Moja ya anguko kubwa sana la kibiashara kuwahi kutokea Duniani, ni kutoka Kampuni ya Nokia. .
.
Jifunze kitu, Mwaka 1998 Nokia alitajwa kuwa kampuni kubwa ya Simu za mkononi Duniani.
.
.
Mwaka 2003,Walitoa simu ya "Nokia 1100" ambayo ilitajwa kuja kuleta mapinduzi makubwa katika Ulimwengu wa Simu na kweli ilinunuliwa Haswa (SWIPE KUIONA) na mpaka sasa ndio Brand ya Nokia ambayo imenunuliwa zaidi kuzidi zingine... Lakini hapa ndipo matatizo yalianzia...Kivipi?
.
.
Ni hivi... Wakati Apple wanatoa simu ya iPhone toleo la kwanza mwaka 2007, asilimia 95 ya simu zote duniani zilizokuwa zikitumiwa na watu zilikua ni Nokia. .
.
Lakini Chaajabu ni baada ya Miaka 5 mbele Thamani ya Nokia ilishuka kwa takribani asilimia 90, na mwaka 2013 Microsoft waliinunua Nokia hapo ndio Wakazidi kujizika zaidi. .
.
Kuna kitu Tujifunze, Kilichowaangusha Nokia ni Kubweteka na Sifa kemkem Walizokuwa wakipewa, Walijiona wao ndio bora na hakuna Kampuni yoyote ingeweza Kuwapindua hivyo Walikosa kuendana na Soko Kwa kushindwa kuleta Ubunifu mzuri kwa Haraka Na Chaajabu zaidi katika Kampuni ambayo hata hawakuifikiria au Haikufikiriwa ingeweza kufanya Maajabu katika Upande wa Simu ni Apple. .
.
Sababu wao walionekana kuwa wapo upande zaidi wa computers na iPod.. Lakini kilichowatokea hawatokaa Kuamini mpaka sasa. .
.
Wakati wanastuka kutoka Usingizini, ilikua tayari hali imebadilika licha ya kujitahidi kufanya mabadiriko kadhaa Bado hali kwao imekuwa ngumu. .
.
Mambo yanaweza kubadirika kwa haraka sana zaidi hata unavyofikiria, Hakuna Muda wa kupoteza. Hakikisha Unapambana kikamilifu kwa nguvu sana, Sababu Wakati wewe unafurahia Mafanikio yako, Kuna mtu yupo Chini Anapambana Afikie Mafanikio tena katika Jambo ambalo wewe Pia Unafanya. .
.
Acha Kuutumia UBONGO wako katika mambo yasiyofaa, Hakikisha kila siku unakuwa mtu mpya. .