Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: 2018 Ilikuwa Nzuri

Ninaandika kukushukuru wewe mdau wa Jukwaa hili ambaye kila wakati sichoki kukwambia kuwa unalifanya Jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kabisa kuwepo. Ni kutokana na wewe, yes, wewe unayesoma sasa, MF imekuwa ni sehemu ya kipekee katika JF. Nimeweza kuelimika na kujifunza mengi kupitia wewe, ninaamini nami nimekuwa na mchango kiasi kwako, maana maarifa/kujifunza ni 2way trafiki.

Nakushukuru sana Lyon Lee , Shunie , Tumosa , Transcend , SHIMBA YA BUYENZE , BlessedHope (mama yenu huyu na ninampenda sana), Mndali ndanyelakakomu , Tetramelyz , Clkey , shululu , The Book , Da'Vinci , husna muba , Nyagei mtaasisi mwenzangu, Bitoz , Jimena , ningendako , demi , Sakayo , ABJ , Mtoto halali na hela , Mussolin5 marybaby , Madame S , capitalpool , dingimtoto , hearly , Wick , Malcom Lumumba na wewe ambaye nimesahau kukutaja lakini unajijua kuwa umekuwa sehemu nzuri ya kunifunza, kunirekebisha na zaidi kulifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Ninaamini kiuhakika sisi ni marafiki ambao hatujakutana.

Muziki sasa, nakumbuka wakati naanza kuandikia kipengele cha muziki ( baadaye niliandika kipengele cha kisiasa Tafasiri Unavyoweza) nilisema napenda muziki wenye gitaa na si kinanda pekee, hapa niliweka kina Kalala Hamza, Mabela, Ray Vaughan, BB King, Jimi H, Santana, Franco Luambo, Buddy Guy, Tracy Chapman na wengine wengi. Nyimbo nyingine uliziomba wewe na ulijua kabisa mimi ni kijana mwenye mambo ya kizee sababu ya aina ya muziki nilioanza kuweka hapa, Jazz, Blues na Afro. Burudika na hizi ambazo zilibamba humu na hii ni kwa sababu wewe umekuwa na msaada kwangu. Asante na nikuambie tu ulikuwa mtu muhimu 2018 na ninaamini tutaendelea kuwa binadamu 2019
Love
Obe









NB: Ninajaribu kumaliza bundle langu kwa hiyo kama bundle lako ni la wasiwasi basi nakutakia mwaka mpya mwema
 
Muziki: 2018 Ilikuwa Nzuri

Ninaandika kukushukuru wewe mdau wa Jukwaa hili ambaye kila wakati sichoki kukwambia kuwa unalifanya Jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kabisa kuwepo. Ni kutokana na wewe, yes, wewe unayesoma sasa, MF imekuwa ni sehemu ya kipekee katika JF. Nimeweza kuelimika na kujifunza mengi kupitia wewe, ninaamini nami nimekuwa na mchango kiasi kwako, maana maarifa/kujifunza ni 2way trafiki.

Nakushukuru sana Lyon Lee , Shunie , Tumosa , Transcend , SHIMBA YA BUYENZE , BlessedHope (mama yenu huyu na ninampenda sana), Mndali ndanyelakakomu , Tetramelyz , Clkey , shululu , The Book , Da'Vinci , husna muba , Nyagei mtaasisi mwenzangu, Bitoz , Jimena , ningendako , demi , Sakayo , ABJ , Mtoto halali na hela , Mussolin5 marybaby , Madame S , capitalpool , dingimtoto , hearly , Wick , Malcom Lumumba na wewe ambaye nimesahau kukutaja lakini unajijua kuwa umekuwa sehemu nzuri ya kunifunza, kunirekebisha na zaidi kulifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Ninaamini kiuhakika sisi ni marafiki ambao hatujakutana.

Muziki sasa, nakumbuka wakati naanza kuandikia kipengele cha muziki ( baadaye niliandika kipengele cha kisiasa Tafasiri Unavyoweza) nilisema napenda muziki wenye gitaa na si kinanda pekee, hapa niliweka kina Kalala Hamza, Mabela, Ray Vaughan, BB King, Jimi H, Santana, Franco Luambo, Buddy Guy, Tracy Chapman na wengine wengi. Nyimbo nyingine uliziomba wewe na ulijua kabisa mimi ni kijana mwenye mambo ya kizee sababu ya aina ya muziki nilioanza kuweka hapa, Jazz, Blues na Afro. Burudika na hizi ambazo zilibamba humu na hii ni kwa sababu wewe umekuwa na msaada kwangu. Asante na nikuambie tu ulikuwa mtu muhimu 2018 na ninaamini tutaendelea kuwa binadamu 2019
Love
Obe









NB: Ninajaribu kumaliza bundle langu kwa hiyo kama bundle lako ni la wasiwasi basi nakutakia mwaka mpya mwema
Hahahhaha bundle la wasiwasi
 
Tatzo binamu anakuja kimya kmya,,,acha apambane na hali yake kwanza

Msumbufu sana huyu,,,atataka mizigo yote amiliki yeye

Sent using Jamii Forums mobile app

...sikuja kimyakimya, yaani labda hukusikia tu, pale stesheni walijaa watu kunipokea, watu kibao nadhani wengine walikuja kupokea ndugu zao toka Mpanda maana mimi nilitokea Mtwara.

Ilibidi nije natreni ndo maana ulisikia makelele, ningelipwa ningekuja na bombadia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom