Makapuku Forum

Makapuku Forum

Usiabudu mtu, jiabudu mwenyewe. Kuna kasumba za watu ambao wana tabia ya kuwaabudu matajiri. Kwa mfano, wafanyakazi wengi hasa wale wa sekta binafsi kama vile wahudumu hotelini na wengine wanapoteza uwezo wao halisi wa kufanya kazi kwa kuwa mkurugenzi yupo karibu yao na hivyo wafanyakazi wanakuwa waoga ambao unatokana na kuamini kuwa mkurugenzi huyo anao uwezo wote juu ya maisha yao hivyo kusahau kuwa nao wanaweza kumiliki mradi kama huo na mkurugenzi pia ni mtafutaji kama wao na siku moja wanaweza kumuajiri katika miradi yao.
 
Tafuta mlezi kocha katika kazi unayoifanya au unayotaka kuifanya. Huyu atakusaidia kukupa mbinu na kukuelekeza namna ya kufanya shughuli hiyo. Ninaposema KOCHA ninamaanisha kuwa mlezi huyo awe mtu anayefanya shughuli hiyo, ameizoea na anaijua kwa undani zaidi.
 
Epuka kufanya kitu pasipokuwa na mtu wa kukuongoza ambaye pia anafanya au ana utaalam juu ya shughuli hiyo.

Kumbuka kuwa yaliyopita yamepita, yawezekana umewahi kufanya jambo fulani ukashindwa hapo awali, fumba macho usitazame matokeo ya nyuma, anza upya na utafanikiwa. Mara nyingi watu hutumia matokeo ya nyuma kufanya maamuzi ya sasa na ya baadae na wengine utasikia wanasema, mbona fulani alifanya na akashindwa, na wewe pasipokufikiri kwa umakini kuwa ni yeye lakini wewe utaweza kufanikiwa.
 
Jifunze kuwa na malengo makubwa, huwezi kufanya jambo lolote la mafanikio bila kuwa na malengo juu ya kazi hiyo. Malengo ndio kichochezi kikuu katika kutafuta mafanikio. Wataalam wanasema, mtu asiye na malengo anafananishwa na dereva anayeendesha gari bila kujua aendako. Kadri unavyokuwa na malengo makubwa ndivyo unavyokuwa na bidii ya kuhakikisha unafikia malengo yako.
 
Ongoza pesa zako na si kuziachia pesa zikuongoze. Watu wengi huongozwa na pesa ambapo mtu akiwa na pesa utamjua tu kwani atabadilika, kama kunywa pombe atalala baa. Unashauriwa, kuongoza pesa yako hata kama ni nyingi kiasi ambacho ni mara yako ya kwanza kuzipata. Hii itakusaidia kujiwekea faida na kujua mapato na matumizi ya kila siku.
 
Jifunze kujitegemea, epuka utegemezi kwa watu. Ni tabia ya baadhi ya watanzania kutojifunza kujitegeme kwani unakuta mtoto wa kiume mwenye umri wa kribani 27 bado anaishi nyumba moja na wazazi huku akilishwa kama mtoto mdogo na pengine kama ana biashara anaiendesha kwa msaada wa mzazi wake na hivyo kufanya biashara akijua hata akipata hasara mzazi atamsaidia na wengine hukaa nyumbani hadi wazazi wanaamua kuwaanzishia biashara lakini kwa kawaida biashara hizo hufa kwani wazo la biashara linatakiwa litoke ndani ya moyo wake na si kutoka kwa mtu mwingine.
 
Usiache kujifunza, siku zote watu hudhani wanajua kila kitu lakini ukweli ni kwamba kila kukicha kuna mambo mapya yanagundulika hivyo, kujifunza hakuna kikomo. Kuna kasumba za baadhi ya watu hudhani kuwa mtu akisoma hadi chuo kikuu basi anajua kila kitu, hii si kweli kwani masomo ya darasani ni tofauti na masomo ya maisha yanayopatikana katika mazingira yetu na elimu hutusaidia katika kuendana na mabadiliko ya mazingira.
 
Hivyo, mtu anashauriwa, hata kama ana elimu kubwa akitaka afanikiwe kimaisha anatakiwa kutodharau mafunzo mbalimbali yanayopatkana katika mazingira husika ikiwa ni pamoja na semina ambazo zinaweza kukupa wazo juu ya fursa zilizopo.
 
Jifunze kujitegemea, epuka utegemezi kwa watu. Ni tabia ya baadhi ya watanzania kutojifunza kujitegeme kwani unakuta mtoto wa kiume mwenye umri wa kribani 27 bado anaishi nyumba moja na wazazi huku akilishwa kama mtoto mdogo na pengine kama ana biashara anaiendesha kwa msaada wa mzazi wake na hivyo kufanya biashara akijua hata akipata hasara mzazi atamsaidia na wengine hukaa nyumbani hadi wazazi wanaamua kuwaanzishia biashara lakini kwa kawaida biashara hizo hufa kwani wazo la biashara linatakiwa litoke ndani ya moyo wake na si kutoka kwa mtu mwingine.

...huu ni mtizamo mzuri, lakini katika kujitegemea tambua kuwa kuna kutegemeana (tuseme mfano wa ecosystem-interacting organism + physical environment). Tunategemeana sana kupata mawazo mapya, kujifunza na kufundisha.
Hapa inabidi mmoja utoke kwenye comfor zone yako uingie kwanye uwanda wa kukuchakarisha, sio lazima uwe peke yako, unaweza kuwa na wengi wenye lengo linalofanana.

Asante kwa andiko fupi zuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom