Makapuku Forum

Makapuku Forum

Siku hizi watu wengi wameelimika , wanafanya mazoezi na kufuata kanuni bora za ulaji, kuliko huko nyuma watu walijua kula vyakula vya mafuta na kupata vitambi ndio afya. kumbe walikuwa wanakaribisha magonjwa bila ya wao kujua.

Leo nakuletea watu ambao wanapenda kufanya diet lakini wanajikuta bado wanaongezeka uzito.. kuna wale ambao hawali vyakula vizuri siku za kazi , yaani siku za week. lakini siku za weekend wanakula zaidi vyakula mbalimbali kama kukomoa vile. na hii imekuwa ni mtindo wa maisha ya watu wengi hapa mjini.

Hupungua wakati wa siku za kawaida na kuongezeka siku za weekend, kwa kula nyama choma , pombe nyingi ilimradi kulipiza zile siku za kawaida za diet. sasa hapo unafanya nini?
 
Hebu tuangalie hizi tips zifuatazo huenda zikakusaidia kuacha kula sana wakati wa weekend.

1.Jitahidi Kula Chakula cha kawaida siku za kawaida.

kula chakula kama kawaida siku zote, lakini tumia akili ya kuchagua chakula unachokula. tena kula wakati ukiwa na njaa, usile kama hauna njaa, kwa sababu watu wengi eti kwa sababu ni saa saba wakati wa Lunch basi na yeye anaenda kula , wakati hana njaa.



Kula chakula ambacho moyo wako unatamani kula kwa kiasi sana.
 
2.Usiseme leo sili bila sababu.

kama hukufunga kula chakula chako vizuri kwa wakati maalum. lakini kama umefunga hakuna madhara yeyote yatakayokutokea. kama unakula kupita kiasi , na kila ukila unajilaumu acha kula kwa mtindo huo. kula kwa kiasi. Unajua nini, usipokula siku nzima , halafu ikifika wakati ambao umetaka kula ni lazima utakula zaidi ya kipimo.

3.Jiwekee Sheria Rahisi.

Weka sheria wewe mwenyewe, kwamba hivi vyakula sitakula na hivi nitakula. na uifuate hio sheria kweli kweli. kula chakula inapobidi ili usije kulipiza wakati wa siku za mapumziko.
 
4.Tafuta Sababu Inayokufanya Ule Kupita Kiasi.

Kuna sababu nyingi za kumfanya mtu ale chakula kupita kiasi, wengine wakiwa kwenye sherehe mbalimbali hula kupita kiasi, lakini kuna wale ambao hula kwa sababu ya kupatwa na matatizo kama vile Hasira, Huzuni, Mawazo mengi, upweke nao husababisha watu kula sana na hata wengine wanaofanya mazoezi hutaka kula sana hasa mazoezi mazito.



Lakini kuna watu wengine wakati wa matatizo hawali kabisa, hawa watu sasa hupatwa na matatizo ya vidonda vya tumbo. lakini hata hivyo, hizo sio sababu pekee ya kukufanya wewe ule kupita kiasi, tafuta sababu yako.
 
5.Ukiwa Upo Nyumbani siku za weekend tafuta kazi za kufanya ili uwe bussy.



Ili akili yako isifikirie kula chakula kila wakati, kuwa bize na shughuli za nyumbani , fanya usafi kuzunguka nyumba yote, soma vitabu, nenda matembezi. lakini kama ukikaa na kuangalia tamthilia utakula sana, usitumie pombe, pombe ina calories nyingi haitakusaidia kupungua uzito na diet yako itakuwa ni bure.

Epuka kutumia pombe. ukifuatilia hizi tips zitakusaidia kupunguza nafasi ya kula zaidi, iwe siku za kazi au za kawaida, na ukumbuke kuwa hii sio njia pekee , zipo nyingi. jitahidi kutafuta zile ambazo zitakusaidia.
 
Unatafuta chakula kizuri cha kukuvutia kwa ajili ya kulala usingizi mzuri? Usitafute mbali, Ndizi ziko kila mahali unapopita , kwenye magenge, sokoni, na supermarket

Unashangaa? Hata mimi nilishangaa pia.

Nilipokuwa nataka kula Ndizi kawaida nilikuwa nakula asubuhi tu kwa ajili ya kuongezea breakfast yangu iwe na uzito , lakini mbinu ya kula ndizi usiku, saa moja au mawili kabla ya kwenda kulala ili chakula kiyeyuke vizuri tumboni. Virutubisho vya ndizi vinasaidia kuleta usingizi murua na kupata ndoto nzuri . hii ni moja ya hatua muhimu ya kulala , na husafisha vitu vyote ulivyokusanya tumboni kwa siku nzima.
 
1.Zina Magnesium Ya Kutosha.

Watu wengi wamepungukiwa na magnesium na hata hawajui kuwa wamepungukiwa. Nashauri kabisa kwenda kwa dactari wako kupima kiasi cha magnesium ulichonacho. Dalili za kawaida kujua kama umepungukiwa na magnesium ni kuwa maumivu ya miguu wakati wa usiku, digestion yako kwenda polepole, na kutokupata usingizi mzuri, unakuwa unahangaika kutafuta usingizi kwa dawa. Lakini usiogope, Ndizi zipo na zina full magnesium kuliko hata matunda mengine.

Vyanzo vingine vya kupatikana kwa magnesium ni kula mbegu za maboga, na karanga.
 
  • Thanks
Reactions: Obe
2.Zina Potassium Ya Kutosha.

Hiki chakula cha nguvu na kinachopatikana kwa urahisi kina virutubisho vingi tunavyohitaji .potasium inakamilisha magnesium ili kuboresha kupata usingizi mzuri na kusaidia digestion pamoja na kurahisisha msukumo wa damu.msukumo wa damu yako kwa kawaida unatakiwa uwe wa kawaida hata usiku , na hii ni dalili ya kuwa na afya ya moyo. Ukiwa na kiasi cha chini cha potassium inaweza kuchangia maumivu ya misuli na moyo kutokuwa na msukumo mzuri.

Vyanzo vingine vya vinatokana na parachichi, broccoli na uyoga.
 
  • Thanks
Reactions: Obe
3.Zinaweza Kusaidia Kiasi Cha Amino Acid.

Amino acid na ikiwa ni mtangulizi wa serotonin na melatonin, (maneno ya kitaalamu haya) – vyote vina umuhimu kwa afya ya usingizi wa usiku.Serotonin inarekebisha na kudhibiti hali yako , wakati melatonin inarekebisha sikadiani ya mfuatano wa mwendo. , inayoshawishi, inayoshawishi homoni tunazotoa kila siku mchana na za usiku.

Vyanzo vingine vya Amino Acid ni pamoja na chia seeds, viazi vitamu, almonds, na majani ya kijani kabisa , kama spinachi.
 
Back
Top Bottom