Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kama mwanamke atajiona yupo appreciated nje ya chumbani basi akifika chumbani atakuwa mwenye furaha (excited), hivyo haina maana kusubiri umpe maneno matamu akiwa kitandani badala yake mpe maneno matamu kuanzia jikoni au sebuleni.

“Never tell a woman she is beautiful when lights are off”

Mwanamke ana hamu kubwa ya ukaribu wa kimapenzi (intimacy) kutoka kwa mume wake, kujisikia yupo karibu na connected.


Kwa mwanaume sex hutokea kule downstairs chini ya mkanda ulivaa, kwa mwanamke sex ni upstairs, kwenye kichwa chake (brain).

Ndiyo maana kwao foreplay ndiyo mfumo wa maisha ya mapenzi.

Na ndiyo maana hawafiki kileleni mara zote.
 
Wanawake hutumia muda mwingi kuwaza ni kitu gani wanaume wanahitaji katika mahusiano na tatizo kubwa ni kwamba wanaume wachache sana huwaza kuhusu nini wanawake wanahitaji katika mahusiano, basi unahitaji kuwa mmoja ya wanaume ambao si kuwaza tu bali wanafanya kile wanawake wanahitaji.


Mwanamke anapoongea usimkatishe kwani ndiyo njia pekee ya yeye kuwa karibu na wewe.
 
Kumbuka anapokwambia matatizo yake wakati mwingine hana maana umpe majibu namna ya kutatua (fix the problem) bali anahitaji wewe umsikilize tu na wewe kumsikiliza maana yake unamjali.


Kwa mwanaume fedha ni status hata, hivyo kwa mwanamke fedha ni security, hivyo usiseme fedha zangu, bali sema fedha zetu.
 
Kuna usemi mmoja wa kingereza unaosema:

“Someone is better than no one”

Kwa maana kwamba wapo watu ambao (hasa wanawake wale ambao wanaona muda unaenda bila kuwa na mchumba au mpenzi wa kuwa naye katika maisha) huamua kushikana na bora mwanaume kwa imani kwamba ni heri kuwa na huyo mmoja (unfaithful, untrustworthy) kuliko kutokuwa na mwanaume yeyote.


Subiri kidogo nikwambie!

Kujiingiza kwa mwanaume ambaye moyo wako hauko radhi eti kwa sababu unataka na wewe uonekane una mpenzi au una mchumba au una mume ni kuumiza hisia zako.
 
Hata kama unaamini utafanikisha matakwa yako bila kuunganishwa emotionally, intellectually au affectionally utaishia kuumizwa.


Pia huyo someone ambaye unaona ni afadhari kuliko kuwa mwenyewe ni looser ambaye anakuzuia wewe kumpata anayefaa, kwa lugha nyingine huwezi kumpata mwanaume mwenye sifa njema kama utaendelea kukaa au kushikamana na huyo someone wako ambaye hata hivyo ana sifa ovyo.

Wengi wanajuta kwa sababu ya kuamini kwamba "someone is better than no one, hata hivyo waliokiri kwamba "no one is better than a relationship that lack respect" wanapeta.
 
Watu tunatofautiana katika mitazamo kuhusu fedha, baadhi huiangalia fedha kwa jicho la kutoa (giving) na wengine kwa jicho la kuitunza (saving) na wengine kutumia (spending)

Kama wewe ni kijana wa kiume au kike ambaye upo katika harakati za kusaka mwenzi wa maisha basi ni muhimu sana kuwa na makubaliano au kufahamu mtazamo wa huyo mtarajiwa kuhusu fedha.
 
Judy ni mwanamke ambaye mume wake Jeffy akipata mshahara huamuriwa akabidhiwe na anachofanya ni kugawa zile pesa na kuziweka kwenye bahasha tofauti tofauti, bahasha moja kwa ajili ya kununua chakula, bahasha nyingine usafiri, nyingine pango la nyumba, nyingine kununua nguo na nyingine sadaka kanisani na nyingine kwa ajili ya dharura.


Mume akitumia pesa kutoka moja ya bahasha lazima aeleze ni bahasha ipi alichukua pesa, na amefanyia kitu gani, na risiti ziko wapi na change zipo wapi na duka gani alienda kununua na alikuwa na nani na ametumia usafiri gani na amelipa kiasi gani.

Jeffy hujikuta oppressed, frustrated na hawezi kuvumilia tena!
 
Je, unadhani hiyo ndoa itadumu kwa muda gani?


Kumbuka wengine hutumia pesa kama emotional agenda, kama kwenye huo mfano bahasha za Judy si bahasha tu bali ni mfuko anaotumia ku-mcontrol Jeffy.

Kuna watu walitembelea ndoa moja na ilikuwa ni summer time na joto lilikuwa limepanda nyuzi 40 centigrade.

Ikafika mahali watu wakawa wana sweat utadhani wapo ndani ya sauna wakati huohuo nyumba ilikuwa na viyoyozi vya uhakika ila vimezimwa kwa utaratibu kwamba hadi ifike tarehe iliyowekwa ndipo huwashwa.
 
Wanandoa walipoulizwa kwa nini kuzima wakati joto linatuua, wakawajibu tarehe tuliyoweka kuwasha viyoyozi haijafika bado na kuwasha sasa ni matumizi mabaya ya pesa.

Hawa wanandoa wanafurahia ndoa yao kwa kuwa wanamtazamo sawa kuhusu fedha na hakuna kulemba!

Kuna wanawake ambao kwao fedha za mume ni za familia, na pesa zake ni zake.

Hii ilitokea kwa Suzy na Simon wakati fulani ambapo Suzy alikuwa anafanya kazi na Simon naye alikuwa anafanya kazi.
 
Simon akipata mshahara, Suzy humkomalia na kupanga bajeti namna ya kutumia hizo fedha kwani anachojua ni kwamba mshahara wa mume ni wa familia na mshahara wake ni kwa ajili yake tu.

Hata Simon alipotaka kununua kitu kutokana na ule mshahara basi Suzy huja juu kwa kuanza kutoa lecture kwa Simon namna watoto wanavyohitaji nguo na vifaa vingine wakati huohuo yeye Suzy pesa anayopata kazini kwake anaila kisirisiri.
 
Mitazamo kama hii huweza kuharibu ndoa kwa kasi ya ajabu kama dhoruba.

Angalia kwa makini yule unategemea kuwa mke au mume anazielewaje fedha kama unaona mtazamo wake ni wa ajabu ajabu ushauri wangu ni kwamba fikiria kwa makini kabla ya kuchukua uamuzi wa kuwa naye.
 
“Mhubiri Timothy Omotoso alinibaka kanisani tangu nikiwa na miaka 14” Ushuhuda wa Cheryl Zondi mwenye umri wa miaka 22 umewaacha mamilioni ya waumini wa kanisa la Jesus Dominion International nchini Afrika Kusini , wameduwaa wasijiue iwapo wamuamini ”mtume”wao mwenye umri wa miaka 60 au ushuhuda wa kipusa huyo aliyedai alibakwa akiwa mchanga.

Mhubiri huyo raia wa Nigeria anakabiliwa na makosa 97 ya ubakaji na unyanyasaji wa kingono.
Screenshot_20181024-202010.jpeg
 
Kifaa kinachosadikiwa kuwa ni bomu kimebainika kutumwa katika nyumba ya rais wa zamani wa Marekani Bill na Hillary Clinton leo hii, maafisa wa usalama wameiviambia vyombo vya habari nchini Marekani.

Kifurushi kingine kinachoshukiwa kuwa na bomu kimetumwa pia katika ofisi za rais wa zamani wa Marekani Barack Obama.
Screenshot_20181024-202604.jpeg
 
Watu sita waliingia katika duka moja viungani mwa mji wa Charleroi Ubelgiji wakiwa na mpango wa kumuibia.

Mwenye duka akawaambia warudi tena baadaye atakapokua na pesa zaidi, na majambazi hao wakaitikia mwito...Bila kusita watu hao walirejia kama walivyoagizwa na badala ya kuiba pesa wakakamatwa na polisi.

Je majambazi hawa ndio wajinga zaidi Duniani?
Screenshot_20181024-202703.jpeg
 
Asanteeeeeeee hapa ukweli kabisa pamenikuna
Kumbuka anapokwambia matatizo yake wakati mwingine hana maana umpe majibu namna ya kutatua (fix the problem) bali anahitaji wewe umsikilize tu na wewe kumsikiliza maana yake unamjali.


Kwa mwanaume fedha ni status hata, hivyo kwa mwanamke fedha ni security, hivyo usiseme fedha zangu, bali sema fedha zetu.
 
Back
Top Bottom