuliko ilivyokawaida na hivyo kusababisha ajali hiyo.



"Nyaya hizi za umeme zimekuwa zikiwaua twiga na wanyama wengine. Ripoti ya kiufundi ya kutathmini manufaa na hatari kabla ya mradi kuidhinishwa na serikali zinafanywa kiholela.
Inasikitisha kwamba hadi hali kama hii itokee ndio hatua ichukuliwe!"

Mwanaharakati mhifadhi wa wanyama Paula Kahumbu aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter .


Sasa KPLC wametuma vikosi vya wahandisi kusuluhisha tatizo hilo
20210222_185542.jpg
20210222_185526.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom