Tarehe 2 mwezi wa 11, mwaka 2000 ndiyo ilikuwa mara ya mwisho kwa binadamu wote kuwa Duniani kwa wakati mmoja.
Tangu hapo watu wamekuwa wakishinda kwenye kituo cha kimataifa cha anga za juu (ISS), na mpaka muda huu kunawatu wapo kwenye kituo hicho wanafanya kazi.
Huawei wanaswa kutumia kamera za DSLR kwenye matangazo ya simu zao. Hii imefahamika hivi karibuni baada ya mmoja kati ya mwanamitindo aliyetumika katika tangazo la simu za Huawei, kuweka picha iliyokuwa inaonesha jinsi walivyotengeneza tangazo hilo kwenye akaunti yake ya Instagram.
Sayari hizo zipo kwenye nyota changa iliyoko umbali wa miaka 500 ya mwanga kutokea Duniani ambayo kwa sasa ina umri wa miaka bilioni 2 iliyopita.
Nyota hiyo ukubwa wake ni kama asilimia 80% ya ukubwa wa Jua letu na nusu ya umri wake.
Kitu ambacho kinawachanganya wanasayansi ni uwepo wa sayari kubwa sana CI Tau b pamoja na ndugu zake wengine wanaoizunguka sayari hiyo ambayo bado hata sahani la mavumbi na gesi zilizochangia uundwaji wake kitaalamu linalofahamika kama protoplanetary disk halijatoka.
CI Tau b ukubwa wake ni mara 10 ya ukubwa wa Sumbula - sayari kubwa zaidi kwenye mfumo wetu wa Jua, na inakamilisha mzunguko wake kwenye hiyo nyota kila baada ya siku tisa. Kwa mlinganisho Sumbula inakamilisha mzunguko wake kwenye Jua letu kila baada ya miaka 12.
Wanasayansi mwanzo walifikiri sayari kubwa kama hizo huwa zinachukua muda sana mpaka kutengamaa ila uelewa wao huo umebadirika baada ya kuona CI Tau b ambayo imetengamaa haraka kuliko hata nyota inayoizunguka.
Licha ya Dunia yetu kuwa moja kati ya sayari ndogo sana kwenye mfumo wetu wa Jua, Dunia ndiyo sayari yenye uzito mkubwa kuliko zote kutokana na kuundwa kwake kwa mawe na nyenzo zingine ambazo hazipo kwenye sayari zingine.
Hizo sayari zingine kubwa zimeundwa kwa gesi tupu na zina dense ndogo sana kiasi cha kwamba unaweza ukaziweka juu ya maji na zikaelea.
Kuna mtu alishawahi kumuuliza 'live' wakati alipokuwa anasoma komenti za watu wakati wa Q&A kwenye mtandao wake wa Facebook, jamaa alimuuliza "Are you a lizard?" Mark alikwepa swali na Q&A ikaisha.
Utafiti uliofanywa na chuo cha Harvard unaonesha wanaume wanaojichua au kufanya mapenzi mara 21 au zaidi kwa mwezi wanapunguza uwezekano wa kupata saratani ya tezi dume kwa asilimia 33%.
Katika tafiti zilizofanywa kipindi cha nyuma zilikuwa zinaonesha kufanya mapenzi mara kwa mara kunasaidia kupunguza hatari ya kupata saratani hiyo, ila utafiti huu wa Harvard umehusisha na kujichua ambapo vitendo hivyo vinasaidia kuondoa toxins zinazosababisha saratani kwenye kibofu.
Wapiga puchu hapa mmepata sababu sabuni zitaadimika sasa
Hii ni barua ya kuombea kazi iliyoandikwa kwa mkono na Steve Jobs alipokuwa na miaka 18 mwaka 1973. Barua hii iliuzwa kwenye mnada kwa dola 174,000 (milioni 300).
Haikufahamika Steve Jobs alikuwa anaomba nafasi gani ya kazi. Kwenye elimu aliandika amesomea English Literature chuoni Reed japo aliacha masomo baada ya kusoma semista moja mwaka 1972.
Pia ameandika anauzoefu wa kutumia kompyuta pamoja na kikokotoo. Inasemekana mwaka mmoja baada ya kutuma maombi Steve Jobs alipata kazi kwenye kampuni ya kutengeneza michezo ya kompyuta 'Atari' kisha miaka michache baadae aliamua kuacha na kuanzisha kampuni yake iliyoitwa 'Apple' mwaka 1976, akiwa na mwenzake Steve Wozniak.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.