Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mikato ya nywele inafaa kuzingatia kichwa










Hakuna kitu kinachofurahisha kama nywele za mwanamke. Nywele za mwanamke zinapowekwa sawa na uso wake, humfanya awe na mng'ao usiokuwa wa kawaida.
Nywele za mwanamke zinaheshimika zinathaminika na ama hakika ni hazina moja ya maana kwa mwanamke iwe zimekaangwa au zimewekwa tu kama vile mchemsho.
 
Nywele na staili zake hazijabadilika sana ingawa zamani nywele zilikuwa zinawekwa vitu vingi katika mizungusho ya kawaida ya kuremba na wakati mwingine kuachwa tu zikijiotea na wengine wakitumia muda mwingi kuzisuka.
Ni vyema kama mwanamke unataka kupendeza kichwani kufika kwa wataalamu wa nywele ambao watazitengeneza au kukupa ushauri kutokana na kichwa chako na si vingine.
Ni kutokana na hali hiyo lkeo tunakuletea picha mbalimbali za watu na miondoko yao kichwani kwa lengo la kukuonyesha kwamba unachosuka kichwani inafaa kifanane na kichwa chako.
 
Si misuko tu bali hata utengenezaji wa huria wa kutumia dawa au hata dawa za asilimi ni lazima izingatiwe ukubwa wa kichwa na namna ambavyo ungelipenda wewe uonekane.
Zamani misuko ilikuwa ya kuchekesha zaidi na matumizi ya kofia yalimaliza utata uliopo kichwani kwa wakati unapoangaliwa kwa makini.
Nataka kukuambia kwamba nywele nyingi hutengenezwa kwa kuangalia unataka kumvutia nani na kwanini.
 
Chumvi,sukari nyingi huzeesha ngozi

Shosti niwaambieni kuwa matumizi makubwa ya chumvi au sukari ni hatari na sumu kubwa katika ngozi zetu kwani husababisha ngozi kuwa na makunyanzi kabla ya umri.

Kawaida makunyanzi hutokea unapokaribia kuimaliza miaka ya 40.Watu ambao ngozi zao zimeathiriwa na matumizi makubwa ya sukari na chumvi wanashauriwa kupunguza matumizi yavitu hivyo kwa kula mboga za majani na matunda kwa wingi ili kuweza kuondoa sumu ambayo imejengekamwilini na pia kunywa maji mengi.
 
Wanasayansi wanasema kuwa, watu wanaotaka kutunza ngozi zao kutotumia sukari kwa wingi kwani sukari huchangia kuzeesha ngozi. Sukari nyingi hufanya misuli ya protini katika ngozi kujikusanya pamoja na kusababisha kutoweka kwa mnyunyuriko unaotakiwa.

Ili ngozi iwe laini ni yema ukanywa maji mengi, maji husaidia kulainisha miili yetu kwani mwili unapokuwa hauna maji ya kutosha unakuwa mkavu na ngozi haipendezi hata kama unatumia vipodozi vya aina mbalimbali na vya gharama. Ni bora kuulisha na kuunywesha mwili wako ili ngozi ijitengeneze yenyewe.
 
Namna yakujiweka fiti kwa mwanamke

Katika kujiweka fiti au tuseme kujiweka sawa kwa ajili ya kuonekana mrembo ni kazi ambayo inahitaji muda na uvumilivu vinginevyo unaweza kuwa sawa na chizi yoyote aliyejiwekea si tu maleba bali na mwili usiotamanika.
 
Na kwa mwanamke ambaye ana mji wake, watoto , familia na kazi inayohitaji ukakamavu mkubwa huku akitakiwa kuonekana bomba namchangamfu ni dhahiri kuwa la ziada lazima lifanyike vinginevyo mahali fulani utapwaya.unaweza kupwaya ofisini, ukaonekana huna maana , unaweza kupwaya nyumbani mtoto mkubwa akashindwa kukuangalia mara mbili na unaweza kupwaya mtaani watu wakajiuliza hee mama fulani vipi mbona usafi unamshinda?ndio kusema katika hili unahitaji mwanamke kuwa makini sana.
 
Inavyoonekana wanawake wengi wanapokuwa katika mtawanyiko wa mambo hujisahau kabisa na mara nyingi husahau kabisa kuwa wanahitaji kula nakufanya vitu fulani ili kujiweka fiti.Kimsingi wanawake wote wawe wanachapa kazi kama wazimu, wawe na familia, wawe na mtoto mkubwa wanatakiwa kujiweka safi na sawa muda wote pamoja na majukumu yao yaliyotawanyika.
 
1) siku zote hakikisha una tunda wakati wa kifungua kinywa chako. Hii unasaidia kuondoa sumu katika mwili wako na kusaidia kuondoa uchafu uliojiweka kwa namna inavyostahili.

2) Kunywa maji ya kutosha , punguza chai na kahawa kufikia angalau vikombe viwili kwa siku na muda uliobaki kunywa vinywaji ambavyo ni vya mizizi kama jasmine, chamoile tea. Vinywaji hivi katika mfumo wajuisi ni dawa tosha kwa ngozi yako na ili ionekane ya ujana muda wotena isiwe kavu.
 
3) Huku umri wako ukiwa unapanda,punguza vyakula vya nafaka na kulazaidi matunda na mbogamboga ili kupunguza uzito.

4) hakikisha unatembea vya kutosha na kujinyoosha ili uwe na mwili wakuvutia, mwembamba na wenye nguvu za kutosha na wa ujana.
5) Punguza uvutaji sigara na pombe kwani ni vitu viwili vinavyozeeshangozi kwa kasi.
 
6) Ongeza vyakula vya samaki katika chakula chako au aina yake

7) Uwe unakula na mizizi inayokabiliana na uzee kama tulsi, amla, ashwagandha

8) Jipatie vitamu vya asili kama asali na raisins.

9) Kula vyakula vyako unavyopenda vya hovyo angalau mara moja kwa wiki

10) Kujisikia vyema ni namna bora za kukufanya uwe mwanamke bomba naanayevutia muda wote.

NB:Kujisikia vyema huku ni kujipenda mwenyewe kama hujipendi huwezi kuvutia na kama unaridhika kwa sababu ya kuridhika una tatizo kwelikweli.
 
NAMNA NZURI YA KUOSHA NYWELE ZAKO


KUNA kitu muhimu kuhusu uoshaji wa nywele, nywele zako ambazo unataka zikae unavyotaka kulingana na kichwa chako ili uwe na uvuto wa haiba yake katika mambo yote yanayokuzunguka.
 
katika mazingira ya kawaida uoshaji nywele ni kitu cha kawaida na hivyo mara nyingi hatufikirii sana suala la kuosha nywele, si la kawaida tu mwenzangu? Lakini uoshaji nywele wa uhakika wenye makini kwa kutumia shampuu kunaweza kuleta mabadiliko makubwa katika muonekano na umetaji wa nywele zako na hata makuzi yake.
Ndio kusema uoshaji wa kutumia shampuu unaweza kabisa kukupa kile ambacho huwezi kukipata katika hali ya kawaida , muondoko wa ukaaji wa nywele baada ya kuosha.
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Lakini kama hutajali tulijadili hili suala la uoshaji nywele ambalo ni la kawaida tu.Naama, la kawaida lakini lenye maana kubwa kwa watu wanaojijali.
Mimi nadhani haitaumkiza kama nikisema kwa ufupi fupi kuhusu hizi shampuu za kuonshea nywele, hizi shampuu ambazo unazipata dukani, kwenye dula la urembo.
Kwanza ni lazima utambue kwamba si kila shampuu inafaa katika kusuklia nyweleza ko (uoshaji) kwani nyingine huleta mushkeri hasa kama unaumwa eczema, hali ya kuchoma choma, uwasho wa nywele, mba au aina ya grisi katika ngozi ya nywele zako wakati wa kuzitengeneza.
 
Nataka kukuambia kwamba bidhaa zinazotokana na uasili husaidia sana kutengeneza utamu wa nywele kama kweli unaujua na mara zote hufanyakazi bora kwa aina zote za vichwa hata kama zina matatizo niliyotaja hapo juu.
Na pia huleta aina ya burudiko.
Mara zote tunapoosha nywele zetu huwa tunaharibu lakini kama utakuwa mwangalifu kwa kutumia shampuu zenye viambata vya asili (organiki-natural botanical)utakuwa na nafasi kubwa ya kuwa na nywele tamu na wewe kuondokana na adha za uchafu wa nywele unaotia 'wazimu'.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom