Makapuku Forum

Makapuku Forum

ILI UFANIKIWE FANYA YAFUATAYO,
Tambua kitu au shughuli unayoitamani na komaa nayo hadi upate kile ulichokitegemea katika shughuli ile kwa mfano, unatamani kuwa mwimbaji maarufu, hakikisha unafanya juhudi katika hiyo shughuli unayoitamani.

Fanya kitu au shughuli unayoipenda, siri mojawapo katika kuleta mafanikio ya kweli ni kupenda shughuli au kazi unayoifanya kwa mfano, wewe kama ni mmachinga, penda kazi hiyo kwani usipoipenda haitafanyika vizuri kwani kazi nyingi zinahitaji moyo mgumu na wa ziada ili kuifanikisha, kwa kazi ya umachinga inahitaji muda mwingi kuifanya yaani inahitaji kuamka mapema na kuchelewa kulala vipi, usipoipenda, utaifanya?
 
Badili fikra zako, epuka kuwaza kushindwa na waza mafanikio. Utakuta mtu hata bado hajaanza kazi fulani anasema, hawezi wakati hajafanya akashindwa kwa mfano, suala la ujasiriamali, ukimwambia mtu aanze kujishughulisha na ujasiriamali, jambo la kwanza atasema, hawezi kutengeneza bidhaa kama sabuni na mafuta ya kupaka. Wengine watasema, hawawezi kwani hawana mtaji, hebu jiulize, ukiambiwa kuna gari jipya aina ya Noah au Toyota linauzwa shilingi za kitanzania laki moja na nusu (150,000/=) hutazipata?




Ukweli ni kwamba, mjasiriamali wa kawaida huanza na mtaji chini ya laki na nusu na faida na mtaji huongezeka kadri anavyoendelea kufanya biashara na hatimaye kumiliki biashara kubwa. Hivyo ondoa ile fikra ya kushindwa na jiamini kuwa unaweza.
 
Endeleza wazo linalokujia, usiliache liyeyuke. Kwa mfano, unaweza kukaa chini na ukawaza kuanzisha biashara fulani, wazo hilo lifanyie kazi ili kama linawezekana liendeleze katika vitendo. Watu wengi mawazo yao mazuri hufa kwa kutopewa kipaumbele na matokeo yake mtu hufa masikini. Jiulize, mawazo yako mangapi yameyeyuka?
 
Jiongoze mwenyewe na usimruhusu mtu aongoze maisha yako. Mara nyingi watu wanapopata wazo la kufanya jambo fulani huwauliza marafki zao na matokeo yake hushauriwa vibaya na kukatishwa tamaa. Inasemekana kuwa, Picha kubwa ya maisha unayoyatamani imo ndani kabisa moyoni mwako, hivyo usimruhusu mtu yeyote aiharibu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom