Barcelona wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Uingereza na Manchester United Marcus Rashford, 21. Mkataba wa mshambuliaji huyo na United utaisha 2020. (Mundo Deportivo - in Spanish)
Miamba hiyo ya La Liga inamouna Rashford kama mbadala wa muda mrefu kwa mshambuliaji wao nyota Luis Suarez, lakini United hawatazamiwi kumuuza mshambuliaji huyo. (ESPN)
Arsenal wana nia ya kuwauza viungo wake Henrikh Mkhitaryan, 30, na Mesut Ozil, 30, kama njia ya kupunguza gharama kubwa za mishahara za klabu hiyo. (Mirror)