Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kuna kipindi nilimuuliza mtu, ni kitu gani kinakufanya uwe na furaha, alinielezea jinsi tabia ya furaha inavyoleta usawa ndani ya mwili na akili ya mtu. Tunapokuwa na furaha tunapata afya njema . watu husema tuna ng’aa, ni kweli, tunahisi kama tunang’aa!

Kujisikia huna afya au mgonjwa ni moja ya sababu watu kujisikia wameshushwa moyo , wana huzuni, wana changanyikiwa na hata kuwa na hasira. Dalili za mwili zinaweza kuumiza kichwa , kuumwa na maumivu, tumbo au matatizo ya utumbo, kwenye mwili na kuhisi uchovu.
 
Hizi aina ya misongo hutokea kwa watu maishani mwao kila siku na kwenye afya zao. Kwa hio tutaondoaje haya matatizo ili kuongeza furaha yetu na ustawi wa afya?

Zaidi ya kazi za ubongo inasukumwa na njia ya kula vyakula vyenye mlo kamili vyenye amino acid . Na hii ni pamoja na mtu kujisikia vizuri , homoni kukaa sawa, na ni pamoja na kulala, hali, hamu ya kujamiana, hamu, na tabia za kijamii.
 
1.Kula Whole Foods Kwa Moyo Wenye Furaha.

Baadhi ya vyakula , hasa vile vyenye vitamini na madini , vinaweza kukufanya ujisikie vizuri , sio katika kujisikia vizuri bali huweka sawa homoni zako. Kula mlo kamili,mlo wa vyakula kamili vya nafaka kiasi kidogo cha vyakula vinavyotokana na wanyama ni moja ya chombo kinachotunza hisia nzuri.

Mafunzo yanaonyesha kuwa baada ya vyakula vyenye tryptophan vinapopungua mwilini vinaweza kuleta kutoelewana katika mahusiano mazuri na kuhukumiana wenyewe, kwa hio jitahidi kupata mlo kamili ili kuepuka matatizo na mwenza wako.



Kula mlo wenye mkusanyiko wa mboga za majani na matunda kama nanasi, pamoja na maharage ya soya, oti meal, chia seeds karanga, samaki na dagaa. Epuka sukari, maziwa na vyakula vya viwandani.
 
  • Thanks
Reactions: Obe
2.Fanya Mazoezi Kwa Furaha Ya Mwili.

Mazoezi yanaweza kusaidia kuboresha hali nzuri na kuamsha kiasi cha Serotonin.

Mazoezi ya kawaida pia hukufanya ujisikie vizuri zaidi katika mwili wako, na yanasaidia kupunguza msongo wa mawazo. Kuwa katika hali ya msongo wa mawazo utasababisha mwili kutoa adrenalin na cortsol, vinavyoleta hali ya magonjwa na kuondoa muunganiko .

Hivi hutokea mara nyingi wakati ukiwa kwenye hali ya kutishiwa , kuogopeshwa . kwa hio acha misongo fanya mazoezi kila mara ili uwe na furaha na mwili usiokuwa na magonjwa ya madogo madogo
 
  • Thanks
Reactions: Obe
3.Pata mwanga wa jua kwa ajili ya furaha ya nafsi.

Toka nje.

Mwanga wa jua hufurahisha na kukufanya uwe na nguvu,kwa sababu unaongeza serotonin kwenye ubongo . hasa jua la asubuhi , hata kama upo kazini jitahidi kupata jua la asubuhi . unapojisikia umechanganyikiwa , nenda nje tembea, huko utajisikia tofauti maana utakutana na vitu mbalimbali na watu , mbalimbali.
 
  • Thanks
Reactions: Obe
4.Kwa ajili ya furaha ya ubongo ,

Hakikisha unapata vutamini madini, na vidonge vya kuongeza homoni mwilini, kila asubuhi kama utaweza , vinasaidia kujaza ubongo na kurutubisha immune system yako . kwa ujumla kiakili na kimwili vitakaa sawa . na pia vitakusaidia na kila hali utakayokutana nayo katika mazingira yoyote yale , ya ugonjwa, ya huzuni, ya kuchanganyikiwa kwa sababu ya mambo mengi.

Kujisikia mtu mwenye afya ni kuwa na maana ya Ulimwengu kupata mtu imara na mwenye nguvu. Na sio tu kimwili bali pia kiakili na kihisia , na ni hivyo vitu vitatu ambavyo vinakufanya uwe na afya ya ukweli.



Kuwa na afya nzuri ya mwili itakusaidia kufanya kazi vizuri na hata maisha yako binafsi yatakuwa mazuri.
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Kizazi na Uzao: Macho Tofauti Kuangalia Jambo Moja

Wakati anaulizwa kuhusu namna utawala wake ulivyokuwa, baada ya kuwa amestaafu, rais alhaji Ali Hassan Mwinyi (mwalimu huyu) alisema kila zama na kitabu chake. Kuna ukweli katika hili, kila zama na kitabu chake. Nchi yetu kwa sasa, upande wa idadi ya watu unashuhudia kiwango kikubwa cha ongezeko la watu na la kuvutia zaidi ni idadi kubwa ya vijana ambao hawazalishi (chini ya miaka 15), hawa wanaunda asilimia 45 ya watanzania. Asilimia hii inatekutegemea wewe ulete, yenyewe ikae chini ile na kushiba na uhakikishe umeandaa mazingira mazuri ya kizazi hiki (kizazi cha milenia na kizazi cha uzao Z- kuanzia mwaka 1981 na 1995).

Kuna mammbo ya msingi kujadili sasa, nyumba bora hujengwa kwa ramani na msingi. Tunajiandaa vipi kuhakikisha kizazi hiki kinafurahia kuwepo kwetu sasa (BTW, mimi ni kizazi cha milenia FYI)

Tunaliangaliaje hili suala? Huu ni mjadala unaohitaji utulivu kuujadili na hasa kama tunaona kabisa tunakabiliwa na changamoto za utoaji wa huduma za afya, elimu na ajira. Majuzi tu tumesoma na kuona kuwa bajeti inayotengwa kwa ajili ya huduma ya afya haifiki kikamilifu, inafika kwa chini ya asilimia 40.

Makapuku ni sehemu nzuri kuwepo maana mabadiliko hayaletwi na wapiga kelele bali watu wa uzao tofauti wanaoleta tofauti zao pamoja na kuamua kuzitatua kuliko uzao mmoja unaodhani mawazo yake ndiyo suluhu ya changamoto tunazoziona sasa. This is the beauty of diversity, bringing differences together such that the whole is greater than the sum of its parts. Tunaweza kuwa na uono tofauti wa masuala (different optic) lakini hii haimaanishi kuwa kizazi fulani ni sahihi dhidi ya kingine. na hapa ndipo tunapohitaji kukaa kama taifa bila kujali wewe ni wa uzao gani ili kuja na suluhu ya changamoto za leo, kesho na kesho kutwa.

Kama kuna jipya, unaweza kuchangia chochote nikijiaminisha kabisa wewe ni wa kizazi kinachoiangalia juzi kuiona jana na kikishaiona jana kinaifanyia kazi leo kuiboresha kesho na kesho kutwa salama kwa wote na si wachache wenye kufaidika kwa jasho la wengi kesho kutwa.
 
[emoji120] [emoji120] [emoji120]
FB_IMG_1540350308139.jpg
 
Back
Top Bottom